STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, June 26, 2015

YANGA KUANIKA SILAHA ZAKE MBELE YA WAZIRI PINDA



http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/02/Mizengo-Pinda1.jpgSTRAIKA Donald Ngoma wa FC Platinum ya Zimbabwe alitarajiwa kutua nchini jioni ya leo na ilitarajiwa jioni ya kesho angeishuhudia Yanga inayotaka kumsajili ikitambulisha nyota wake wapya katika pambano dhidi ya Sc Villa ya Uganda.
Hata hivyo mchezaji huyo imeshindikana kutua leo, lakini hakuna kilichoharibika kwani Yanga itatambulisha nyota wake wote mbele ya Waziri Mkuu na Mtangaza Nia ya Urais, Mhe. Mizengo Pinda. Waziri Pinda atakuwepo katika pambano hilo ili kubariki silaha hizo mpya za Jangwani wakati wa mchezo huo maalum wa kuchangisha fedha za Ujenzi wa Majengo ya Watoto Wanaoisha katika Mazingira Magumu.
MKurugenzi wa asasi wa Nyumbani Kwanza, Mossy Magere aliiambia MICHARAZO MITUPU kuwa, Yanga itavaana na SC Villa ambapo pia kutakuwa na burudani ya kutosha kwa watakaohudhuria.
Mossy alisema kuwa, Waziri Pinda ndiye mgeni rasmi katika pambano hilo ambalo Yanga watalitumia kutambulisha nyota wake wapya na kusindikizwa na burudani ya muziki toka kwa kundi la Yamoto Band.
"Maandalizi yamekamilika na kwamba wageni mbalimbali tumewaalika, ila Waziri Pinda ndiye atakayekuwa mgeni rasmi na atabariki kikosi hicho cha kocha Hans Pluijm," alisema Mosi.
Mosi alisema kuwa SC Villa walitua juzi jioni wakiwa na kikosi cha wachezaji 18 na viongozi watano na kwamba jana walipasha misuli kwenye Uwanja wa Taifa kabla ya leo kuivaa Yanga.
Yanga ambao imetoka kuichapa Friends Rangers kwa mabao 3-2 katika mechi ya mazoezi, inauchukuliwa kwa uzito mkubwa mchezo huo wa leo kwani ni sehemu ya maandalizi ya ushiriki wao wa michuano ya Kagame na kocha atataka kupima uwezo wa wachezaji wao mbele ya Villa.
Baadhi ya wachezaji wapya wa Yanga ambao watakuwa majaribuni ni Malimi Busungu, Geofrey Mwashiuya na kipa Benedict Tinocco kwani Mwinyi Haji Ngwali na Deus Kaseke wapo kambi ya Taifa Stars kujiandaa na pambano la marudiano la kuwania Chan dhidi ya Uganda The Cranes.
Katibu Mkuu wa Yanga, Dk Jonas Tiboroha alinukuliwa juzi kuwa, huenda akawashtukiza mashabiki wa klabu hiyo katika mchezo huo wa kesho, bila kufafanua lakini imebainika ni kwamba Donald Ngoma alipangwa kuwepo uwanjani kuwashuhudia wenzake kwani angetua nchini ili kumalizana na klabu hiyo.

Jennifer Mgendi kufanya tamasha kubwa Dar Jumapili

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj7CxGiIU1N594esKNg1xe0mepyXDXaYznz92rl6kyK9TGgAbFQXUuEIonXEf3N5HWzU5AqbhmndSU2qveH5Qc0NqREOL9nlP95F4KqStJZMwq-XxH4wfAbnkufcoKfvtHZZh7_jyqffWUi/s1600/MGENDI.JPG
Jennifer Mgendi
MUIMBAJI nyota wa muziki wa Injili ambaye pia ni muigizaji na mtayarishaji wa filamu nchini, Jennifer Mgendi anajiandaa kuifanya tamasha kubwa kwa ajili ya Kumshukuru Mungu kwa kuweza kudumu kwenye fani hizo kwa miaka 20 sasa.
Jennifer alidokeza kuwa Tamasha hilo lililopewa jina la 'Tamasha la Miaka 20 ya Shukrani litafanyika kwenye Kanisa la DCT lililopo Tabata Shule karibu na Kituo cha Polisi Tabata siku ya Jumapili Juni 28 na kusindikizwa na wasanii mbalimbali wa muziki wa Injili nchini.
"Natarajia kufanya tamasha la Shukran ya Miaka 2o, litakalofanyika Juni 28 ambapo Mgeni Rasmi anatarajiwa kuwa Askofu Mkuu wa TIG, Dk Barnabas Mtokambali na waimbaji mbalimbali watanisindikiza akiwamo Bahati Bukuku, Bonny Mwaitege, Cosmas Chidumule, Ency Mwalukasa, Mchungaji Charles Jangalason na wengineo," alisema Jennifer.
Jennifer alisema ana haki ya kumshukuru Mungu kwa kumwezesha kumpa kipaji na kumwezesha kudumu katika huduma ya uimbaji kwa miaka hiyo yote 20.
Muimbaji huyo kwa sasa anatamba na albamu nane za muziki wa Injili tangu alipojitosa kwenye fani hiyo mwaka 1995 na katika tamasha hilo ataizundua video ya albamu yake inayotamba sasa ya 'WEMA NI AKIBA'.
Mbali na kwenye muziki, Jennifer pia anatamba kwenye filamu akiwa anakimbiza kwa sasa na kazi zake kadhaa ukiwamo 'Teke la Mama', 'Chai Moto', 'Pigo la Faraja', 'Mama Mkwe' na nyinginezo ambazo zimemfanya kuwa matawi ya juu licha ya kwamba hana makeke kama wasanii wengine.

Unyama! Watu 17 wauwawa hotelini

UNYAMA dhidi ya wanadamu umeendelea tena baa da ya Watu wenye silaha wameshambulia hoteli moja ya kitalii iliyoko kwenye pwani ya Tunisia na kuwauwa watu 27.
Maafisa wa serikali ya Tunisia wamesema kuwa mmoja wa washambuliaji hao aliuawa kwa kupigwa risasi na maafisa wa ulinzi na kuwa waliosalia bado wanasakwa na polisi.
Shambulio hilo lilitokea katika mji wa Sousse, ambao huwavutia maelfu ya watalii kutoka bara Ulaya na Afrika ya Kaskazini.
Hili lilikuwa shambulizi la pili dhidi ya hoteli ya watalii nchini Tunisia katika kipindi cha miezi michache iliyopita.
Inaaminika kuwa washambuliaji hao waliwavamia watalii ufukweni.
Mnamo mwezi Machi mwaka huu, wanamgambo wa Kiislamu waliokuwa wamejihami kwa bunduki waliwauawa zaidi ya watu 26 katika makavazi ya Bardo, iliyoko katika mji mkuu wa nchi hiyo Tunis.
Makavazi hayo ya Bardo hilo lilikuwa maarufu sana kwa watalii.
October mwaka wa 2013, mlipuaji wa kujitoa, alijilipua nje ya nyumba moja mjini Sousse, baada ya maafisa wa polisi kutibua jaribio lake la kutaka kuingia ndani na kuishambulia.
BBC

