STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, April 29, 2018

HIZI NDIZO REKODI ZA MECHI 99 ZA WATANI TANGU 1965










RAHIM JUNIOR
SIMBA na Yanga leo zinatarajiwa kuvaana kwenye Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam katika pambano la marudiano la Ligi Kuu Bara msimu huu.
Kumekuwa na mkanganyiko mkubwa juu ya ukweli kuhusu timu hizi kongwe zimekutana mara ngapi katika mechi za Ligi Kuu Bara tangu ligi hiyo ilipoasisiwa mwaka 1965.
MICHARAZO MITUPU, limeamua kukata mzizi wa fitina kwa kuwawekea rekodi halisi ya mechi hizo kuthibitisha kuwa leo Jumapili ya Aprili 29, 2018 linapigwa pambano la 100 kwa klabu hizo.
Nani atakayeibuka na ushindi kwenye Uwanja wa Taifa? Hiyo ni baada ya kumalizika kwa dakika 90 za mchezo huo utakaochezwa na Mwamuzi Emmanuel Mwandembwa.

Rekodi zenyewe hizi hapa chini...titirika nayo...!

1) JUNI 7, 1965 (Monday)
Yanga 1-0 Sunderland (Simba)
MFUNGAJI: Mawazo Shomvi dk. 15).

2) JUNI 3,  1966 (Friday)
Yanga 3-2 Sunderland (Simba)
WAFUNGAJI:
Yanga: Abdulrahman Lukongo dk. 54, Andrew Tematema dk 67, Emmanuel Makaidi dk. 83. Sunderland: Mustafa Choteka dk 24, Haji Lesso dk. 86.

3) NOVEMBA 26, 1966 (Saturday)
Sunderland 1-0 Yanga
MFUNGAJI: Mustafa Choteka dk. 44.

4) MACHI 30, 1968 (Saturday)
Yanga 1-0 Sunderland
MFUNGAJI: Kitwana Manara dk. 28.

5) JUNI 1, 1968 (Saturday)
Yanga 5-0 Sunderland
WAFUNGAJI:
Maulid Dilunga dk. 18 (penalti), Dilunga dk. 43, Salehe Zimbwe dk. 54, Zimbwe dk. 89, Kitwana Manara dk. 86.

6) MACHI 3, 1969 (Monday)
Yanga v Sunderland
(Yanga ilipewa pointi za chee na ushindi wa mabao 2-0, baada ya Sunderland kugoma kuingia uwanjani).

7) JUNI 4, 1972 (Sunday)
Yanga 1-1 Sunderland
WAFUNGAJI:
Yanga: Kitwana Manara dk. 19,
Sunderland: Willy Mwaijibe dk. 11.

8) JUNI 18, 1972 (Sunday)
Yanga 1-0 Simba
MFUNGAJI: Leonard Chitete.

9) JUNI 23,  1973 (Saturday)
Simba 1-0 Yanga
MFUNGAJI: Haidari Abeid 'Muchacho' dk. 68.

10) AGOSTI 10, 1974 (Saturday)
Yanga 2-1 Simba
WAFUNGAJI:
Yanga: Gibson Sembuli dk. 87, Sunday Manara dk. 97.
Simba: Adam Sabu dk. 16.
(Mechi ya kihistoria iliyochezwa Uwanja wa Nyamagana mjini Mwanza).

11) JULAI 19, 1977 (Tuesday)
Simba 6-0 Yanga
WAFUNGAJI:
Abdallah Kibadeni dk. 10, 42 na 89, Jumanne Hassan 'Masimenti' dk. 60 na 73, Selemani Sanga alijifunga dk. 20.

12) OKTOBA 7, 1979(Sunday)
Simba 3-1 Yanga
WAFUNGAJI:
Simba: Nico Njohole dk. 3, Mohammed Bakari 'Tall' dk. 38, Abbas Dilunga dk.72. Yanga: Rashidi Hanzuruni dk. 4.

13) OKTOBA 4, 1980 (Saturday)
Simba 3-0 Yanga
WAFUNGAJI: Abdallah Mwinyimkuu dk. 29, Thuwein Ally dk. 82, Nico Njohole dk. 83.

