STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, September 30, 2012

MASHETANI WEKUNDU HOI KWA SPURS, YALALA OLD TRAFFORD




Jan Vertonghen akishangilia bao aliloifungia timu yake ya Tottenham dhidi ya Manchester United jana. Picha:Reuters


TIMU ya soka ya Tottenham Hotspurs chini ya kocha wake Andre Villa Boas jana walivunja mwiko wa kutoifunga Manchester United kwa muda mrefu baada ya kuwalaza Mashetani Wekundu hao kwenye dimba lao la nyumbani la Old Frafford kwa mabao 3-2.
Bao la mapema lililofungwa na Vertonghen liliwachanganya Man United kabla ya kukujikuta wakifungwa jingine nusu saa baadae na Garret Bale na kuwafanya Spurs kwenda mapumziko wakiongoza mabao 2-0.
Katika mechi nyingine, vinara wa ligi hiyo Chelsea wameendelea kung'ara kwa kuilaza Arsenal mabao 2-1, huku Liverpool ikitoa kisango cha 'mbwa mwizi' kwa Norwich City kwa kuilaza mabao 5-2, huku jahazi la Swansea City likiendelea kuzama kwa kulazwa mabao 2-0 na Stoke City mabao yote yakitupiwa kambani na Peter Crouch.
Matokeo mengine ya mechi za Ligi Kuu ya England kwa jana ni kama iofuatavyo:


29 September
Man Utd2 - 3Tottenham
LCAdC Nani (50)
S Kagawa (53)

J Vertonghen (1)
G Bale (31)
CD Dempsey (51)
Old TraffordAttendance (75566)
Teams | Report
29 September
Stoke2 - 0Swansea
P Crouch (11)
P Crouch (35)

Britannia StadiumAttendance (27330)
Teams | Report

29 September
Norwich2 - 5Liverpool
S Morison (60)
G Holt (86)

L Suarez (1)
L Suarez (37)
N Sahin (46)
L Suarez (56)
S Gerrard (67)
Carrow RoadAttendance (26831)
Teams | Report
29 September
Sunderland1 - 0Wigan
S Fletcher (50)
Stadium of LightAttendance (37742)
Teams

29 September
Fulham1 - 2Man City
M Petric (pen 9)
SL Aguero (42)
E Dzeko (86)
Craven CottageAttendance (25698)
Teams
29 September
Everton3 - 1Southampton
L Osman (24)
N Jelavic (31)
N Jelavic (37)

G Ramirez (5)
Goodison ParkAttendance (37922)
Teams

29 September
Reading2 - 2Newcastle
JB Kebe (57)
N Hunt (61)

D Ba (57)
D Ba (82)
Madejski StadiumAttendance (24097)
Teams | Report
29 September
Arsenal1 - 2Chelsea
YK Gervinho (41)
FJS Torres (19)
JMG Mata (52)
Emirates StadiumAttendance (60101)
Teams | Report

Yanga, Lyon kujiuliza leo Taifa

MABINGWA wa Kombe la Kagame, Yanga leo ikiwa chini ya kocha wake mpya, Ernstus Brandts inatarajiwa kuivaa Africna Lyon katika mfululizo wa mechi za Ligi Kuu Tanzania Bara pambano litakalofanyika kwenye uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam.
Yanga ambayo imemsainisha mkataba wa mwaka mmoja kocha huyo kutoka Uholanzi, itaikaribisha Lyon ikiwa bado inachekelea ushindi mnono wa mabao 4-1 iliyopata dhidi ya JKT Ruvu.
Pambano hilo ambalo litarushwa hewani na kituo cha Super Sport katika ule muendelezo wa Tanzania Weekend Soccer, linatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa kutokana na wapinzani wa Yanga kutoka kupokea kichapo cha mabao 2-1 toka kwa Prisons ya Mbeya.
Yanga itahitajika ishinde ili kujiweka pazuri kabla ya kuvaana na watani zao keshokutwa kwenye pambano lao la kwanza ambapo wana Jangwani wana deni kubwa la kulipa kisasi cha kufungwa mabao 5-0 katika mechi ya kufungia msimu uliopita.
Mbali na deni hilo la karibuni, pia Yanga ina deni la miaka 37 la kipigo cha mabao 6-0 ilichopewa mwaka 1977 ambacho imekuwa ikihangaika kukirudisha bila ya mafanikio.
Bila shaka pambano hilo litakuwa kipimo kizuri kwa makocha wa timu hizo mbili, Brandts wa Yanga na Muargentina anayeinoa Lyon, iliyoshinda mechi moja tu kama wapinzani wao hao wanaovaana wakiwategemea mshambiliaji wake nyota, Adam Kingwande na wengineo.

