STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, March 12, 2014

Askari Magereza amuua mwenzake kinyama

ASKARI wa magereza wa jela la Taveta Boniface Muriithi amemuua kwa kumpiga risasi mwenzake kwa jina Livingstone Sowene.
 
Tukio hilo limetokea leo saa mbili asubuhi ya Jumanne lilitokea nje ya gereza hilo wakati Muriithi alipoamua kummiminia mwenzake risasi tano kwenye kifua bila kumuuliza chochote.

Wawili hao hata hivyo wamekuwa na uhasama ambao unadaiwa kuzidi baada yao kupangwa wafanye kazi katika shifti moja.

Mkuu wa gereza hilo Bw Soud Ramadhan amethibitisha kisa hicho na kusema kuwa wamemnasa mwenzao huyo na kumkabidhi kwa polisi ili afunguliwe mashtaka.

“Muriithi alimkuta Sowene akisubiri kupeleka wafungwa kazini alipompiga risasi tano kifuani, alikufa akiwa ameketi papo hapo. Ni jambo la kushangaza kwa hata hawakuongea ndiposa tujue kama palikuwepo uhasama wowote,” akasema askari huyo. 

Duru hata hivyo zinasema mshukiwa alijawa na ghadhabu baada ya kupashwa habari kwamba askari huyo alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na mumewe.

Jamii na rafiki wa marehemu wamelalamika kumpoteza mmoja wao kwa njia katili ya kuangamizwa na mfanyakazi mwenzake.

Babake marehemu Bw Joseph Sowene amesema kuwa mwanaye aliamkia kumpeleka bintiye shuleni na mkewe shuleni Makloriti anakofunza. 

“Tumetatizika pakubwa kwa kuwa aliyeuawa ni mzazi mchanga aliyejali sana jamii yake. Hatujui kilichosababisha hili na tunataka polisi watuambie kilichotokea,” akalalama mzazi.

Mkuu wa polisi wa Taita Taveta Richard Bitonga alithibitisha kisa hicho na kusema uchunguzi unaendelea kubaini kiini hasa cha mauaji hayo.


Mshukiwa anazuiliwa katika kituo cha polisi cha Taveta akisubiri kufikishwa mahakamani karibuni.

Crd: Paparaz.

Breaking News! Majambazi wanaswa wakijiandaa kufanya tukio Mbagala

http://www.mwanakijiji.com/overance/uploads/2013/11/SelemanKova.jpg
HABARI zilizotufikia muda huu zinasema kuwa Watu wawili wanaosadikiwa kuwa majambazi wamenaswa na jeshi la Polisi wakijiandaa kufanya tukio eneo la Mbagala-Dar es Salaam.
Taarifa hizo zinasema kuwa majambazi hao walinaswa wakiwa kwenye pikipiki yenye namba za usajili T 225 CQC aina ya Kapor baada ya kushtukiwa.
Inaelezwa wakora hao walinaswa wakiwa na silaha wakijiandaa kufanya uhalifu katika kituo cha kuuza mafuta cha Oilcom kilichopo Kongowe-Mbagala, jijini Dar! 
Majambazi hayo yametiwa mbaroni na askari polisi zaidi ya kumi waliokuwa wamevalia nguo za kiraia wakiwa na magari aina ya Land Cruiser yenye namba za usajili T 148 AEN na T 848 AGF!
Tukio hili limekuja siku moja baada ya jana jeshi hilo kuwanasa watu wengine wanaodaiwa kuwa majambazi kwenye kituo cha mabasi cha Ubungo wakijiandaa kufanya uhalifu.

Yanga warejea toka Misri, Simba wawapa dole!