Simba waiwahi TFF kuhusu makocha wa makipa

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi-ErV4LDze29At9zLOJ5-K7zmESxzpny61EoTZ3Oj0BwcGnaHSSYJesvEuGbG8W3_LmcXp-5IKsJPPyMBUZZ6N0_rCe840K_0q4lFxI8OEaEgFOGs4iLDRaMuGeQX20S4EGDP4_CFZ-_A/s1600/Simba+logo+white.jpg
SIMBA wajanja sana, wakati Shirikisho la Mpira wa Mpira wa Miguu nchini (TFF) likitoa agizo na kuvioomba klabu zote zinavyoshiriki Ligi Kuu ya Vodacom kuwasilisha jina la kocha wa magolikipa kufikia jumatatu ya tarehe 29 Juni, 2015 katika ofisi za TFF, tayari klabu hiyo imeshamleta kocha wake kutoka Kenya, Abdul Salim.
TFF imeandaa kozi ya magolikipa hivyo inahitaji kupata jina la kila kocha wa magolikipa ili kuweza kushiriki kwenye kozi hiyo itakayoanza tarehe 13 - 17 Julai, 2015 jijini Dar es Salaam kwa mpango huo Simba itakuwa imeikatia denge TFF mapema. Coastal Union nayo ilifanya yao mapema juzi baada ya kumsainisha kocha wa zamani wa KCC ya Uganda, Lumu Fred ili kuwanoa makipa wa timu hiyo itakayokuwa chini ya Kocha Mkuu, Jackson Mayanja pia wa Uganda aliyekuwa akiinoa Kagera Sugar katika msimu uliopita.

SITA ZAPANDA DARAJA, MADINI ARUSHA NAO WAMO!

KLABU za Abajalo FC ya Tabora, Alliance FC (Mwanza), Changanyikeni Rangers FC (Dar es Salaam), Coca-Cola Kwanza FC (Mbeya), Madini SC (Arusha), na Sabasaba United FC (Morogoro) ndizo timu zilizopanda kucheza Ligi Daraja la Pili (SDL) msimu wa 2015/2016.
Timu hizo zimepanda daraja baada ya kufanya vizuri kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa wa Mikoa (RCL) iliyomalizika hivi karibuni kwenye vituo vya Lindi, Manyara na Rukwa na kushirikisha jumla ya timu 27.

SDL inayoshirikisha timu 24 zilizogawanywa katika makundi manne inatarajia kuanza kutimua vumbi Oktoba 17 mwaka huu. Ligi hiyo itachezwa kwa mtindo wa nyumbani na ugenini, na timu itakayoongoza kundi ndiyo itakayopanda daraja kucheza Ligi Daraja la Kwanza (FDL) kwa msimu wa 2016/2017.

Kundi A lina timu za Abajalo FC (Tabora), Green Warriors (Dar es Salaam), Milambo FC (Tabora), Mvuvumwa FC (Kigoma), Singida United (Singida) na Transit Camp (Dar es Salaam).

Kundi B lina timu za AFC (Arusha), Alliance FC (Mwanza), Bulyanhulu FC (Shinyanga), JKT Rwamkoma FC (Mara), Madini SC (Arusha) na Pamba SC (Mwanza).

Wakati kundi C lina timu za Abajalo FC (Dar es Salaam), Changanyikeni Rangers FC (Dar es Salaam), Cosmopolitan (Dar es Salaam), Kariakoo FC (Lindi), Mshikamano FC (Dar es Salaam) na Villa Squad (Dar es Salaam).

African Wanderers ya Iringa, Coca-Cola Kwanza FC (Mbeya), Mkamba Rangers (Morogoro), Sabasaba United FC (Morogoro), Town Small Boys (Ruvuma) na Wenda FC ya Mbeya ndizo zinazounda kundi D.

Dirisha la usajili wa wachezaji limeshafunguliwa tangu Juni 15 mwaka huu, na litafungwa Agosti 6 mwaka huu.

TFF yavichimba mkwara vyama vya soka mikoani

KUFUATIA pendekezo la sekretariet ya TFF ambalo baadae lilipitishwa na Mkutano Mkuu wa TFF kila mkoa unatakiwa kuwa na kituo chake cha kulea na kukuza vipaji vya mpira wa vijana umri kuanzia miaka 8-17.

Kwa mikoa ambayo tayari ina kituo ambacho inakiendesha yenyewe TFF inaonba ipatiwe taarifa hiyo ikiwa ni pamoja na kufahamishwa jina la kituo, jina la mwalimu na sifa zake na utaratibu wa mafunzo.

Kwa mikoa ambayo haina kituo TFF inagiza mikoa hiyo kuingia ubia na kituo kimoja ambacho tayari kina program ya kukuza na kuendeleza vipaji ili kijulikane kuwa ni kituo maalum cha mkoa husika.

Katika hilo TFF inaagiza kamati ya utendaji ya mkoa husika iandae muhtasari wa kikao cha utendaji cha chama cha mkoa wa kupitisha maamuzi hayo, MoU (makubaliano rasmi) yasainiwe kati ya chama cha mkoa na kituo husika na hati hiyo nakala yake iletwe TFF.

MoU hiyo ionyeshe majukumu ya chama cha mpira cha mkoa kama kutoa vifaa, kutoa mwalimu, usimamizi nk na pia kuonyesha majukumu ya mwenye kituo kama kutoa uwanja,ulinzi nk. MoU itaonyesha pia nani atafaidika na vipaji vitakavyoibuliwa kati ya mzazi,kituo na chama cha mkoa.

TFF itaandaa MoU ya mfano kwa ajili ya vyama vyote vya mikoa na ingependa kufikia tarehe 31/Desemba/2015 kila mkoa uwe umetekeleza jambo hilo
.

Stars ya Kwanza yaanza kujifua jijini Dar

Kocha wa Stars, Boniface Mkwasa (kulia)
KIKOSI cha timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) kinachodhaminiwa na bia ya Kilimanjaro Premium Lager kimeanza mazoezi leo asubuhi katika uwanja wa Boko Veterani kujiandaa na mchezo wa marudaino kuwania kufuzu kwa CHAN dhidi ya uganda mwishoni mwa wiki ijayo.

Stars inayonolewa na makocha wazawa, Charles Mkwasa na msaidizi wake Hemded Morocco, itakua ikifanya mazoezi asubuhi na jioni katika uwanja huo wa Boko Veterani, huku timu ikiweka kambi yake katika hoteli ya Kiromo mjini Bagamoyo.