14) SEPTEMBA 5, 1981 (Saturday)
Yanga 1-0 Simba
MFUNGAJI: Juma Hassan Mkambi dk. 42

15) APRILI 29, 1982 (Thursday)
Yanga 1-0 Simba
MFUNGAJI: Rashid Hanzuruni dk 2.

16) SEPTEMBA 18, 1982(Saturday)
Yanga 3-0 Simba
WAFUNGAJI:
Omar Hussein dk. 2 na 85, Makumbi Juma dk. 62.

17) FEBRUARI 10, 1983 (Thursday)
Yanga 0-0 Simba.

18) APRILI 16, 1983 (Saturday)
Yanga 3-1 Simba
WAFUNGAJI:
Yanga: Charles Mkwasa dk. 21, Makumbi Juma dk. 38, Omar Hussein dk. 84, Simba; Kihwelu Mussa dk. 14.

19) SEPTEMBA 10, 1983 (Saturday)
Yanga 2-0 Simba
WAFUNGAJI: Lila Shomari alijifunga dk. 72, Ahmed Amasha dk. 89.

20) SEPTEMBA 25, 1983 (Sunday)
Yanga 1-1 Simba
WAFUNGAJI:
Yanga: Makumbi Juma dk. 75,
Simba: Sunday Juma dk. 72.

21) MACHI 10, 1984 (Saturday)
Yanga 1-1 Simba
WAFUNGAJI:
Yanga: Omar Hussein dk. 72.
Simba: Idd Pazi kwa penalti dk 20.

22) JULAI 14, 1984 (Saturday)
Yanga 1-1 Simba
WAFUNGAJI:
Yanga: Abeid Mziba dk. 39.
Simba: Zamoyoni Mogella dk. 17

23) MEI 19, 1985 (Sunday)
Yanga 1-1 Simba
WAFUNGAJI:
Yanga: Omar Hussein dk. 6
Simba: Mohammed Bob Chopa dk. 30.

24) AGOSTI 10, 1985 (Saturday)
Yanga 2-0 Simba

25) MACHI 15, 1986 (Saturday)
Yanga 1-1 Simba
WAFUNGAJI:
Yanga: Abeid Mziba dk. 44
Simba: John Hassan Douglas dk. 20.

26) AGOSTI 23, 1986 (Saturday)
Simba 2-1 Yanga
WAFUNGAJI:
Simba: Edward Chumila dk. 9, Malota Soma dk. 51
Yanga: Omar Hussein dk. 5.

27) JUNI 27, 1987 (Saturday)
Yanga 1-0 Simba
MFUNGAJI: Edgar 'Fongo' Mwafongo dk. 36.

28) AGOSTI 15, 1987 (Saturday)
Yanga 1-0 Simba
MFUNGAJI: Abeid Mziba dk. 14.

29) APRILI 30, 1988 (Sunday)
Yanga 1-1 Simba
WAFUNGAJI:
Yanga: Justin Mtekere dk. 28
Simba: Edward Chumila dk. 25.

30) JULAI 23, 1988 (Saturday)
Simba 2-1 Yanga
WAFUNGAJI:
Simba: Edward Chumila 21, John Makelele dk. 58
Yanga: Issa Athumani dk. 36.

31) JANUARI 28, 1989 (Saturday)
Yanga 2-1 Simba
WAFUNGAJI:
Yanga: Issa Athumani dk. 4, Abeid Mziba dk. 85
Simba: Malota Soma dk. 30.

32) MEI 21, 1989 (Sunday)
Yanga 0-0 Simba

33) MEI 26, 1990 (Saturday)
Simba 1-0 Yanga
MFUNGAJI: Mavumbi Omari dk 6.

34) OKTOBA 20, 1990 (Saturday)
Yanga 3-1 Simba
WAFUNGAJI:
Yanga: Makumbi Juma dk 33, Thomas Kipese dk. 82, Sanifu Lazaro dk. 89
Simba: Edward Chumila dk. 58.

35) MEI 18, 1991 (Saturday)
Yanga 1-0 Simba
MFUNGAJI: Said Sued 'Scud' dk.  7.

36) AGOSTI 31, 1991 (Saturday)
Yanga 1-0 Simba
MFUNGAJI: Said Sued Scud.