SIMBA YAREJEA KILELENI, YAITUNGUA PRISONS 2-1

 
MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu, Simba jana waliendelea kutakata kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara baada ya kuitandika Prisons ya Mbeya mabao 2-0 na kurejea kileleni wakiiondosha Azam Fc iliyowaengua kwa saa kadhaa.
Bao la kwanza la Mrisho Ngassa kwa timu hiyo ndilo lililoipa Simba ushindi iliyomaliza mechi hiyo iliyochezwa kwenye uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ikiwa wachezaji tisa uwanjani.
Kwa ushindi huo, Simba imeendelea kuwa timu pekee yenye matokeo ya asilimia 100 baada ya raundi nne, ikiwa na pointi 12, mbili juu ya Azam, katika pambano lililohudhuriwa na watazamaji wachache kuliko kawaida ya mechi za mabingwa watetezi hao.
Coastal Union ni ya tatu ikiwa na pointi nane, tatu juu ya Prisons ambayo imeshuka kwa nafasi moja mpaka kuwa timu ya tano nyuma ya JKT Oljoro kwa uwiano wa mabao, zote zikiwa na pointi tano baada ya michezo minne.
Siku iliisha vibaya kwa Simba baaada ya beki wake Amiri Maftaha kuonyeshwa kadi nyekundu na muamuzi Paul Soleji dakika mbili kabla ya filimbi ya miwsho, baada ya kumchezea rafu mbaya Khalid Fupi.
Siku ilianza vibaya pia kwa Simba baada ya Lugano Mwangama kuipatia Prisons bao la kuongoza katika dakika ya saba tu ya mchezo kwa shuti kali ambalo lilimbabatiza beki Juma Nyoso wa Simba kabla ya kutinga wavuni, kwenye Uwanja wa Taifa.
Iliichukua Simba kipindi kizima cha kwanza kupata bao la kusawazisha lililofungwa na Felix Sunzu katika dakika ya 45 akiunganisha krosi ya Mwinyi Kazimoto.
Kama alivyomalizia ngwe ya kwanza, Sunzu angeweza kuongeza idadi ya mabao ya Simba dakika tatu tangu kuanza kwa kipindi cha pili lakini shuti lake kutokana na pasi ya Mrisho Ngassa lilipaa juu.
Ndipo Ngassa alipochukua jukumu la kusahihisha kosa hilo mwenyewe dakika saba baadaye kwa shuti lililomshinda David Abdallah kuzuia katika lango la Prisons, akiunganisha krosi ya Said Nassoro.  
Simba iliwatoa Amri Kiemba na nafasi yake kuchukuliwa na Salim Kinje, Ramadhani Chombo aliyempisha Jonas Mkude na Edward Christopher kwa Daniel Akuffor baada ya goli la Ngassa ikiwa ni jitihada za kutawala zaidi mechi hiyo, lakini hapakuwa na goli la ziada.
Kocha wa Simba Milovan Circovic alisema timu yake ilipata ushindi kutokana na kucheza vizuri, na akasikitikia athari za kadi nyekundu ya Maftah ingawa alisema kuna wachezaji wa kuziba pengo lake.
Timu zilikuwa:
SIMBA: Juma Kaseja, Nassoro Masoud, Amir Maftah, Shomari Kapombe, Juma Nyoso, Mwinyi Kazimoto, Amri Kiemba (Salim Kinje dk.74), Ramadhani Chombo (Jonas Mkude dk.67), Edward Christopher (Daniel Akuffor dk.76), Felix Sunzu, Mrisho Ngassa.
PRISONS: David Abdallah, Aziz Sibo, Laurian Mpalile, Lugano Mwangama, David Mwantika, Khalid Fupi, Misango Magai, Fred Chudu, Elias Maguri, Peter Michael (Sino Agustino dk.67), John Matei.