Wachezaji wote walioitwa wameripoti kambini tangu jana na leo wamefanya mazoezi asubuhi isipokua Aggrey Morris ambaye ni majeruhi nafasi yake imekuchukuliwa na Vicent Andrew (Mtibwa Sugar) na Jonas Mkude aliyekwenda kufanya majaribio Afrika Kusini nafasi yake ikizibwa na Mudathir Yahya (Azam FC).

TFF yafunga kozi ya Makocha wa Vijana

Viongozi wa TFF, Rais Jamal Malinzi na Katibu Mkuu, Celestine Mwesigwa
SHIRIKISHO la Soka Nchini (TFF) leo limefungua kozi ya makocha wa mpira wa miguu kwa watoto na vijana kwa nchi nzima kwa lengo la kuhakikisha vijana wengi wanapata nafasi ya kufundishwa mpira na kuucheza mpira kuanzia katika umri mdogo.

Akifungua kozi hiyo, Katibu Mkuu wa TFF Mwesigwa Selestine amesema ili nchi/Taifa lifanikiwe katika soka ni lazima kuwekeza katika mpira wa watoto na vijana ambao makocha hao ni sehemu ya uwekezaji huo.

“Tumekua na mashindano ya Taifa U-13, kikosi cha timu ya Taifa ya U-15 ambayo inashirikisha vijana wadogo, vijana hao wanapaswa kupata malezi na mafunzo yenu waalimu ili wafikiapo kuchezea timu za Taifa wawe wamekua kwenye msingi bora wa kuujua mpira wa miguu” alisema Mwesigwa.

Naye mkufunzi wa FIFA wa kozi hiyo ya makocha kutoka nchini Ujerumani, Eric Muller amesema hata ujerumani imefanikiwa baada ya kuwekeza katika soka la vijana, mwaka 2000 kwenye fainali za Euro nchi yao ilishika nafasi ya mwisho katika msimamo kundi lao kwa kupata poniti moja, lakini uwekezaji walioufanya kwenye soka la watoto na vijana umewapelekea kutwaa Ubingwa wa Dunia mwaka 2014.

Washiriki wa kozi hiyo ni makocha wa timu za vijana za mikoa yoye Tanzania, ambao watashirki na timu zao za mikoa katika michuano ya Copa Coca Cola mwaka huu.

Kozi hiyo ya makocha wa timu za watoto/vijana inayoendeshwa na wakufunzi wa FIFA, Ulric Mathews kutoka shelisheli na Eric Muller kutoka nchini Ujerumani itamalizika jumatatu tarehe 29 Juni, 2015
.

Kazi imeanza, makocha Simba watua

Alianza huyu wa Kenya kwanza
Mwishowe wakakutana wote kwa pamoja
KLABU ya Simba imeonyesha haina utani baada ya makocha wake wapya Dylan Kerr kutoka Uingereza na Abdul Salim kutoka Kenya atakayewanoa makipa kutua nchini mchana huu wakitokea makwao.
Makocha hao wamelamba shavu la kuinoa Simba baada ya aliyekuwa kocha wa klabu hiyo, Goran Kopunovic kushindwa kuelewana na uongozi wa Rais Evans Aveva.
Kocha wa kwanza kutua nchini alikuwa Mkenya aliyewahi kuzinoa timu mbalimbali ikiwamo Gor Mahia na AFC Leopard ambaye alitua majira ya saa nane mchana kabla ya Kerry kutua saa 10 kwa Ndege ya Shirika la Emirates.
Makocha hao wametua tayari kuanza yao katika klabu hiyo ambayo kwa miaka mitatu sasa haijaonja taji la Ligi Kuu, huku ikiwa imebadilisha makocha wasiopungua watano tangu walipotwaa taji la mwisho msimu wa 2011-2012 ikiwa chini ya Cirkovic Milovan aliyefurshwa baadaye.
Kikosi cha wachezaji wa Simba kwa sasa wanajifua kwenye Gym ya Chang'ombe kabla ya kuanza rasmi mazoezi yao Julai Mosi ambapo Rais Aveva alidokeza kuwa itakuwa visiwani Zanzibar kwa muda wa majuma sita.
Hata hivyo Simba itaanza kambi hiyo bila baadhi ya nyota wake kadhaa wakiwamo wale waliopo katika kikosi cha timu ya taifa, Taifa Stars inayojiandaa kuifuata Uganda the Cranes katika pambano la marudiano la kuwania fainali za CHAN-2016 zitakazofanyika Rwanda.
Wengine ambao hawatakuwapo ni Jonas Mkude aliyetimkia Afrika Kusini kwa ajili ya kufanya majaribio ya kucheza soka la kulipwa katika klabu ya Afrika Kusini, huku Okwi akiwa kwao kwa ajili ya Fungate ya Arusi yao anayofunga kesho kwao Uganda na Raphael Kwireza akiwa amepewa mapumziko ya mwezi mmoja kusikilia majereha yake yanayomtibulia kukipiga Msimbazi licha ya kuwa na mkataba wa miaka miwili unaomalizika mwakani.

Wednesday, June 24, 2015

Mkwasa aanza mambo Stars amrudisha Barthez

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhis1ruGzLmA1ni2IyaqnEsKPAAEcU8JO7z8W9li0En3Om_Boh3slIOKzhOTagB1Zu0FOQX-o3UpDYsxHBOmjwTFUuzSFtBgGlYmjZwAXkl0M_f-9MAmTsfs2ZcGHTmYwU-tCrQRuZ8DReg/s1600/Kocha+Mkwasa+%2528kushoto%2529+na+msaidizi+wake+Hemed+Morocco+wakiongea+na+waandishi+wa+habari.jpgKOCHA Mkuu Mpya wa Taifa Stars, Charles Boniface Mkwasa ameanza mambo yake baada ya kutangaza kikosi cha wachezaji 26 akimjumuisha kipa wa Yanga Ally Mustafa 'Barthez'.
Mkwasa alitangaza kikosi hicho kilichowajumuisha pia mshambuliaji wa JKT Ruvu Samuel Kamuntu, huku pia akitangaza jopo lake la Benchi la Ufundi atakalosimamia akisaidiana na Hemed Morocco.
Wachezaji walioitwa kwa ajili ya pambano la marudiano la kuwania kucheza fainali za Chan 2016 dhidi ya Uganda The Cranes ni; Makipa: Mudathir Khamis (KMKM), Mwadini Ally (Azam), Ally Mustafa “Barthez” (Yanga).
Walinzi: Shomari Kapombe (Azam), Michael Aidan (Ruvu Shooting), Mohamed Hussein “Tshabalala” (Simba), Haji Mwinyi (KMKM), Nadir Haroub “Cannavaro” (Yanga), Kelvin Yondani (Yanga), Hassan Isihaka (Simba), Aggrey Morris (Azam).
Viungo: Jonas Mkude (Simba), Abdi Banda (Simba), Salum Telela (Yanga), Frank Domayo (Azam).
Mawinga: Saimon Msuva (Yanga), Said Ndemla (Simba), Deus Kaseke (Mbeya City), Ramadhan Singano “Messi” (Simba).
Washambuliaji: John Bocco (Azam), Atupele Green (Kagera Sugar), Rashid Mandawa (Kagera Sugar) na Ame Ally (Mtibwa Sugar).
Wachezaji Juma Abdul (Yanga), Mudathir Yahya (Azam) na Samwel Kamuntu (JKT Ruvu) wameitwa kama wachezaji wa akiba katika kikosi cha timu ya Taifa kinachoingia kambini kesho.
Katika hatua nyingine Mkwasa ametangaza benchi la ufundi la Taifa Stars, kocha msaidizi Hemed Morocco, kocha wa magolikipa Peter Manyika, Mshauri wa timu Abdallah Kibadeni, mtunza vifaa Hussein Swedi Gaga huku mratibu wa timu akiwa ni Alhaj Ahmed Mgoyi.
Kamati ya tiba ya TFF itapendekeza majina ya daktari wa timu na mchua misuli watakaoungana na kambi ya Taifa Stars

