STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, September 27, 2012

Coastal yatakata Mkwakwani, Toto ikiendeleza mdudu wa sare

 MABAO mawili toka kwa mshambuliaji nyota na mzoefu, Nsa Job na jingine la Daniel Lyanga jana yaliipaisha timu ya Coastal Union hadi nafasi ya pili mwa msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara baada ya kuilaza Kagera Sugar goli 3-2.
Coastal  ilipata ushindi huo katika pambano lililochezwa kwenye uwanja wa Mkwakwani Tanga ikiwa chini ya kocha wao wa makipa, Juma Pondamali na kulingana kila kitu na Azam waliokuwa wakiishikilia nafasi hiyo.
Huo ni ushindi wa pili kw atimu hiyo baada ya awali kufanya hivyo katika mechi ya fungua dimba la Ligi Kuu dhidi ya 'majirani' Mgambo Shooting kabla ya kutoka sare mbechi nyingine mbili.
Katika mfululizo wa ligi hiyo timu ya Toto Africans ya Mwanza imeendelea na mdudu wake wa sare baada ya jana kutoka suluhu ya bila kufungana na wenyeji wao Polisi Morogoro.
Hiyo ni sare ya nne kwa Toto Africans baada ya awali kufanya hivyo dhidi ya JKT Oljoro ilitoka sare ya 1-1, Azam 2-2 na kisha Mgambo Shooting mechi yao iliyopita.
Ligi hiyo inatarajiwa kuendelea mwishoni mwa wiki kwa michezo kadhaa itakazozihusisha timu za Azam, Yanga na Simba ambazo kwa sasa zinawindana kwa ajili ya pambano lao litakalofanyika Jumatano ijayo jijini Dar. 

No comments:

Post a Comment