STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, March 12, 2014

Samuel Sitta ashinda kwa kishindo Uenyekiti Bunge la Katiba

http://www.dar24.com/wp-content/uploads/2013/05/sitta.jpg
Mhe Samuel Sitta
WAJUMBE 487 kati ya 563 wamemchagua Mbunge wa Urambo Mashariki na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta kuwa Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba.
Sitaa aliyekuwa akipewa nafasi kubwa ya kushinda katika king'anyiro hicho alimwangusha mpinzani wake, Hashim Rungwe aliyeambulia kura 69, huku kura 7 ziliharibika katika uchaguzi uliofanyika jioni hii.
Kabla ya zoezi la kupigwa kura Mwenyekiti wa Muda wa Bunge hilo, Pande Ameir Kificho aliwatangaza wagombea hao na kuwapa nafasi ya kujieleza kwa wajumbe ambapo Mzee Sitaa alifunika kwa kusisitiza kuwa falsafa yake ya Standard and Speed ipo pale pale katika kuihakikishia Tanzania inaopata Katiba Mpya na yenye kiwango kwa mujibu wa matakwa ya wananchi.
MICHARAZO Inampa heko zake Mhe Sitta na kumtakia kila la heri katika kazi yake hiyo kwani ni wazi wajumbe na watanzania kwa ujumla wanamuamini kutokana na ufanisi wake serikali na alipokuwa Mbunge wa Bunge la Tanzania.

No comments:

Post a Comment