37) OKTOBA 9, 1991 (Wednesday)
Yanga 2-0 Simba
WAFUNGAJI: Athumani China dk. 3, Abubakar Salum 'Sure Boy' dk. 54.

38) NOVEMBA 13, 1991 (Wednesday)
Yanga 2-0 Simba

39) APRILI 12, 1992 (Sunday)
Yanga 1-0 Simba
MFUNGAJI: Kenneth Mkapa dk. 10.

40) SEPTEMBA 26, 1992 (Saturday)
Simba 2-0 Yanga

41) OKTOBA 27, 1992 (Tuesday)
Simba 1-0 Yanga
MFUNGAJI: Damian  Kimti.

42) MACHI 27, 1993 (Saturday)
Yanga 2-1 Simba
WAFUNGAJI:
Yanga: Said Mwamba Kizota dk. 47 na 57
Simba: Edward Chumila dk. 75.

43) JULAI 17, 1993 (Saturday)
Simba 1-0 Yanga
MFUNGAJI: Dua Said dk. 69.

44) SEPTEMBA 26, 1993 (Sunday)
Simba 1-0 Yanga
MFUNGAJI: Dua Said dk. 13.

45) NOVEMBA 6, 1993 (Saturday)
Simba 0-0 Yanga

46) FEBRUARI 26, 1994 (Saturday)
Yanga 2-0 Simba
MFUNGAJI: Mohammed Hussein 'Mmachinga' na James Tungaraza 'Boli Zozo'.

47) JULAI 2, 1994 (Saturday)
Simba 4-1 Yanga
WAFUNGAJI:
Simba: George Masatu, Athumani China, Madaraka Selemani, Dua Saidi
Yanga: Constantine Kimanda.

48) NOVEMBA 2, 1994 (Wednesday)
Simba 1-0 Yanga
MFUNGAJI: Madaraka Selemani dk. 71

49) NOVEMBA 21, 1994 (Monday)
Simba 2-0 Yanga
WAFUNGAJI: George Lucas dk. 18, Madaraka Selemani dk. 42.

50) MACHI 18, 1995 (Saturday)
Simba 0-0 Yanga

51) OKTOBA 4, 1995 (Wednesday)
Simba 2-1 Yanga
WAFUNGAJI:
Simba: Said Mwamba 'Kizota' dk. 70, Mchunga Bakari dk. 79,
Yanga: Mohammed Hussein 'Mmachinga' dk. 40.

52) FEBRUARI 25, 1996 (Sunday)
Yanga 2-0 Simba

53) SEPTEMBA 21, 1996 (Saturday)
Yanga 0-0 Simba

54) OKTOBA 23, 1996 (Wednesday)
Yanga 1-0 Simba
MFUNGAJI: Mohamed Hussein 'Mmachinga' dk. 46

55) NOVEMBA 9, 1996 (Saturday)
Yanga 4-4 Simba
WAFUNGAJI:
Yanga: Edibilly Lunyamila (penalti) dk. 28, Mustafa Hozza alijifunga dk 64, Said Mwamba 'Kizota' dk. 70, Sanifu Lazaro dk. 75.
Simba: Thomas Kipese dk. 7, Ahmed Mwinyimkuu dk. 43, Dua Saidi dk. 60 na 90.
(Mechi hii ilichezwa Uwanja wa Sheikh Amri Abeid mjini Arusha)

56) APRILI 26, 1997 (Saturday)
Yanga 1-1 Simba
WAFUNGAJI:
Yanga: Idelfonce Amlima dk. 16
Simba: Abdallah Msamba sekunde ya. 56

57) AGOSTI 31, 1997 (Sunday)
Yanga 0-0 Simba

58) OKTOBA 11, 1997 (Saturday)
Yanga 1-1 Simba
WAFUNGAJI:
Yanga: Sekilojo Chambua dk. 52
Simba: George Masatu dk. 89
(Mechi hii ilichezwa Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya)

59) NOVEMBA 8, 1997 (Saturday)
Yanga 1-0 Simba
MFUNGAJI: Sekilojo Chambua dk. 85
(Mechi hii ilichezwa Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma)

60) FEBRUARI 21, 1998 (Saturday)
Yanga 1-1 Simba
WAFUNGAJI:
Yanga: Akida Makunda dk. 46
Simba: Athumani Machepe dk. 88

61) JUNI 7, 1998 (Sunday)
Yanga 1-1 Simba
WAFUNGAJI:
Yanga: Idelfonce Amlima dk. 28
Simba: Abuu Juma (penalti) dk. 32

62) MEI 1, 1999 (Saturday)
Yanga 3-1 Simba
WAFUNGAJI:
Yanga: Idd Moshi dk. 59, Kalimangonga Ongala dk. 64, Salvatory Edward dk. 70
Simba: Juma Amir dk. 12.