Yanga
WAKATI kikosi cha Yanga kilichotolewa kishujaa katika Ligi ya Mabingwa ya Afrika dhidi ya Al Ahly ya Misri, kikirejea nchini kutoka Cairo, watani zao Simba wamewapongeza kwa kiwango cha soka walichoonyesha mbele ya watetezi wa michuano hiyo ya Afrika.
Yanga iling'olewa kwa mikwaju ya penati 4-3 na watetezi hao baada ya kukubali kipigo cha 1-0 katika dakika 90 na kulingana magoli baada ya mechi ya kwanza wenyewe kushinda nyumbani idadi kama hiyo iliwasili leo na kupokewa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe Said Mecky Sadiq.
RC huyo aliapongeza wachezaji na viongozi wa Yanga kwa namna walivyoipigania Tanzania, ingawa bahati haikuwa yao huku akiwataka wanaowasakama wachezaji hasa Said Bahanuzi kuacha jambo hilo kwa madai hata mastaa duniani hukosa penati na bado wanapongezwa na wadau wao.
Katika hali isiyotarajiwa Katibu Mkuu wa Simba, Ezekiel Kamwaga amenukuliwa akiwapongeza watani zao kwa mchezo waliouonyesha ugenini licha ya kushindwa kufikia rekodi yao ya kuwang'oa watetezi wa taji la Afrika,
Kamwaga alisema kila mtu ameona watani zao walivyopigana ingawa hawakuwa na bahati ya kupenya hatua hiyo na Simba kama wadau wengine wa soka wanapongeza na kuwakarisha kwenye ligi kuu.

Samuel Sitta ashinda kwa kishindo Uenyekiti Bunge la Katiba

http://www.dar24.com/wp-content/uploads/2013/05/sitta.jpg
Mhe Samuel Sitta
WAJUMBE 487 kati ya 563 wamemchagua Mbunge wa Urambo Mashariki na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta kuwa Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba.
Sitaa aliyekuwa akipewa nafasi kubwa ya kushinda katika king'anyiro hicho alimwangusha mpinzani wake, Hashim Rungwe aliyeambulia kura 69, huku kura 7 ziliharibika katika uchaguzi uliofanyika jioni hii.
Kabla ya zoezi la kupigwa kura Mwenyekiti wa Muda wa Bunge hilo, Pande Ameir Kificho aliwatangaza wagombea hao na kuwapa nafasi ya kujieleza kwa wajumbe ambapo Mzee Sitaa alifunika kwa kusisitiza kuwa falsafa yake ya Standard and Speed ipo pale pale katika kuihakikishia Tanzania inaopata Katiba Mpya na yenye kiwango kwa mujibu wa matakwa ya wananchi.
MICHARAZO Inampa heko zake Mhe Sitta na kumtakia kila la heri katika kazi yake hiyo kwani ni wazi wajumbe na watanzania kwa ujumla wanamuamini kutokana na ufanisi wake serikali na alipokuwa Mbunge wa Bunge la Tanzania.

Huu si wivu bali unyama na unyanyasaji

http://www.ippmedia.com/media/picture/large/shilogile-aug31-2013.jpg 
Na Mariam Kamgisha, Morogoro
MWANAMKE mmoja Juliana Wambura (24) mkazi wa kijiji cha Ruaha, ameuawa kwa kuchomwa kisu tumboni na mumewe.
Akizungumzia tukio hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Faustine Shilogile, alisema lilitokea juzi saa 2:00 usiku katika kijiji cha Ruaha tarafa ya Mikumi wilayani Kilosa.
Alisema marehemu aliuawa kinyama kwa kuchomwa na kisu tumboni  na mumewe  aliyefahamika kwa jina la  Fredi Ernest (34) mkazi wa Shirati Mara  na kupelekea utumbo wa mkewe kutoka nje.
Alisema chanzo cha mauaji hayo ni wivu wa mapenzi na mtuhumiwa baada ya kutekelea mauaji hayo amekimbia.
Katika tukio jengine alisema alisema Machi 8 mwaka huu saa 1:30 asubuhi, Gerry Joseph (23) alifariki dunia baada ya pikipiki aliyokuwa akiiendesha  kugonga mti.

Aidha alisema katika tukio jengine  gari aina ya Scania lililokuwa likiendeshwa na Juma Saidi (30) mkazi wa Dar es Salaam lilimgonga mtembea kwa miguu mwanamme asiyefahamika na kumsababishia kifo.

