STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, November 15, 2013

Japhet Kaseba azidunda Australia

 
BINGWA wa Taifa wa Ngumi za Kulipwa, Japhet Kaseba 'Champion' yupo nchini Australia kwa ajili ya kupigana na bondia Jeremy van Dieman wa nchini humo katika pambano la kimataifa.
Pambano hilo la uzito wa Heavy Light  (kilo 79) linatarajiwa kufanyika kwenye Ukumbi wa Metro City, uliopo mjini Northbridge nchini humo.
Kwa mujibu wa taarifa zilizotumwa nchini na Kaseba akiwa Australia, mabondia hao walipimwa uzito jana tayari kwa pambano hilo la leo ambalo litakuwa la kwanza kwake kimataifa tangu aliporejee kwenye ngumi.
"Nipo Australia na tumetoka kupima uzito kwa ajili ya pambano letu la kesho (leo) la kimataifa dhidi ya mwenyeji wangu Jeremy van Dieman ambaye nitapigana naye kwenye Ukumbi wa Metro City, Magharibi mwa Australia," alisema Kaseba.
Kaseba alisema mara baada ya pambano hilo ambalo ametamba kufanya vizuri ili kujitengenezea mazingira ya kuwania ubingwa wa dunia, atarejea nchini siku ya Jumapili majira ya saa nane mchana.
"Nitarejea nchini Jumapili ya Novemba 17 saa nane mchana, nawaomba Watanzania waniombee kila la heri niweze kufanya vema katika mchezo huo wa Ijumaa (leo)," alisema Kaseba, bingwa wa zamani wa Dunia wa Kick Boxing.
Kaseba mwenye rekodi ya kucheza michezo minne akishinda miwili na kupoteza miwili, atavaana na Dieman anayeshikilia nafasi ya tisa nchini mwake kwenye uzito huo wa Heavy Light huku akicheza michezo minne na kutoka sare miwili.