63) AGOSTI 29, 1999 (Sunday)
Yanga 2-0 Simba
WAFUNGAJI: Bakari Malima dk. 49, Mohammed Hussein 'Mmachinga' dk 71

64) JUNI 25, 2000 (Sunday)
Simba 2-1 Yanga
WAFUNGAJI:
Simba: Steven Mapunda dk. 59 na 72
Yanga: Idd Moshi dk. 4.

65) AGOSTI 5, 2000 (Saturday)
Yanga 2-0 Simba
MFUNGAJI: Iddi Moshi 37 na 47. (Alifunga mabao hayo, akitoka kwenye fungate ya ndoa yake)

66) SEPTEMBA 1, 2001 (Saturday)
Simba 1-0 Yanga
MFUNGAJI: Joseph Kaniki dk. 76

67) SEPTEMBA 30, 2001 (Sunday)
Simba 1-1 Yanga
WAFUNGAJI:
Simba: Joseph Kaniki dk. 65,
Yanga: Sekilojo Chambua dk. 86
(Mechi hii ilichezwa Uwanja wa CCM Kirumba mjini Mwanza)

68) AGOSTI 18, 2002 (Sunday)
Simba 1-1 Yanga
WAFUNGAJI:
Simba: Madaraka Selemani 65
Yanga: Sekilojo Chambua (penalti). dk. 89

69) NOVEMBA 10, 2002 (Sunday)
Simba 0-0 Yanga

70) SEPTEMBA 28, 2003 (Sunday)
Simba 2-2 Yanga
WAFUNGAJI:
Simba: Emmanuel Gabriel dk. 27 na 36
Yanga: Kudra Omary dk. 42, Heri Morris dk. 55

71) NOVEMBA 2, 2003 (Sunday)
Simba 0-0 Yanga

72) AGOSTI 7, 2004 (Saturday)
Simba 2-1 Yanga
WAFUNGAJI:
Simba: Shaaban Kisiga dk. 64, Ulimboka Mwakingwe dk. 76
Yanga: Pitchou Kongo dk. 48

73) SEPTEMBA 18, 2004 (Saturday)
Simba 1-0 Yanga
MFUNGAJI: Athumani Machuppa dk. 82

74) APRILI 17,  2005 (Sunday)
Simba 2-1 Yanga
WAFUNGAJI:
Simba: Nurdin Msiga dk. 44, Athumani Machupa dk. 64,
Yanga: Aaron Nyanda dk. 39
(Mechi hii ilichezwa Uwanja wa Jamhuri, Morogoro)

75) AGOSTI 21, 2005 (Sunday)
Simba 2-0 Yanga
MFUNGAJI: Nico Nyagawa dk. 22 na 56
(Mechi hii ilichezwa Uwanja wa Sheikh Amri Abeid mjini Arusha)

76) MACHI 26, 2006 (Sunday)
Simba 0-0 Yanga.

77) OKTOBA 29, 2006 (Sunday)
Simba 0-0 Yanga

78) JULAI 8, 2007 (Sunday)
Simba 1-1 Yanga
1-1 (dakika 120)
WAFUNGAJI:
Simba: Moses Odhiambo (penalti dk. 2)
Yanga: Said Maulid (dk. 55).
(Simba ilishinda kwa mikwaju ya penalti 5-4 baada ya sare hiyo).
(Mechi hii ilichezwa Uwanja wa Jamhuri, Morogoro)

79) OKTOBA 24, 2007 (Wednesday)
Simba 1-0 Yanga
Mfungaji: Ulimboka Mwakingwe
(Mechi hii ilichezwa Uwanja wa Jamhuri, Morogoro)