Jackson Mayanja atua Coastal, Kabange amfuata Tanga

https://thumbp22-ne1.mail.yahoo.com/tn?sid=2126005954&mid=AKh2imIAABLOVYqUbQ6C2E2ZEoE&midoffset=2_0_0_1_3671977&partid=3&f=1214&fid=Inbox&m=ThumbnailService&w=3000&h=3000
Kocha Jackson Mayanja akiweka dole gumba katika mkataba wa kuifundisha Coastal msimu ujao anayemuangalia ni Katibu Mkuu, Kassim El Siagi
https://thumbp22-ne1.mail.yahoo.com/tn?sid=2126005954&mid=AKh2imIAABLOVYqUbQ6C2E2ZEoE&midoffset=2_0_0_1_3671977&partid=4&f=1214&fid=Inbox&m=ThumbnailService&w=3000&h=3000Na Tariq Kimwaga, Tanga
MABINGWA wa Ligi kuu soka Tanzania bara mwaka 1988,Coastal Union,Wagosi wa Kaya imeingia mkataba wa miaka miwili na aliyekuwa Kocha Mkuu wa Kagera Sugar, Jackson Mayanja ambaye ni raia wa Uganda kuifundisha timu ya Coastal Union katika msimu ujao wa Ligi kuu soka Tanzania Bara itakayoanza Mwezi Agosti mwaka huu .
Utiliaji wa saini wa Kocha huyo ulifanyika (leo)jana mjini hapa na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa timu ya Coastal Union akiwemo Mjumbe wa Kamati ya Utendaji Albert Peter na Katibu Mkuu wa timu hiyo,Kassim El Siagi.
Akizungumza baada ya kumalizika zoezi hilo,Ofisa Habari wa Coastal Union,Oscar Assenga amesema kuwa kutokana na umahiri aliokuwa nao kocha huyo wanaimani kubwa ataipa mafanikio timu hiyo hasa katika harakati za kuhakikisha inafanya vizuri ligi kuu msimu ujao.
Amesema kuwa uwezo wa Kocha huyo utaleta matumaini makubwa ya mafanikio hasa ukizingatia ni kocha mwenye uwezo mzuri wa kufundisha na kuzipa mafanikio timu hivyo tunaamini kuja wake kwetu itakuwa chachu katika maendeleo.
Mayanja ambaye aliwahi kuzifundisha timu za soka Kiyuvu FC ya Rwanda,Timu ya Mamlaka ya Mapato nchini Uganda (URA),Vipers  FC ya Bunamwaya  na KCC ya Uganda amesema kutua kwenye timu hiyo kumpa faraja kubwa hivyo atahakikisha anatoa mchango wake kwenye kuipa mafanikio.
Amesema kuwa mipango yake mikubwa ni kuhakikisha timu hiyo inang’ara katika michuano ya Ligi kuu msimu ujao ikiwemo kubadili aina ya mchezo wa timu hiyo ili iweze kupata mafanikio kwa kuweka umoja baina ya wachezaji mashabiki, wanachama na wapenzi.
Amesistiza pia umuhimu wa mshikamano baina ya wapenzi,wanachama na viongozi ili kuiwezesha timu hiyo kuchukua Ubingwa wa Ligi kuu msimu ujao kwani dhamira yake ni kutaka kuona timu hiyo inang’ara kwenye medani za kitaifa na kimataifa.
Katika hatua nyingine aliyekuwa msaidizi wa Mayanja ndani ya Kagera Sugar, Mrage Kabange ameamua kumfuata bosi wake mjini Tanga kwa kusaini African Sports.
Kabange amechukuliwa na Wana Kimanumanu waliopanda Ligi Kuu msimu ujao baada ya kutemeshwa kazi kwa Wakata Miwa mara baada ya msimu wa 2014-2015 kumalizika Mei 9 mwaka huu.

