STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, September 27, 2012

Arsenal, Man Utd, Liverpool zang'ara Kombe la Ligi

Mchezaji Ignasi Miquel akishangilia bao lake dhidi ya Coventry City
VIGOGO vya Ligi Kuu wa England, Arsenal, Manchester United, Liverpool na Tottenham Hotspurs usiku wa kuamkia zimefanya vema katika michuano ya Kombe la Ligi baada ya kutoa vipigo kwa wapinzani wao na kuvuka raundi nyingine.
Arsenal iliisasambua  Coventry City kwa mabao 6-1 kwenye pambano lililochezwa uwanja wa Emirates mjini London, wakati mahasimu wao Tottenham walipata ushindi wa magoli 3-0 dhidi ya Carlisle United ikiwa ugenini.
Manchester United wenyewe walipata ushindi wa mabao 2-1 wakiwa uwanja wa Old Trafford dhidi ya Newcastle United, wakati Liverpool ilitoka kupokea kichapo katika Ligi Kuu toka kwa wapinzani wao wa jadi Man United iliitafuna West Bromwich Albion kwa idadi kama hiyo ya mabao 2-1.
Mechi nyingine zilizochezwa jana WPR ilijikuta ikinyukwa nyumbani na Readind kwa mabao 3-2 na Norwich City iliilaza kwa bao 1-0 timu ya Doncaster Rovers.
Matokeo kamili ya mechi za michuano hiyo kwa siku ya jana ni kama ifuatavyo:
Norwich City 1-0 Doncaster Rovers
QPR 2-3 Reading
Arsenal 6-1 Coventry City
Celtic 2-1 Benfica
Manchester United 2-2 Newcastle
Carlisle United 0-3 Tottenham
West Brom 1-2 Liverpool
More: Scores | Fixtures | League Cup
 

No comments:

Post a Comment