80) APRILI 27, 2008: (Sunday)
Simba 0-0 Yanga

81) OKT 26, 2008 (Sunday)
Yanga 1-0 Simba
MFUNGAJI: Ben Mwalala dk15.
(Mechi hii ilichezwa Uwanja mpya wa Taifa, Dar es Salaam)

82) APRILI  19, 2009 (Sunday)
Simba 2-2 Yanga
WAFUNGAJI:
SIMBA: Ramadhan Chombo dk 23, Haruna Moshi dk 62
YANGA: Ben Mwalala dk48, Jerry Tegete dk90
(Mechi hii ilichezwa Uwanja mpya wa Taifa, Dar es Salaam)
(Matokeo haya yanahusu mechi za Ligi ya Bara na iliyokuwa Ligi ya Muungano pekee)

83) OKTOBA 31, 2009 (Saturday)
Simba 1-0 Yanga
MFUNGAJI: Mussa Hassan Mgosi dk 26
(Mechi hii ilichezwa Uwanja mpya wa Taifa, Dar es Salaam)

84) APRILI 18, 2010 (Saturday)
Simba 4-3 Yanga
WAFUNGAJI:
SIMBA: Uhuru Suleiman dk 3, Mussa Mgosi dk 53 na 74, Hillary Echesa dk 90+
YANGA: Athumani Iddi dk 30, Jerry Tegete dk 69 na 89

85) OKTOBA 16, 2010 (Saturday)
Yanga 1-0 Simba
MFUNGAJI: Jerry Tegete dk 70

86) MACHI 5, 2011 (Saturday)
Simba 1-1 Yanga
WAFUNGAJI:
YANGA: Stefano Mwasyika (penalti) dk 59.
SIMBA:  Mussa Mgosi dk 73.
(Refa Orden Mbaga alizua tafrani uwanjani, kwanza kwa kulikataa bao la kusawazisha la Simba, kisha akalikubali baada ya kujadiliana na msaidia wake namba moja).

87) OKTOBA 29, 2011 (Saturday)
Yanga 1-0 Simba
MFUNGAJI: Davies Mwape dakika ya 75

88) MEI 6, 2012 (Sunday)
Simba 5-0 Yanga
WAFUNGAJI:
Emmanuel Okwi dk 1 na 65, Patrick Mafisango pen dk 58, Juma Kaseja pen dk 69 na Felix Sunzu pen dk 74

89) OKTOBA 3, 2012 (Wednesday)
Yanga 1-1 Simba
WAFUNGAJI:
Simba:Amri Kiemba Dk 4
Yanga:Said Bahanuzi (pen) Dk 65

90) MEI 18, 2013 (Saturday)
Yanga 2-0 Simba
WAFUNGAJI: Didier Kavumbagu dk 5 na Hamis Kiiza dk 62

91) OKTOBA 20, 2013 (Sunday)
Yanga 3-3 Simba
WAFUNGAJI:
Yanga:Mrisho Ngassa dk 14 na Hamis Kiiza dk 35 na 45
Simba:Betram Mombeki dk 55, Joseph Owino dk 57 na Gilbert Kazze dk 83

92) APRILI 19, 2014 (Saturday)
Simba 1-1 Yanga
WAFUNGAJI:
Simba:Haruna Chanongo dk 75
Yanga:Simon Msuva dk 86

93) OKTOBA 18, 2014 (Saturday)
Yanga 0-0 Simba

94) MACHI 8, 2015 (Sunday)
Simba 1-0 Yanga
MFUNGAJI: Emmanuel Okwi Dk 52

95) Septemba 26, 2015 (Saturday)
Simba 0-2 Yanga
WAFUNGAJI: Amissi Tambwe dk 44 na Malimi Busungu dk 76

96) Feb 20, 2016 (Saturday)
Yanga 2-0 Simba
WAFUNGAJI: Donald Ngoma dk 36 na Amissi Tambwe dk 72

97) Okt 01, 2016 (Saturday)
Yanga 1-1 Simba
WAFUNGAJI: Amissi Tambwe 26',  Shiza Kichuya 82'

98) Feb 25, 2017 (Saturday)
Simba 2-1 Yanga
WAFUNGAJI: Simon Msuva 5' pen; Laudit Mavugo 66' na Shiza Kichuya 81'