Monday, June 22, 2015

HUYU NDIYE KOCHA MKUU MPYA WA SIMBA

SIMBA SC imeingia Mkataba wa miaka mwaka mmoja na kocha Dylan Kerr (pichani) mzaliwa wa Malta na mchezaji wa zamani wa England kwa ajili ya kuinoa klabu hiyo kuanzia Julai 1 mwaka huu. BIN ZUBEIRY inafahamu kocha huyo aliyezaliwa Januari 14 mwaka 1967 mjini Valletta amefikia makubaliano ya kuingia Mkataba wa mwaka mmoja na Simba SC wenye kipengele cha kuongezewa mmoja mwingine, iwapo atafanya kazi nzuri. Uongozi wa Simba SC wakati wote unakiri kuleta kocha Muingereza, lakini umekuwa ukigoma kutaja jina, ingawa BIN ZUBEIRY baada ya uchunguzi wa kina, imefanikiwa kumbaini mwalimu mpya wa Wekundu wa Msimbazi.
DYLAN KERR NI NANI NA AMETOKEA WAPI? Kerr anakuja Simba SC akitokea klabu ya Ligi Kuu ya Vietnam, Hai Phong aliyojiunga nayo Januari mwaka 2014. Huyo ni beki wa zamani wa kushoto aliyeibukia klabu ya Sheffield Wednesday mwaka 1984. Hakucheza mechi yoyote ya Ligi Kuu katika miaka yake minne ya kuwa na klabu hiyo ya Hillsborough hivyo akahamia Arcadia Shepherds ya Afrika Kusini mwaka 1988. Mwaka mmoja baadaye akarejea England kujiunga na Leeds United, ambako alicheza mechi 13 tu za Ligi Kuu katika miaka yake minne Elland Road kabla ya kutolewa kwa mkopo katika klabu mbili, kwanza Doncaster Rovers alikofunga bao lake la kwanza katika ligi, kisha Blackpool.  Katika miezi yake mitatu ya kuwa na Blackpool msimu wa 1991–1992, alifunga moja ya mabao katika ushindi wa 5-2 ugenini dhidi ya Lancashire na mabingwa wa Daraja, Burnley Uwanja wa Bloomfield Road. Mwaka 1993, Kerr akahamia Mortimer Common kujiunga na Reading, ambako alicheza mechi nyingi zaidi za ligi katika historia yake (89) na kufunga mabao matano.  Alikuwemo kwenye kikosi cha Royals kilichotwaa ubingwa wa Ligi Daraja la Pili, na wakati timu hiyo inashika nafasi ya pili katika Daraja la Kwanza msimu uliofuata alikuwepo kikosini. Mwaka 1996, Kerr akasaini Kilmarnock ya Scotland, ambako alicheza mechi 61 za ligi Killie katika miaka minne. Mwishoni mwa msimu wake wa kwanza katika klabu hiyo, alishinda Kombe la Scotland, kabla ya kuumia nyonga na kuwa nje kwa zaidi ya mwaka.
Dylan Kerr enzi zake anacheza Ligi Kuu England
Mwonekano wa sasa wa kocha Dylan Kerr
Kerr akatemwa Kilmarnock, na baada ya mechi moja ya kucheza kwa mkopo Carlisle United akajiunga na Slough Town Oktoba mwaka 2000, kabla ya Septemba mwaka huo kujiunga kwa muda na Kidderminster Harriers, lakini Mkataba wake wa mwezi mmoja ukasitishwa kwa utovu wa nidhamu. Akarejea Scotland kujiunga na Hamilton Academical Januari mwaka 2001 na miaka mitatu iliyofuata akacheza timu za Exeter City kwa miezi mitatu, Greenock Morton, Harrogate Town, East Stirlingshire na Hamilton Academical kwa mara nyingine kabla ya kustaafu akiwa na Kilwinning Rangers mwaka 2003. Baada ya kutungika daluga zake, Kerr akaenda kufundisha Marekani klabu ya Phoenix, Arizona ambako baada ya kukosa viza ya kuishi nchini humo akalazimika kurejea Scotland, ambako alifanya kazi kama Ofisa Maendeleo wa Argyll na Bute kati ya mwaka 2005 na 2009. Septemba mwaka 2009, Kerr akasaini Mkataba wa kuwa kocha Msaidizi wa Mpumalanga Black Aces ya Afrika Kusini hadi Juni mwaka 2010 alipohamia Thanda Royal Zulu kama Kocha Msaidizi pia, 2011 akaenda Nathi Lions (Msaidizi), 2012 akaenda Khatoco Khanh Hoa (Msaidizi) na mwaka 2012 akasaini Mkataba wa kuwa kocha wa mazoezi utimamu wa mwili (feetness) wa timu ya taifa ya Vietnam. Mwaka 2013 akahamia Hai Phong kama Kocha Msaidizi pia, kabla ya mwaka 2013 kuwa Kocha Mkuu wa timu ya vijana chini ya umri wa miaka 21 ya Hai Phong na mwaka 2014 akawa kocha Mkuu wa Hai Phong, ambayo aliipa ubingwa wa Taifa wa nchi hiyo. Kocha huyo kijana, anakuja Simba SC kurithi mikoba ya Mserbia, Goran Kopunovic ambaye baada ya miezi sita ya kufundisha klabu hiyo akashindwana na uongozi juu ya dau la Mkataba mpya. 
Credit:BIn Zubeiry

Sunday, June 21, 2015

Kamara, Ngoma watua Jangwani kilaini, Azam Mmh!

http://taarifa.co.tz/wp-content/uploads/2015/05/donald-ngoma.jpg
Ngoma
http://api.ning.com/files/-hwEeqCyyzcUDSa8niMV*j4Gexh4YMQlbQbOpDDsm5bj8CsNc1iWuShfdoofoJoxVS3yme2QGbewS7taPYct0Vd6GrOaJlx*/2.JPG
Kamara mwenye jezi nyeusi akiwa na wachezaji wenzake wa Yanga
KAMATI ya Utendaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limebariki ongezeko la wachezaji wa kigeni kutoka watano hadi saba na kwa maana hiyo imetoa fursa kwa wachezaji waliokuwa wakiwaniwa na Yanga, Donald Ngoma wa Fc Platimuz ya Zimbabwe na Lansana Kamara toka Sierra Leone kuwa na nafasi kubwa ya kukipiga Jangwani.
Kadhalika ongezeko hilo ambalo hata hivyo limeenda kinyume na maombi ya Umoja wa Klabu ya kutaka wachezaji wa kigeni wafikie 10, litazinufaisha Azam na Simba zilizokuwa zikiipigia debe ongezeko hilo. 
Ebu isome mwenyewe taarifa ya TFF juu ya maamuzi yao ya Kamati ya Utendaji iliyokutana jana visiwani Zanzibar

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI - RELEASE NO. 101
TAREHE 20 JUNI, 2015
MAAMUZI YA KAMATI YA UTENDAJI
Kamati ya Utendaji ya TFF imefanya kikao chake cha kawaida leo tarehe 20/06/2015 katika ukumbi wa Wizara ya Habari, Utalii, Utamaduni na Michezo kisiwani Zanzibar,

Baadhi ya maamuzi yake ni haya yafuatayo:

  1. TUNZO ZA VODACOM.
Baada ya kuzingatia  mapungufu yaliyojitokeza katika uteuzi wa tuzo za ligi kuu ya Vodacom msimu wa 2014/15, Kamati ya utendaji imeagiza Rais wa TFF aunde kamati maalum ya kusimamia mchakato wa utoaji wa tuzo za Vodacom. Kamati hii itazingatia umuhimu wa kuhusisha idara za ufundi za TFF katika zoezi hilo na wadhamini na ligi watahusishwa kwa ukaribu katika zoezi hili.

  1. KANUNI ZA LIGI 2015/16.
Kamati ya utendaji ilipitia rasimu ya kanuni za ligi kuu, FDL na SDL za msimu ujao wa 2015/16.
Mabadiliko makubwa yaliyofanywa ni kwenye maeneo yafuatayo:

  1. LESENI ZA VILABU.
Kamati ya utendaji imesisitiza kuwa hakuna klabu itakayopitishiwa usajili wake kama kupewa leseni ya klabu ya msimu.( Club Licencing).

  1. WAAMUZI.
Kamati ya utendaji imeridhia wazo la kamati ya maamuzi kuwa kuanzia msimu 2015/16 kutakuwa na jopo maalum ya waamuzi ( Elite referees) litakalochezeshwa mechi zote za ligi kuu.

Waamuzi hawa watakuwa ni 16 wa kati, 32 wa pembeni na 4 wa akiba. Hii itasaidia kuongoza ufanisi katika uamuzi. (refereeing).