Sitta njia nyeupe Uenyekiti Bunge la Katiba

Samuel Sitta akiwa na fomu ya kuwania nafasi ya Uenyekiti Bunge Maalum la Katiba
WAKATI uchaguzi wa Mwenyekiti wa kudumu wa Bunge Maalumu la Katiba ukitarajiwa kufanyika leo, wagombea wawili waliojitokeza kutaka kuwania nafasi hiyo, wameenguliwa baada ya ya kushindwa kurudisha fomu ya kuwania nafasi hiyo kwa muda uliopangwa

Wajumbe hoa Dk Theria Uvisa pamoja na Danstan Chipaka walienguliwa katika kinyang’anyiro hicho kufuatia kushindwa kurudisha fomu za kugombea ambazo zilipaswa kurudishwa leo saa 4 asubuhi.

Kufuatia kuenguliwa kwa wajumbe hao, nafasi hiyo itawaniwa na Samwel Sitta pamoja  na Hashim Rungwe ambao ndiyo waliokidhi vigezo kwa kuchukua fomu na kurudisha kwa wakati.

Uchaguzi wa Mwenyekiti unatarajiwa kufanyika leo saa 10 jioni, ambapo baada ya kutangazwa matokeo kutatangazwa uchukuaji fomu kwa wajumbe watakaotaka kuwania nafgasi ya umakamo mwenyekiti.

Mpaka sasa anayetajwa kutarajiwa kuwania nafasi hiyo ya Makamu Mwenyekiti, ni Samia Suruhu.

Kwa mujibu wa kanuni za Bunge Maalumu la Katiba, Makamu Mwenyekiti wa Bunge anapaswa kutoka upande wapili wa muungano iwapo Mwenyekiti atakuwa amechaguliwa kutoka upande mwingine wa muungano hili kuleta usawa.
FK

TANZANIA BILA DAWA ZA KULEVYA INAWEZEKANA?!


KATIKATI ya mwaka jana iliyowahi kuchapishwa barua iliyoandikwa na kusainiwa na baadhi ya wafungwa wa dawa za kulevya waliopo China. Katika barua yao hiyo waliwataja baadhi ya wahusika na biashara hiyo waliopo nchini kwa majina yao na kumgusa mmoja wa Wabunge wa Tanzania, Mhe. Idd Azan ambaye alikanusha taarifa hiyo na kuapa yu tayari apigwe risasi hadharani kama atabainika anahusika.
Wakati hilo likiwa limesahulika, mfungwa mwingine ametuma barua akisisitiza kuwa Tanzania Bila Madawa ya Kulevya Inawezekana iwapo tu vigogo wahusika na biashara na mtandao huo watashughulikiwa kivipi?
Isome barua ya mfungwa huyo kama ilivyo;

DRUG FREE TANZANIA IS POSSIBLE

I write this letter on behalf of the Drug Free Tanzania Movement (Tanzanian Prisoners in Hong Kong jails). Today I write to you inspired by Dr. Harrison Mwakyembe “One of the men of goodwill in our current government”, with his renowned dedication and strong determination to dismantle drug trafficking networks in our nation. I also write on behalf of all men of goodwill to whom beauty is truth and truth and who eyes the beauty of genuine Drug Free Tanzania is more precious than silver or gold or diamond. My fellow compatriots, drug trafficking is still a fact in Tanzania. We must keep on building the momentum, we must keep up our campaign until next national election in 2015. We must keep revealing all those who involves in this illicit trade (from civilian, businessmen/women, law enforcement personnel and politicians). We must keep on confronting drug trafficking in its hidden and subtle forms.

Brethren, I am mindful that democracy as defined by Abraham Lincoln “is the government of the people, for the people and by the people”, and I am also mindful that if democracy is to live in our nation, politicians and their associates who involves in this Evil trade must be wiped and out of the Tanzania Political Map. If democracy is to live in our nation, drug trade must die, because democracy is people’s power and we (people) are not unmindful that drug trade is the universal Evil and anyone who associates himself with this Evil is an agent of the Devil. And since the ripple effect of drugs to our community as well as the international community is incalculable, we must eliminate all devil agents and their associates and their family members in our political map.

