STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, July 4, 2014

Algeria waoinyesha mfano wa kuigwa

KATIKA mafundisho ya Qur'an na Hadithi za Mtume Muhammad (SAW) inasema Muislam ndugu na Uhurumiana wenyewe kwa wenyewe.
Hiyo imethibitishwa na timu iliyoonyesha soka la kusisimua nchini Brazil, Algeria iliyong'oka kishujaa mbele ya Ujerumani.
Mshambuliaji nyota wa timu ya taifa ya Algeria Islam Slimani aliyepo kwenye orodha ya wafungaji bora akiwa na mabao mawili amebainisha kuwa kikosi kizima cha nchi hiyo kinatarajiwa kutoa msaada wa posho zao kwa watu wa Gaza. 
Timu ilirejea nyumbani wakiwa mashujaa na wachezaji wameamua kutoa posho zao kwa wale ambao wanazihitaji zaidi, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa miongoni mwa Ibada ndani ya Uislam.
Hatua hiyo ya Algeria imekuja huku wawakilishi wengine wa Afrika katika michuano hiyo kama Ghana, Nigeria na Cameroon kukumbwa na msuguano katika kambi zao kutokana na posho hatua iliyochangia kwa kiasi kikubwa kuenguliwa mapema.
Algeria ni nchi ya Kiislam iliyopo Kaskazini mwa Afrika na inaelezwa kufungwa kwa mabao 2-1 katika hatua ya lala salama na Ujerumani ilitokana na swaumu.

No comments:

Post a Comment