  1. MGAWANYO WA MAPATO YA MILANGONI.
Vilabu vimeongezwa mgawanyo wa mapato  ya milangoni na sasa vitakuwa vinachukua asilimia 60% ya mapato ya mlangoni, makato mengine ni 18% VAT na 15% gharama za uwanja.

  1. UDHIBITI WA WACHEZAJI.
Kanuni ilikuwa inatoa fursa timu ya kuamua mechi ipi mchezaji asicheze baada ya kuwa na kadi tatu za njano imefutwa.

  1. KUSAJILI MIKATABA YA WACHEZAJI.
Kuanzia sasa mikataba kati ya wachezaji na klabu itakayotambuliwa na TFF itakuwa ni ile ambayo ni nakala halisi zilizopigwa muhuri na lakiri ya TFF  na kusajiliwa kwenye kumbukumbu ya TFF. Vilabu na mwachezaji watapewa nakala hizi baada ya  kusajiliwa na TFF.

  1. WACHEZAJI WA KIGENI.
Kamati ya utendaji imeamua kuwa kuanzia msimu 2015/16 idadi ya wachezaji wa kigeni watakaosajiliwa na klabu ya ligi kuu itakuwa 7 (saba) wachezaji wote hawa, wote wataruhusiwa kucheza kwa wakati wote.

Mikakati ya kusajiliwa wachezaji hawa ni haya yafuatayo:
  1. Mchezaji awe ni mchezaji wa timu za Taifa za nchi yake ( Senior, U23, U20, U19, U17 nk) au
  2. Mchezaji awe anacheza katika ligi kuu ya nchi yake au nchi nyingine wakati anasajiliwa.

  1. Kila mchezaji wa kigeni atakayesajiliwa atalipia ada ya maendeleo. Mpira wa vijana ya dola 2,000 kwa kila msimu atakyocheza hapa nchini. Fedha hizi zitapelekwa katika mfuko wa maendeleo ya mpira (Football Development Fund).

Pia imeamriwa kuwa mikataba ya vilabu na wachezaji iliyo hai itaendelea kutambuliwa na TFF. Na kwa wale ambao tayari wapo nchini wataruhusiwa  kuuhisha (to renew) mikataba yao iwapo watakubaliana na vilabu vyao.

4. LESENI ZA MAKOCHA
Kamati ya utendaji imeamua kuwa kuanzia msimu huu, Kocha wa timu ya ligi kuu sharti awe na leseni B ya CAF au itakayolingana nayo kutoka katika mashirikisho mengine duniani na kocha msaidizi awe na leseni C ya CAF, hii ni kwa misimu mitatu.
Kuanzia msimu wa 2018/2019 kocha wa Ligi Kuu atatakiwa kuwa na leseni A ya CAF au inayolingana na hiyo kutoka katika mashirikisho mengine duniani.

Aidha Kamati ya Utendajji ya TFF imemteua Meshack Bandawe kuwa mjumbe wa bodi ya mfuko wa  maendeleo ya mpira wa miguu - TFF (FDF), Bandawe ni meneja wa PPF kanda ya ziwa.


IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)


Argentina yaifumua Jamaica kidude, yatinga robo fainali

Argentina
Safi sana kijana, Higuain (kulia) akipongezwa na Messi na Di Maria baada ya kufunga bao la mapema

Argentina 4
Messi akikikusanya kijiji kama kawaida yake
Argentina 5
Gonzalo Higuain akishangilia bao lililoivusha Argentina robo fainali za Copa America
BAO la dakika 11 ya Gonzalo Higuain kutokana na pazi murua ya Angel di Maria imeiwezesha Argentina kusonga mbele katika kundi lake kwenye michuano ya Copa America, huku Chile ikiitafanua Bolivia 5-0 na Uruguay na Paraguay wakitoshana nguvu katika mechi nyingine.
Argentina kwa ushindi huo imeongoza kundi lake la B kwa kufikisha pointi saba mbili zaidi ya Paraguay na zote zimesonga mbele hatua ya robo fainali.
Bolivia licha ya kupigwa mkono na Chile, lakini timu hizo mbili zimefuzu hatua ya robo fainali kutoka kundi A, huku kundi C likitarajiwa kutua washindi wao leo sambamba na timu mbili zitakazoungana na zilizofuzu moja kwa moja. Timu tatu za Uruguay, Venezuela na Ecuador zinawania nafasi ya Best Looser katika michuano hiyo.

Utukutu wamponza Neymar, afungiwa mechi nne Copa America

Mshikemshike baada ya Neymar kuzua tafran kwa kupiga mpira ulio 'mbabua' mgongoni mchezaji wa Colombia
Neymar (10) akizozana na wachezaji wa Colombia huku akizuiwa na wenzake wa Brazil
Neymar vurugu
Kwani we unataka nini? Neymar akizozana na wachezaji wa Colombia huku mwamuzi akiteta naye
AMA kweli hasira hasara! Straika tegemeo na nahodha wa timu ya taifa ya Brazil, Neymar Jr anatarajiwa kuikosa michuano ya Copa America inayoendelea nchini Chile baada ya kufungiwa kucheza mechi nne. 
Mshambuliaji huyo wa Barcelona mwenye umri wa miaka 23 alionyeshwa kadi nyekundu kwa kuzozana na wachezaji wa Colombia kufuatia kipigo cha bao bao 1-0 walichopata Brazil katika mchezo wao wa makundi. Mbali na kadi ya moja kwa moja, lakini inadaiwa kuwa Neymar alimtolea lugha ya matusi mwamuzi wa pambano hilo na ndiyo sababu ya kuadhibiwa kukosa mechi nyingine za ziada badala ya moja tu ya kadi aliyopewa.
Nyota huyo tayari anatumikia adhabu ya kutocheza mechi moja hivyo kumfanya kutokuwepo katika mchezo wa mwisho wa makundi dhidi ya Venezuela utakaochezwa usiku wa leo.
Lakini Shirikisho la Soka la Amerika Kusini sasa limepitia tukio hilo na kuongeza adhabu kwa nyota huyo baada ya kudaiwa ripoti ya mwamuzi ilitaarifa kumtusi. 
Mchezaji wa Colombia Carlos Bacca ambaye pia alipewa kadi nyekundu katika tukio hilo naye amepewa adhabu ya kutocheza mechi mbili huku wachezaji wote wakipewa nafasi ya kukata rufani kama hawakuridhika na adhabu.