Every attempt to end our campaign by intimidation, by encouraging fellow inmates to inform, by using death threats toward us and our loved ones further cemented our campaign and brought sympathy for our cause from men and women of goodwill all over the nation.

The great appeal for the nation appears to lie in the fact that we (Tanzanian inmates in HK jails – “The Victims of the illicit trade”) have decided to break our silences and pray that The Almighty God shall give us strength to remain committed to this cause though we may face death.

We dared to dream of a better day in the midst of our sufferings and the nightmare that surrounded us. We have unequivocally declared our hatred for this most colossal of all Evils and we have publicly name and shame our ex-paymasters “the Drug Barons” most of them top brass businessmen and women, politicians, their associates and even law enforcement personnel. We have condemned all crooked politicians regardless of their political parties since we are not politically affiliated with any party.

When we started our campaign most of our brethren they told us we wouldn’t get here. They told us we cannot stop even a single Tanzanian courier coming into Hong Kong, Macau and the Mainland China. But it is now week twenty six (26) not a single Tanzanian courier has been arrested for drug trafficking here in Hong Kong Airport. (What a record? It was hardly to pass a week without several arrests).

And there were those who said that we would get here only over their dead bodies. All the nation knows that we are here and we aren’t going to let nobody turn us around.

So I write you today with the conviction that the illicit trade is on its death bed in Tanzania and the only thing uncertain about is how costly the drug barons and their political backers will make the funeral.

My dear fellow compatriots. Listen! The battle is in our hands. The battle is in our hands in Dar es Salaam, Dodoma and all over the United Republic of Tanzania. So let us be more than ever committed to this cause for better Tanzania. Let us march on the ballot boxes until all bad corrupted and drug related leaders disappear from the political arena. Let us march on the ballot boxes until those politician and their associates who has been barred from entering the United States for drug trafficking allegations and money laundering tremble away in silence.

Let us march on the ballot boxes, until we send to our Municipal councils and the House of parliament councilors and MP’s men and women who will not fear to do justice and walk humbly with their God.

Brethren, there are no broad highways to lead us easily and inevitably to quick solutions. We must keep going. We must be extremely vigilant with the drug enforcers and we must keep on spreading the news (about the dangers of trafficking drugs into HK, Macau and the Mainland China) to our fellow compatriots and we must keep on naming and shaming the Drug barons and their associates. And we shall not let anybody turn us around until we have a drug trafficking free society.

Your fellow compatriot languishing in Hong Kong jail.

Name: withheld Alias: Mckenga (TZA-Prisoner)

Date: 19-02-2014


Credit:Brother Danny

Wenger amponda Arjen Robben kwa udanganyifu

Arsenal's Laurent Koscielny (right) fouls Bayern Munich's Arjen Robben in the penalty area (PA Photos)
Arjen Robben akiwa amenguka ndani ya eneo la penati la Arsenal mbele ya Laurent Koscielny
MENEJA wa Arsenal, Arsene Wenger amemponda winga nyota wa Bayern Munich, Arjen Robben kwa madai ya udanganyifu wa kujirusha ili kushawishi marefa kuipa penati timu yake.
Mfaransa huyo alisema kuwa Robben licha ya kuwa bonge la mchezaji anayemkubali, lakini pia amemsifia kuwa ni hodari wa kujirusha baada ya jana kuhusika na tukio la kujirusha langoni mwa Arsenal ili kushawishi penati kama alivyofanya kwenye mechi ya awali mjini London, japo penati hiyo ilikoswa.
Katika tukio hilo la awali, Mholanzi huyo alisababisha kipa wa Arsenal Wojciech Szczesny kutolewa nje ya dimba kwa kadi nyekundu kwa kile kilichoonekana kumchezea rafu mbaya Robben.
Jana winga huyo alirejea tena na kuipa timu yake penati dakika za lala salama ambayo ilipotezwa na Thomas Muller na kuinusuru Arsenal kuchezea kicha pili mfululizo kwa Bavarians hao ambao hata hivyo wamesonga mbele.
"Siwezi kupinga, Robben ni bonge la mchezaji, ila ni mjanja wa kulazimisha mambo kwa kupenda kwake kujirusha mbele ya mabeki ili aonekane kachezewa vibaya, haivutii," alisema Wenger baada ya mechi ya jana dhidi ya Bayern Munich, ambapo winga huyo alionekana kama kachezewa rafu na Laurent Koscielny.
Wenger alisema kama marefa wangekuwa wakimpa kadi ya njano, hadhani kama angerudia mchezo wake huo ambao alidai unapoteza mvuto wa soka kwani ni udanganyifu unaoziumiza timu nyingine wakati mwingine.

