STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, March 12, 2014

Huu si wivu bali unyama na unyanyasaji

http://www.ippmedia.com/media/picture/large/shilogile-aug31-2013.jpg 
Na Mariam Kamgisha, Morogoro
MWANAMKE mmoja Juliana Wambura (24) mkazi wa kijiji cha Ruaha, ameuawa kwa kuchomwa kisu tumboni na mumewe.
Akizungumzia tukio hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Faustine Shilogile, alisema lilitokea juzi saa 2:00 usiku katika kijiji cha Ruaha tarafa ya Mikumi wilayani Kilosa.
Alisema marehemu aliuawa kinyama kwa kuchomwa na kisu tumboni  na mumewe  aliyefahamika kwa jina la  Fredi Ernest (34) mkazi wa Shirati Mara  na kupelekea utumbo wa mkewe kutoka nje.
Alisema chanzo cha mauaji hayo ni wivu wa mapenzi na mtuhumiwa baada ya kutekelea mauaji hayo amekimbia.
Katika tukio jengine alisema alisema Machi 8 mwaka huu saa 1:30 asubuhi, Gerry Joseph (23) alifariki dunia baada ya pikipiki aliyokuwa akiiendesha  kugonga mti.

Aidha alisema katika tukio jengine  gari aina ya Scania lililokuwa likiendeshwa na Juma Saidi (30) mkazi wa Dar es Salaam lilimgonga mtembea kwa miguu mwanamme asiyefahamika na kumsababishia kifo.

No comments:

Post a Comment