99) Okt 28, 2017 (Saturday)
Yanga 1-1 Simba
WAFUNGAJI: Obrey Chirwa 60'; Shiza Kichuya 57'

100) Apr 29, 2018 (Sunday)
Simba   ?? Yanga
 

Msimamo mechi za watani tangu 1965              P     W      D     L       F        A    PTS
YANGA    99    36    34    29    107    95    142
SIMBA     99    29    34    36    95    107    121

Kariakoo Derby, Kichuya ashindwe mwenyewe tu Uwanja wa Taifa

RAHMA WHITE
WAKATI mashabiki wa soka nchini na Afrika Mashariki wakihesabu saa zilizosalia kabla ya kitendawili cha nani mbabe kati ya wapinzani wa jadi wa soka nchini, Simba na Yanga hazijakutana jioni ya leo Jumapili hii katika pambano la Ligi Kuu, winga matata waSimba, Shiza Kichuya yupo katika nafasi nzuri ya kuandikisha rekodi tamu.
Kichuya anayeichezea Simba kwa msimu wa pili sasa tangu alipotua Msimbazi akitokea Mtibwa Sugar na kuifungia jumla ya mabao 19 katika Ligi Kuu, ni kati ya nyota watatu wanaoshikilia rekodi ya kufunga kwenye mechi tatu mfululizo wa watani.
Winga huyo anakula sahani moja na nyota wa zamani wa Simba, Madaraka Seleman 'Mzee wa Kiminyio' na straika wa Yanga, Amissi Tambwe, lakini kuwepo kwa mchezo wa Jumapili unampa nafasi mkali huyo kuwapiku wenzake na kuandika rekodi tamu.
Kama Kichuya atafanikiwa kuivuruga tena ngome ya Yanga na kufunga bao, atakuwa ndiye kinara na hivyo kuwapiku Madaraka aliyestaafu soka muda mrefu na Tambwe ambaye msimu huu amekuwa na wakati mgumu kuwa majeruhi wa muda mrefu.
Kichuya aliwafikia Mzee wa Kiminyio na Tambwe kwa mechi tatu zilizopita za watani ikiwamo ile ya kwanza kwanza akiwa na uzi wa Simba iliyopigwa Oktoba 1, 2016 akichomoa bao la Yanga liliwekwa na Tambwe na kusababisha vurugu za mashabiki.
Bao lake la pili alilitupia alipoisaidia Simba kuitungua Yanga katika mechi yao ya Februari 16 mwaka jana wakati Msimbazi wakiitambia Jangwani kwa mabao 2-1. Bao jingine la Simba lililokuwa la ushindi likiwekwa wavuni na Laudit Mavugo.
Katika mechi ya mwisho ya watani hao kukutana Oktoba 28, pia mwaka jana ikiwa mchezo wa duru la kwanza, Kichuya tena alifanya mambo ya kuitanguliza Simba kwa bao la dakika ya 57 kabla ya Obrey Chirwa kuisawazishia Yanga dakika tatu baadaye.
Kwa mazingira yaliyopo kwa winga huyo ni nafasi yake ya kuandika rekodi hiyo mpya kama ambavyo nyota wenzake, John Bocco na Emmanuel Okwi walivyo na kibarua cha kuvunja rekodi ya hat trick ya mechi ya watani inayoshikiliwa na Abdallah Kibadeni.
King Kibadeni aliandikisha rekodi hiyo iliyodumu kwa zaidi ya miaka 40 sasa katika pambano la kihistoria la watani lililopigwa Julai 19, 1977 wakati Simba ikiitambia Yanga kwa mabao 6-0, huku yeye akifunga matatu na mengine mawili yakiwekwa kimiani na Jumanne Hassan 'Masimenti' na beki wa Yanga Selemani Sanga alijifunga.
Pambano hilo la watani ambalo litakuwa la 100 tangu klabu hizo kongwe zianze kukutana katika mechi za Ligi ya Bara, inasubiri kuona rekodi mbalimbali zikivunjwa ikiwamo ya matokeo ya kipigo kikubwa ama sare ya maajabu zilizowahi kuwekwa 1996 na 2003 timu hizo zilipofungana mabao 4-4 na 3-3 mtawalia bila kutarajiwa.