Manny Pacquiao nouma amchakaza Hatton

Pacquiao (kushoto) akimtandika mpinzani wake
MOJA ya pambano kali la kusisimua kabisa lilifanyika usiku wa kuamkia Jumapili ya Mei 3, 2009 huko Marekani kwenye ukumbi wa Las Vegas kati ya bondia Manny Pacquiao 'The PacMan' na Ricky Hatton maarufu kama Hitman.
Pacquiao alianza pambano hilo kwa kasi akishambulia ngumi lakini kwa tahadhari kubwa dhidi ya Hatton, ambaye si bondia wa kumtabiria, masabiki walikuwa wakipiga kelele kwa kushangailia wakati wote.
Kadiri randi ilivyokuwa ikisonga mbele ndivyo Pacquiao alivyokuwa akishambulia kwa kasi na kuonyesha ubora wa hali ya juu, alkuwa akipiga ngumi za kudonoa yaani 'jab' kali na kwa hesabu za hali ya juu na kufanikiwa kupenyeza ngumi nyingi kwa 'Hitman' akitumia jab na ngumi mkunjo za kulia yaani 'right hooks'.


Katika raundi hiyo ya kwanza Pacquiao alimkamata Hatton mara tatu kwa right hok zake kali zilizotua barabara katika kichwa chake na 'kumpotzea' kabisa Hatton katika raundi hiyo ambapo alikuwa akijitahidi kukwepa bila mafankio makubwa.


Ukingoni mwa raundi hiyo Hatton naye 'akazinduka' na kurusha makombora kadhaa kwa Pacquiao na kumfanya alalie kamba, Hatton mzaliwa wa Manchester akambana Pacquio na kumshambulia kwa right hook na left hook ambazo hata hivyo nyingi ziliishia katika mikono ya
Pacquiao.
Hatton akaendelea kumbana Pacquaio kweny kamba lakini mpinzani wake huyo akawa anatumia ngumi ndefu za kati aipiga tumbo na kifua na moja moja akitumbukiza katika uso wa Hatton na ngumi zote zilimwingia Hitman.


Ndipo ghafla alipojinasua kwenye kamba na kupiga ngumi mkunjo kali ya kulia yaani 'right hook' na Hitman akadondoka chini kama mzigo wa kuni katika raundi hiyo ya kwanza.


Umati ukalipuka kwa shangwe na hasa mashabiki wa Pacquiao, Hatton akajizoa chini na mwamuzi akamuhesabia hadi 8, akapanguza glavu zake na kusema yuko fit kuendele anapambano zikiwa zimesalia sekunde 46 raundi ya kwanza kumalizika.


Mwamuzi aliporuhusu tu pambano, Pacquaio hakukawia akamfuata kwa kasi Hatton na kumsukumia 'right hooks', na jabs za nguvu na ngumi nyoofu ya kushoto au 'straight lefts'.


Hatton kwa uzoefu wake akajaribu kujikinga lakini hakuweza kukinga ngumi zote kwani ngumi 5 zilimkamta barabara na kumfanya aone' double double' na ndipo Pacquio akakaza musuli wa mkono wa kushoto na kumtandika Hitman, ngumi kali iliyomwelemea na kujikuta akidondoka tena chini kwa mara ya pili katika raundi ya kwanza.


Ilikuwa ni bahati kwake wakati anakwenda chini zlikuwa zimesalia sekunde 7 na hivyo alivyoanza kuhesabiwa raundi ikawa imemalizika na ikawa ni dhahiri Hatton ameokolewa na kengele, mabondia wote wakaenda kwenye kona zao kufuta pumzi.