 

 Wachezaji wa Simba wakishangilia bao la kwanza lililofungwa na Felix Sunzu (kulia)
 Mashabiki wa Simba wakishangilia
 Mshambuliaji wa Simba, mrisho Ngasa akichuana na nahodha wa Tanzania Prisons, Lugano Mwangama
 Golikipa wa Prisons, David Abdallah akiokoa hatari langoni mwake
Wachezahi wa Prisons ya Mbeya wakiongozwa na kipa wao kuomba dua wakati wa mapumziko





CHEKA AMCHAPA TENA NYILAWILA SAFARI HII KWA KO

Bondia Fransic Cheka akinyooshwa mkono juu na mmoja wa mashabiki wa Kigeni waliokuja kuangalia mpambano wake dhidi ya Karama Nyilawila Cheka alishinda katika raundi ya sita baada ya karama kusalimu amri kushoto ni Rais wa PST Emanuel Mlundwa na wa pili kulia ni mgeni rasmi Kamanda wa polisi wa Kanda Maalumu Mkoa wa Dar es salaam Suleiman Kova.Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Refarii wa mpambano akiwaelekeza mabondia wasicheze kwa kukumbatiana

Bondia Fransic Cheka kushoto akipepesuka baada ya kupigwa ngumi na Karama Nyilawila wakati wa mpambano wao uliofanyika usiku wa jumamosi cheka alishinda kwa K.O raundi ya sita na kufanikiwa kunyakuwa ubingwa picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

Bondia Fransic Cheka kushoto akimshambulia Karama Nyilawila kwa masumbwi wakati wa mpambano wao uliofanyika usiku wa jumamosi Cheka alishinda raundi ya sita baada ya kumpiga na kudondoka chini baada ya kuesabiwa akashindwa kuendelea picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Bondia Karama Nyilawila  kulia akijitaidi kukwepa makonde ya mpinzani wake Fransic Cheka wakati wa mpambano wao uliofanyika usiku wa jumamosi cheka alishinda kwa K,o raundi ya sita picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

Mabondia Karama Nyilawila kushoto akionesheana umwamba wa kutupa masumbwi na Fransic Cheka wakati wa mpambano wao cheka alishinda kwa K,O Raundi ya sitapicha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

Fransic Cheka kushoto na Karama Nyilawila wakiwa uringoni kuoneshana uwezo wa kutupiana masumbwi Cheka alishjnda kwa K,O ya Raundi ya sita picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Mabondia Karama Nyilawila kushoto na Fransic Cheka wakionesheana umwamba wa kutupiana makonde wakati wa mpambano wao uliofanyika usiku wa jumamosi katika ukumbi wa PTA Sabasaba Cheka alishinda kwa K,o raundi ya sita picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

Bondia Fransic Cheka akinyooshwa mkono juu na mmoja wa mashabiki wa Kigeni waliokuja kuangalia mpambano wake dhidi ya Karama Nyilawila Cheka alishinda katika raundi ya sita baada ya karama kusalimu amri kushoto ni Rais wa PST Emanuel Mlundwa na wa pili kulia ni mgeni rasmi Kamanda wa polisi wa Kanda Maalumu Mkoa wa Dar es salaam Suleiman Kova.Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

