STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, September 27, 2012

Cheka, Nyilawila kupimwa afya uzito kesho, kuvaana PTA J'mosi

Karama Nyilawila (kushoto) na Francis Cheka wanaotarajia kupima uzito na afya kesho kabla ya kuvaana katika pambano lao lwa kuwania ubingwa wa Mabara wa UBO litakalofanyika siku ya Jumamosi ukumbi wa PTA.

BINGWA wa ngumi za kulipwa anayetambuliwa na  ICB na IBF-Afrika, Francis Cheka na aliyekuwa bingwa wa Dunia wa WBF, Karama Nyilawila wanatarajia kupima uzito na afya zao kesho tayari kwa pambano lao la Jumamosi kuwania ubingwa wa UBO-Mabara.
Mabondia hao wanatarajiwa kupambana katika pambano la uzani wa Super Middle la raundi 12 kwenye ukumbi wa PTA, jijini Dar es Salaam siku ya Jumamosi.
Mratibu wa pambano hilo, Robert Ekerege wa Afrika Kabisa Entertainment, alisema Cheka na Nyilawila watapimwa uzito na afya zao sambamba na mabondia wengine watakaowasindikiza kwenye pambano lao kwenye ukumbi wa Mawela jijini Dar.
Ekerege, alisema kupimwa kwa afya na uzito wa mabondia hao ni kuashiria kuiva kwa pambano hilo la kimataifa litakalochezewa na mwamuzi toka Malawi.
"Tunatarajia kuwapima afya na uzito wao mabondia wote watakaopigana Jumamosi, karibu mabondia wote wameshatua Dar tayari kwa zoezi hilo litakaloanza kufanyika saa 5 asubuhi ili kujiweka tayari kwa mchezo huo utakaofanyika PTA," alisema.
Aliongeza kuwa, maandalizi ya ujumla wa pambano hilo la Cheka na Nyilawila ambalo ni la tatu kwao kukutana na yale ya utangulizi yamekamilika ikiwemo kubadilisha mgeni rasmi wa siku hiyo kutoka Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Vijana na Michezo , Amos Makalla hadi kuwa Kamanda wa Kanda Maalum Dar, Afande Suleiman Kova.
Ekerege alisema wamemkosa Waziri Makalla waliokuwa wamempanga awali kwa vile atakuwa safarini na hivyo kumpa jukumu la kumvika mshindi wa pambano hilo la kesho Mlezi wa mchezo wa ngumi nchini, Kamanda Kova aliyethibitisha kushiriki.
Aliongeza kuwa katika mapambano hayo bendi maarufu ya Mashukaa Band 'Wana Kibega' ndio watakaotoa burudani ukumbini.

Mwisho

Arsenal, Man Utd, Liverpool zang'ara Kombe la Ligi

Mchezaji Ignasi Miquel akishangilia bao lake dhidi ya Coventry City
VIGOGO vya Ligi Kuu wa England, Arsenal, Manchester United, Liverpool na Tottenham Hotspurs usiku wa kuamkia zimefanya vema katika michuano ya Kombe la Ligi baada ya kutoa vipigo kwa wapinzani wao na kuvuka raundi nyingine.
Arsenal iliisasambua  Coventry City kwa mabao 6-1 kwenye pambano lililochezwa uwanja wa Emirates mjini London, wakati mahasimu wao Tottenham walipata ushindi wa magoli 3-0 dhidi ya Carlisle United ikiwa ugenini.
Manchester United wenyewe walipata ushindi wa mabao 2-1 wakiwa uwanja wa Old Trafford dhidi ya Newcastle United, wakati Liverpool ilitoka kupokea kichapo katika Ligi Kuu toka kwa wapinzani wao wa jadi Man United iliitafuna West Bromwich Albion kwa idadi kama hiyo ya mabao 2-1.
Mechi nyingine zilizochezwa jana WPR ilijikuta ikinyukwa nyumbani na Readind kwa mabao 3-2 na Norwich City iliilaza kwa bao 1-0 timu ya Doncaster Rovers.
Matokeo kamili ya mechi za michuano hiyo kwa siku ya jana ni kama ifuatavyo:
Norwich City 1-0 Doncaster Rovers
QPR 2-3 Reading
Arsenal 6-1 Coventry City
Celtic 2-1 Benfica
Manchester United 2-2 Newcastle
Carlisle United 0-3 Tottenham
West Brom 1-2 Liverpool
More: Scores | Fixtures | League Cup
 

Coastal yatakata Mkwakwani, Toto ikiendeleza mdudu wa sare

 MABAO mawili toka kwa mshambuliaji nyota na mzoefu, Nsa Job na jingine la Daniel Lyanga jana yaliipaisha timu ya Coastal Union hadi nafasi ya pili mwa msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara baada ya kuilaza Kagera Sugar goli 3-2.
Coastal  ilipata ushindi huo katika pambano lililochezwa kwenye uwanja wa Mkwakwani Tanga ikiwa chini ya kocha wao wa makipa, Juma Pondamali na kulingana kila kitu na Azam waliokuwa wakiishikilia nafasi hiyo.
Huo ni ushindi wa pili kw atimu hiyo baada ya awali kufanya hivyo katika mechi ya fungua dimba la Ligi Kuu dhidi ya 'majirani' Mgambo Shooting kabla ya kutoka sare mbechi nyingine mbili.
Katika mfululizo wa ligi hiyo timu ya Toto Africans ya Mwanza imeendelea na mdudu wake wa sare baada ya jana kutoka suluhu ya bila kufungana na wenyeji wao Polisi Morogoro.
Hiyo ni sare ya nne kwa Toto Africans baada ya awali kufanya hivyo dhidi ya JKT Oljoro ilitoka sare ya 1-1, Azam 2-2 na kisha Mgambo Shooting mechi yao iliyopita.
Ligi hiyo inatarajiwa kuendelea mwishoni mwa wiki kwa michezo kadhaa itakazozihusisha timu za Azam, Yanga na Simba ambazo kwa sasa zinawindana kwa ajili ya pambano lao litakalofanyika Jumatano ijayo jijini Dar.