Raundi ya pili ilipoanza, Hatton alianza kwa kurusha jab zake nyingi na kutumia zaidi 'left hook' ambazo kadhaa zilimpata Pacquiao ambaye wakati fulani pamona na kupigwa ngumi za nguvu kichwani na kuonekana kulewa, lakini alikuwa na nguvu kiasi cha kushindwa kudondoka.


Pacquiao akawa anatumia ngumi za mnyooko yaani 'straight punch' , kisha akapiga jab ya kushoto akapiga tena ngumi ya kulia na kwa kasi ya ajabu, akaachia ngumi kali ya kushoto iliyompata Hatton na kumpeleka sakafuni.

Ngumi hiyo ilipigwa katikati ya ulingo wakati raundi ya pili inaelekea ukingoni, Hatton akajitutumua kujizoa pale chini kwa nia ya kutaka kuendelea kupigana kama alivyofanya kwenye raundi ya kwanza.

Akamudu kusimama kwa mbinde, mwamuzi akaruhusu pambano kuendelea baada ya kuwa amemhesabia Hatton naye kujibu kuwa ataendelea, Pacquiao hakukawia, akamfuata tena na kumcharaza konde kali la mkono wa kulia na Hatton akadondoka tena chini kama zigo la nyanya.


Safari hii mwamuzi Kenny Bayless hakujisumbua tena kumhesabia Hatton baada ya kumuona akihema kwa nguvu akiwa amelala chali na wala kutokuwa na dalilia ya kunyanyuka mapema, alibaki akipepesa macho pale chini.


Pambano likawa limemalizika katika raundi ya pili na Manny Pacquiao akawa bingwa kwa kumpoka ubingwa Hatton, akajiwekea rekodi ya mapambano 49 akipoteza 3 sare 2 huku 37 akishinda kwa KO na kuifanya rekodi ya Hatton iwe mapambano 45 akipoteza 2, huku 32 akishinda kwa KOs. Hakika hilo lilikuwa ni moja ya pambano bora la KO.

Hawa ndiyo wachezaji 10 wa Kiafrika wanaolipwa vyema

WAKATI Cristiano Ronaldo akitajwa kuwa mchezaji tajiri duniani akimfunika aliyekuwa akiishika nafasi hiyo kwa muda mrefu, David Beckham, pia akiwa ndiye mchezaji anayelipwa vyema duniani akiichezea Real Madrid.
Hata chini ni orodha ya wachezaji wanaovuta mkwanja mrefu katika klabu zao ambapo orodha hii imeanza na namba 10 kwenda namba moja.
John Obi Mikel HDTV Wallpaper
10. John Obi Mikel – $6.1 million

Nigerian John Obi Mikel joined the Premier League Club in 2006 to play midfielder for Chelsea, and has had an extremely successful career since. He has played for the Nigerian national team in the African Cup of Nations and FIFA World Cup in recent tournaments, and almost won the African Footballer of the Year Award in 2012.
http://1000goals.com/football-pictures/file/43/1600x1200/crop/michael-essien-wallpaper-real-madrid.jpg
9. Michael Essien – $6.9 million

Beginning his career with the Liberty Professionals in his home country of Ghana, Michael Essien burst onto the international stage when played for SC Bastia in France for several seasons. He joined Chelsea in 2005, and is on loan this season to Real Madrid. Essien has helped represent Ghana in numerous international competitions, including three African Cup of Nations tournaments and the FIFA World Cup.
http://e1.365dm.com/13/02/504x378/ChrisSambaQPR_2894520.jpg
8. Christopher Samba – $7.5 million

Congolese defender Christopher Samba moved around a fair amount early in his career, playing in the Premier League (with the Blackburn Rovers and Loftus Road), as well as for the Russian team, Anzhi Makhachkala. Earning more than $160,000 per week, Samba easily makes the list of highest-paid African footballers, and has helped represent Democratic Republic of the Congo in many international competitions.
http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2013/10/29/article-2479272-1824A2D100000578-997_634x476.jpg
7. Kolo Toure – $7.8 million