The Cranes yamfukuzisha kazi kocha Nooij Taifa Stars

Bechi la ufundi
Kocha Stars na wenzake wakati wa wimbo wa Taifa kabla ya kuvaana na Uganda The Cranes
Kocha Nooij akisindikizwa na Polisi mara baada ya filimbi ya mwisho ya mchezo wa timu yake dhidi ya Uganda The Cranes am,bapo Stars ilichapwa mabao 3-0 kwenye Uwanja wa Amaan Zanzibar.
Na Mwandishi Wetu Zanzibar

SAFARI ya Kocha Mkuu wa timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars imeifikia tamati baada ya Kamati ya Utendaji ya TFF, kutangaza kulipiga chini benchi nzima baada ya timu hiyo kucharazwa mabao 3-0 na Uganda The Cranes.
Stars ilitandikwa mabao hayo katika mchezo wa kwanza wa kuwania fainali za Mataifa ya Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN) zitakazofanyika mwakani Rwanda, uliochezwa kwenye Uwanja wa Amaan, visiwani hapa.
Mara baada ya pambano hilo ambalo lilikuwa la 18 kwa Stars chini ya Kocha Nooij ikiwa imeshinda mechi tatu tu, moja likiwa la mashindano Kamati ya Utendaji ya TFF ilikutana na kutoa taarifa ya kumtimua kocha huyo na wasaidizi wake na taarifa za chini chini zinapasha kuwa Charles Boniface Mkwasa na Abdallah Kibadeni huenda wakapewa timu.

TFF ilimpa kocha Mart Nooij mtihani wa mwisho na endapo atashindwa kuipeleka Taifa Stars, basi atafute njia ya kuondoka baada ya wapenzi wa soka nchini kuchoshwa na ipigo ya timu hiyo.


Wiki iliyopita, Taifa Stars ilipokea kichapo cha idadi kama hiyo cha mabao kutoka kwa Misri katika mchezo wa kufuzu kwa fainali za Mataifa ya Afrika (Afcon) zitakazofanyika mwaka 2017 nchini Gabon.


Katika mchezo huo ambao Stars ilicheza kama isiyo na mwalimu ilijikuta ikienda mapumziko ikiwa nyuma kwa bao 1-0. bao hilo liliwekwa kimiani na Sekisambo Erisa ambaye alikuja kufunga bao jingine na kufanya aitungie Stars mara mbili na lingine lilifungwa na Miya Farouk.

Kabla ya kuanza mchezo huo, Taifa Stars ilipata pigo baada ya mchezaji wake Oscar Joshua kuugua ghafla na kuukosa mchezo huo.


Kwa mara ya mwisho Stars ilifuzu kwa fainali hizo za Chan mwaka 2009 zilipofanyika kwa mara ya kwanza nchini Iory Coast na ilitolewa katika hatua ya makundi ikiwa chini ya Mbrazil Marcio Maximo.


Mara baada ya pambano hilo mashabiki wenye hasira walitaka kumtandika kocha Nooij kabla ya askari Polisi waliokuwa uwanjani kumuokoa.
Tangu mapema mara baada ya kufungwa bao la kwanza, mashabiki waliibadilika Stars na kuanza kuizomea na kuwafanya wachezaji kupoteza kujiamini na kusababisha kufungwa mabao mengine yaliyoiweka timu hiyo katika wakati mgumu kusonga mbele kwenye michezzo hiyo ya Chan.
Stars na Uganda zitarudiana wiki mbili zijazo na mshindi atakayesonga mbele ataumana na Sudan katika raundi inayofuata.
Chini ni taarifa ya TFF juu ya kusitisha kibarua cha Kocha Nooij.

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
 20 JUNI, 2015
KAMATI YA UTENDAJI YASITISHA AJIRA YA NOOIJ
Kamati ya utendaji ya Shirikishi la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Katika kikao chake cha leo pamoja na mambo mengine ilipitia mwenendo wa Timu ya Taifa (Taifa Stars) ikiwa ni pamoja na kuhudhuria mchezo kati ya Tanzania na Uganda, kama sehemu ya tathmin ya mwenendo wa timu.

Kamati ya utendaji kwa kauli moja imeamua yafuatayo:

1.Ajira ya Kocha Mkuu Maart Nooij inasitishwa mara moja kuanzia  tarehe 21/June/2015.

2.Benchi lote la ufundi la Taifa stars limevunjwa kuanzia tarehe 21/06/2015.

3.Uongozi wa TFF utatangaza punde benchi jipya la ufundi la timu ya Taifa.

IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

Wednesday, June 17, 2015

Boateng kurejea tena San Siro

http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2014/06/26/article-2670725-1F2594FC00000578-295_634x645.jpgTENA? Aah haiwezekani! Wakala wa Kevin-Prince Boateng amethibitisha kuwa kiungo huyo anaweza kujiunga tena na AC Milan katika kipindi hiki cha majira ya kiangazi.
Nyota huyo wa kimataifa wa Ghana alikaa San Siro kwa miaka mitatu na kufanikiwa kushinda taji la Serie A katika msimu wake wa kwanza kabla ya kuondoka kwenda Schalke ya Ujerumani Agosti mwaka 2013. 
Hata hivyo, Boateng anataka kuondoka Schalke baada ya kusimamishwa na klabu hiyo Mei 11 mwaka huu kufuatia kichapo walichopata dhidi ya Koln. 
Wakala wa Boateng, Federico Pastorello amesema kwa sasa wanasubiri ofa, lakini akakiri kuwa uwezekano wa kurejea Milan ni mkubwa. 
Milan baada ya kumtimua kocha Filippo Inzaghi 'Pippo' na kumuajiri Sinisa Mihajlovic, inategemewa kutenga fungu kubwa kwa ajili ya usajili kiangazi hiki ili kurejesha makali yao baada ya kumaliza msimu wa Serie wakiwa nafasi ya 10.

Man City yaongeza dau kwa Sterling

http://a.espncdn.com/combiner/i/?img=/photo/2014/1002/soc_g_sterling_jv_1296x1296.jpg&w=1500&h=1500&scale=crop&site=espnfcBAADA ya kukaushiwa kimtindo na Liverpool, klabu ya Manchester City imeongeza ofa yao kufikia Pauni Milioni 35.5 kwa ajili ya kumwania Raheem Sterling,
Ofa ambayo kuna uwezekano pia wa kukataliwa na Liverpool kwani klabu hiyo wanamthaminisha mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Uingereza kuwa thamani ya ya Pauni Milioni 50. 
Wiki iliyopita Liverpool walikataa ofa ya Pauni Milioni 25 iliyotolewa na City kwa ajili ya nyota huyo. 
Sterling alijiunga na Liverpool akitokea Queens Park Rngers mwaka 2010 na bado ana mkataba na Liverpool unaomalizika mwaka 2017 pamoja na kukataa mkataba mpya ambao ungemuwezesha kulipwa kitita cha Pauni 100,000 kwa wiki. 
Meneja wa Liverpool, Brendan Rodgers amesema mwezi uliopita kuwa anategemea Sterling kubakia Anfield mpaka atakapomaliza mkataba wake.

