STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, March 12, 2014

Breaking News! Majambazi wanaswa wakijiandaa kufanya tukio Mbagala

http://www.mwanakijiji.com/overance/uploads/2013/11/SelemanKova.jpg
HABARI zilizotufikia muda huu zinasema kuwa Watu wawili wanaosadikiwa kuwa majambazi wamenaswa na jeshi la Polisi wakijiandaa kufanya tukio eneo la Mbagala-Dar es Salaam.
Taarifa hizo zinasema kuwa majambazi hao walinaswa wakiwa kwenye pikipiki yenye namba za usajili T 225 CQC aina ya Kapor baada ya kushtukiwa.
Inaelezwa wakora hao walinaswa wakiwa na silaha wakijiandaa kufanya uhalifu katika kituo cha kuuza mafuta cha Oilcom kilichopo Kongowe-Mbagala, jijini Dar! 
Majambazi hayo yametiwa mbaroni na askari polisi zaidi ya kumi waliokuwa wamevalia nguo za kiraia wakiwa na magari aina ya Land Cruiser yenye namba za usajili T 148 AEN na T 848 AGF!
Tukio hili limekuja siku moja baada ya jana jeshi hilo kuwanasa watu wengine wanaodaiwa kuwa majambazi kwenye kituo cha mabasi cha Ubungo wakijiandaa kufanya uhalifu.

No comments:

Post a Comment