Ivorian Kolo Toure makes his living playing for Liverpool, though he got his start in Arsenal, where he played for seven years. He made more than 100 appearances for the Côte d’Ivoire national team, playing in the African Cup of Nations and FIFA World Cup tournaments. He also has a lucrative endorsement deal with Adidas to add to his already formidable salary. Toure’s younger brother, Yaya, also plays for the Côte d’Ivoire national team — and earns a lot more! Read on.

http://www.soccerwallpaper.mackafe.com/var/albums/Fr%C3%83%C2%A9d%C3%83%C2%A9ric-Kanout%C3%83%C2%A9-Wallpaper-Gallery/kanoute_goal_happy.jpg
6. Fr̩d̩ric Kanout̩ Р$8.4 million

Malian Frédéric Kanouté has played for the Chinese club Beijing Goan since June 2012, though he made a name for himself earlier playing for Lyon, West Ham, and Sevilla in Europe. He has played in three consecutive African Cup of Nations tournaments, and is consistently one of the most popular football players in Mali.
http://en.africatopsports.com/wp-content/uploads/2013/09/Emmanuel-Adebayor1.jpg
5. Emmanuel Adebayor – $13.5 million

Togo striker Emmanuel Adebayor has made his name in the English Premier League, playing for Arsenal and Manchester City before landing on his current team, Tottenham, in 2011. He is considered one of the most charitable athletes out there, committed to numerous projects around the world and particularly in his native Togo. Most notably, he started the SEA Foundation, a charity that helps to run educational, economic empowerment, and healthcare projects around Africa.

4. Seydou Keita – $16.2 million

Malian midfielder Seydou Keita currently plays for the Chinese Super League club Dalian Aerbin FC, though he originally made it big during his four-year career with Barcelona. He is captain of the Malian national team and has helped represent his home country quite well in numerous African Cup of Nations tournaments.

http://foreverwestham.com/wp-content/uploads/2014/02/Didier-Drogba.jpg
3. Didier Drogba – $17.5 million

Ivorian star Didier Drogba is the all-time top scorer for the Côte d’Ivoire national team, and has lent his talents to various teams throughout his career. Finding stardom initially in the English Premier League in Chelsea, he then moved to the Shanghai Shenhua FC and finally to Galatasaray, where he plays now in the attacker position. Making more than $20,000 per match, his net worth only expands with the numerous endorsement deals he also has.
Yaya Touré
2. Yaya Toure – $20 million

The brother of aforementioned Kolo Toure, Yaya Toure earned $20 million in 2013, making the Toure brothers the highest-paid siblings in African sports. Playing midfielder for Manchester City, he developed an enormous fan base for his physical power and crystal clear technique. Earlier in his career, Toure played for youth clubs in Côte d’Ivoire before heading to Europe to play for the likes of Baveren, Olympiacos, and Barcelona.
Samuel Eto'o - Chelsea FC - 2013/14 Champions League matches for Chelsea.
1. Samuel Eto’o – $27 million

Perhaps the most recognized name in African sports, Cameroonian striker Samual Eto’o pulled home $27 million in 2013 playing for the Russican club Anzhi Makhachkala, though he recently signed a contract to play for Chelsea for the upcoming year. He brought his talents to various teams through the course of his career, including Real Madrid, RCD Mallorca, and Inter Milan, and has won African Player of the Year four times. He has helped represent Cameroon in numerous international competitions, and is on track to do so again this summer at the 2014 FIFA World Cup in Brazil.

Arsenal majanga, Ozil nje kwa majeraha

Arsenal's Mesut Ozil in action against Bayern Munich (AFP)
Mesut Ozil alipokuwa wakifanya mambo yake kabla ya kutolewa baada ya kuumia jana