Bondia Fransic Cheka akinyooshwa mkono juu na mmoja wa mashabiki wa Kigeni waliokuja kuangalia mpambano wake dhidi ya Karama Nyilawila Cheka alishinda katika raundi ya sita baada ya karama kusalimu amri kushoto ni Rais wa PST Emanuel Mlundwa na wa pili kulia ni mgeni rasmi Kamanda wa polisi wa Kanda Maalumu Mkoa wa Dar es salaam Suleiman Kova.Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Bondia Fransic Cheka akinyooshwa mkono juu na mmoja wa mashabiki wa Kigeni waliokuja kuangalia mpambano wake dhidi ya Karama Nyilawila Cheka alishinda katika raundi ya sita baada ya karama kusalimu amri kushoto ni Rais wa PST Emanuel Mlundwa na wa pili kulia ni mgeni rasmi Kamanda wa polisi wa Kanda Maalumu Mkoa wa Dar es salaam Suleiman Kova.Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
BINGWA wa ngumi za kulipwa anayetambuliwa na vyama vya ICB, IBF na WBC, Francis Cheka 'SMG' usiku wa kuamkia leo amedhihirisha kwamba hana mpinzani katika ngumi hizo nchini baada ya kumchapa kwa KO mpinzani wake mkubwa, Karama Nyilawila na kuongeza taji jingine.
Cheka alimpiga Nyilawila katika raundi ya sita ya pam,bano hilo lililokuwa la uzani wa Super Middle la raundi 12 lililofanyika kwenye ukumbi wa PTA, Temeke jijini Dar es Salaam na kutwaa ubingwa wa Mabara wa UBO uliokuwa wazi.
Pambano hilo lililohudhuriwa na mashabiki lukuki, lilishuhudia raundi zote tano za kwanza Nyilawila akionyesha kumdhibiti Cheka kwa kumchezea 'kibabe' akitumia nguvu nyingi kujihami na baadhi ya watu ukumbini kuamini mwisho wa tambo za Cheka zilikuwa zimewadia.
Hata hivyo raudni ya sita ilipoanza Cheka alionyesha amebadilika na hasa baada ya kocha wake Abdallahj Saleh 'Komando' kupanda ulingoni na kuzungumza na bondia huyo na kumshushia kipigo Nyilawila, ambapo moja ya makonde matatu ya mfululizo yalimpeleka chini mpinzani wake.
Mwamuzi wa pambano hilo, Jerome Waluza alimhesabia Nyilawila ambaye alijitahidi kuinuka, lakini ghafla akaonyesha ishara kwamba asingeweza kuendelea na pambano hilo na ukumbi mzima kuripuka kwa shangwe akishangiliwa Cheka ambaye hiyo ni mara ya pili kumpiga Nyilawila.
Kabla ya pambano hilo lililoanza majira ya saa 3;40 usiku, kulikuwa na mapambano saba ya utangulizi pamoja na burudani ya muziki toka bendi ya Mashujaa ambao hata hivyo sio wapenzi wengi walioweza kuishuhudia kutokana na kuondoka ukumbini mapema.
Katika pambano la kwanza la utangulizi Said Mbelwa alimpiga kwa pointi Dickson Mwakipesile, Juma Kihiyo alipigwa kwa pointi na Ibrahim Mahokola katika pambano lililovutia kwa namna mabondia hao walivyoonyeshana kazi.
Pia mdogo wa Cheka, Cosmas Cheka alifanikiwa kuibuka na ushindi wa pointi dhidi ya Fadhil Awadh katika pamnbano jingine lililosisimua wengi kwa ufundi uliokuwa ukionyesha na mabondia hao, naye Shaaban Kilumbelumbe alimpiga kwa pointi Anthony Mathias kabla ya Safari Mbiyu kumpiga kwa KO ya raundi ya kwanza Khalfan Jumanne.
Michezo minginme iliwakutanisha Stan Kessy na Seba Temba, pambano lililoisha kwa mabondia hao kutoka sare na Hassani Kidebe alitolewa nishai na Deo Samwel kwa kupigwa kwa pointi.
Mgeni rasmi katika pambano hilo alikuwa Kamanda wa Polisi Kanda maalum ya Dar es Salaam ambaye aliutangazia umma kwamba kama Mlezi wa Ngumi za Kulipwa amefanikiwa kuwafuta wafadhili katika mchezo huo na kumtambulisha raia mmoja wa kigeni kwamba ni miongoni mwao.