HUENDA hii ikawa ni taarifa mbaya kwa mashabiki wa klabu ya Arsenal ambao wanaugulia kutolewa kwa timu yao kwenye hatua ya 16 Bora ya Ligi ya Mabingwa Ulaya usiku wa jana, baada ya kudokezwa kuwa huedna wakamkosa kiungo wao mahiri, Mesut Ozil aliyeumia katika pambano hilo la usiku wa jana
Meneja Arsene Wenger amethibitisha kuwa watakosa huduma za kiungo huyo aliyeumia katika mechi hiyo ikiwa ni siku chache baada ya kurejea kwenye kiwango chake na kuivusha Arsenal kwenye Nusu Fainali ya Kombe la FA.
Mchezaji huyo wa bei mbaya kwa klabu hiyo aliyolewa wakati wa mapumziko wakati matokeo yakiwa 1-1 na kocha Wenger amesema hana hakika itamchukua muda gani nje ya dimba, ila amekiri hatamtumia kwenye mechi yao ya Jumapili dhidi ya mahasimu wao wa London Kaskazini, Tottenham Hotspur.
"Linaonekana ni tatizo kubwa," alisema kocha huyo na kuongeza; "Sijui nitamkosa kwa muda gani, ila nina hakika hatacheza mechi ya Jumapili dhidi ya Spurs."
"Tutamfanyia vipimo kesho (leo) ili kujua tatizo lake lipo kwa kiasi gani ina atakuwa nje kwa wiki kadhaa. Natumaini halitakuwa tatizo kubwa sana," aliongeza kocha huyo toka Ufaransa.

Arsenal yang'oka, AC Milan aibu tupu Ligi ya Mabingwa Ulaya

Bastian SchweinsteigerAtletico Madrid's Diego Costa (R) celebrates with teammate Raul Garcia after scoring a goal against AC Milan during their Champions League last 16 second leg (Reuters)
Diego Costa akishangilia bao lake la Garcia

Jikaze wewe hii kazi ya kiume bana!
Atletico Madrid wakishangilia
Frank Ribery akichuana na wachezaji wa Arsenal
MABINGWA wa zamani wa Ulaya, AC Milan ya Italia imeyaaga michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya kukung'utwa ugenini mabao 4-1 na Atletico Madrid ya Hispania, huku Arsenal ikitoka sare ya 1-1 ugenini lakini imekwama kutinga Robo Fainali  dhidi ya Bayern Munich.
Atletico ikiwa kwenye uwanja wa nyumbani wa Vicente Calderon iliifumua Milan na kutinga hatua hiyo kwa jumla ya mabao 5-1 kwani mechi ya kwanza nchini Italia ilishinda 1-0.
Wenyeji waliwashtukiza wageni wao kwa bao la mapema la dakika tatu tu lililofungwa na nyota wa timu hiyo Diego Costa kabla ya Kaka kuisawazishia Milan bao dakika ya 27.
Hata hivyo Atletico iliongeza bao la pili dakika ya 40 kupitia kwa Turan na kwenda mapumziko wakiwa mbele kwa 2-1.
Kipindi cha pili kilikuwa cha wenyeji baada ya kuongeza mabao mengine katika dakika ya 70 lililofungwa na Raul Garcia na Diego Costa aliongeza jingine dakika tano kabla ya pambano kiumalizika.
Katika mechi nyingine iliyochezwa kwenye uwanja wa Allianz Arena, mjini Munich nchini Ujerumani, watetezi wa taji hilo, Bayern Munich waliiondosha tena mashindanoni Arsenal ya England baada ya kutoka nao sare ya 1-1.
Arsenal ilikwama kufuzu hatua ya 16 Bora kwa mwaka wa tano mfululizo baada ya kukubali kipigo cha mabao 2-0 nyumbani kwao wiki mbili zilizopita na hivyo sare ya jana imewafanya waage michuano hiyo kwa jumla ya mabao 3-1.
Wenyeji walikuwa wa kwanza kupata bao lililofungwa na Bastian Schweinsteiger katika dakika ya 54 kabla ya Lukas  Podolski kuisawazishia wageni dakika tatu baadaye.
Kivumbi cha ligi hiyo kitaendelea leo kwa mechi nyingine mbili Barcelona itakuwa nyumbani kuikaribisha Manchester City ambayo katika mechi yao ya kwanza waliifumua kwa mabao 2-0 na pambano jingine ni kati ya PSG ya Ufaransa dhidi ya Bayer Leverkusen walioitambia kwao mabao 4-0.