Copy and WIN : haundi milioni 35.5 kwa ajili ya kumuwania Raheem Sterling, ofa ambayo kuna uwezekano pia wa kukataliwa na Liverpool. Liverpool wanamthaminisha mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Uingereza kuwa thamani ya ya paundi milioni 50. Wiki iliyopita Liverpool walikataa ofa ya paundi milioni 25 iliyotolewa na City kwa ajili ya nyota huyo. Sterling alijiunga na Liverpool akitokea Queens Park Rngers mwaka 2010 na bado ana mkataba na Liverpool unaomalizika mwaka 2017 pamoja na kukataa mkataba mpya ambao ungemuwezesha kulipwa kitita cha paundi 100,000 kea wiki. Meneja wa Liverpool Brendan Rodgers amesema mwezi uliopita kuwa anategemea Sterling kubakia Anfield mpaka atakapomaliza mkataba wake.

 and WIN : h

RATIBA YA LIGI KUU YA ENGLAND 2015-2016 HII HAPA



http://www.hdwallpapersinn.com/wp-content/uploads/2014/08/chelsea-football-club-full-team-celebrations-hd-wallpapers.jpg
Watetezi wa Ligi Kuu ya England

http://www.totalsportek.com/wp-content/uploads/2015/03/Premier-League-Fixtures.jpgRATIBA ya awali ya Ligi Kuu ya England, msimu wa 2015-2016 imetolewa ambapo watetezi wa taji hilo Chelsea wataanzia nyumbani dhidi ya Swansea City na itakuwa ni ukaribisho mzuri wa Andre Ayew Pele.
Mchezaji huyo wa Ghana amesajiliwa na Swansea na pambano hilo litakuwa kipimo tosha kwake kuonyesha kama anahimili ligi hiyo ya EPL.
Mashetani Wekundu wenyewe wataanzia pia nyumbani dhidi ya vijogoo vya London Kaskazini, Tottenham Hotspur, huku Arsenal nao wataanza kwa kupepetana na West Ham United na Liverpool na Manchester City zote kila mmoja zitaanzia ugenini katike mechi zao za kwanza Agopsti 8.

Ratiba kamili ya awali ya ligi hiyo imekaa hivi:



Jumamosi, Agosti 8, 2015

AFC Bournemouth   v Aston Villa

 Arsenal          v West Ham

 Chelsea          v Swansea City

 Everton          v Watford

 Leicester City   v Sunderland

 Man United       v Tottenham

 Newcastle v Southampton

 Norwich City     v Crystal Palace

 Stoke City       v Liverpool

 West Brom  v Man City



Jumamosi, Agosti 15, 2015

Aston Villa       v Man United

Crystal Palace    v Arsenal

Liverpool         v AFC Bournemouth

Man City          v Chelsea

Southampton       v Everton

Sunderland v Norwich City

Swansea City      v Newcastle

Tottenham  v Stoke City

Watford           v West Brom

West Ham    v Leicester City



Jumamosi, Agosti 22, 2015

Arsenal           v Liverpool

Crystal Palace    v Aston Villa

Everton           v Man City

Leicester City    v Tottenham

Man United v Newcastle

Norwich City      v Stoke City

Sunderland v Swansea City

Watford           v Southampton

West Brom   v Chelsea

West Ham    v AFC Bournemouth



Jumamosi, Agosti 29, 2015

AFC Bournemouth   v Leicester City

Aston Villa       v Sunderland

Chelsea           v Crystal Palace

Liverpool         v West Ham

Man City          v Watford

Newcastle   v Arsenal

Southampton       v Norwich City

Stoke City        v West Brom

Swansea City      v Man United

Tottenham   v Everton



Jumamosi, Septemba 12, 2015

Arsenal           v Stoke City

Crystal Palace    v Man City

Everton           v Chelsea

Leicester City    v Aston Villa

Man United v Liverpool

Norwich City      v AFC Bournemouth

Sunderland v Tottenhamr

Watford           v Swansea City

West Brom   v Southampton

West Ham    v Newcastle





Jumamosi, Septemba 19, 2015

AFC Bournemouth   v Sunderland

Aston Villa       v West Brom

Chelsea           v Arsenal

Liverpool         v Norwich City

Man City          v West Ham

Newcastle   v Watford

Southampton       v Man United

Stoke City        v Leicester City

Swansea City      v Everton

Tottenham   v Crystal Palace





Jumamosi, Septemba 26, 2015

Leicester City    v Arsenal

Liverpool         v Aston Villa

Man United v Sunderland

Newcastle   v Chelsea

Southampton       v Swansea City

Stoke City        v AFC Bournemouth

Tottenham   v Man City

Watford           v Crystal Palace

West Brom   v Everton

West Ham    v Norwich City





Jumamosi, Oktoba 3, 2015

AFC Bournemouth   v Watford

Arsenal           v Man United

Aston Villa       v Stoke City

Chelsea           v Southampton

Crystal Palace    v West Brom

Everton           v Liverpool

Man City          v Newcastle

Norwich City      v Leicester City

Sunderland v West Ham

Swansea City      v Tottenham





Jumamosi, Oktoba 17, 2015

Chelsea           v Aston Villa

Crystal Palace    v West Ham

Everton           v Man United

Man City          v AFC Bournemouth

Newcastle  v Norwich City

Southampton       v Leicester City

Swansea City      v Stoke City

Tottenham  v Liverpool

Watford           v Arsenal

West Brom   v Sunderland



Jumamosi, Oktoba 24, 2015

AFC Bournemouth   v Tottenham

Arsenal           v Everton

Aston Villa       v Swansea City

Leicester City    v Crystal Palace

Liverpool         v Southampton

Man United v Man City

Norwich City      v West Brom

Stoke City        v Watford

Sunderland v Newcastle

West Ham    v Chelsea



Jumamosi, Oktoba 31, 2015

Chelsea           v Liverpool

Crystal Palace    v Man United

Everton           v Sunderland

Man City          v Norwich City

Newcastle   v Stoke City

Southampton       v AFC Bournemouth

Swansea City      v Arsenal

Tottenham   v Aston Villa

Watford           v West Ham

West Brom   v Leicester City



Jumamosi, Novemba 7, 2015

AFC Bournemouth   v Newcastle

Arsenal           v Tottenham

Aston Villa       v Man City

Leicester City    v Watford

Liverpool         v Crystal Palace

Man United v West Brom

Norwich City      v Swansea City

Stoke City        v Chelsea

Sunderland v Southampton

West Ham    v Everton



Saturday, November 21st, 2015

Chelsea           v Norwich City

Crystal Palace    v Sunderland

Everton           v Aston Villa

Man City          v Liverpool

Newcastle  v Leicester City

Southampton       v Stoke City

Swansea City      v AFC Bournemouth

Tottenham   v West Ham

Watford           v Man United

West Brom   v Arsenal



Jumamosi, Novemba 28, 2015

AFC Bournemouth   v Everton

Aston Villa       v Watford

Crystal Palace    v Newcastle

Leicester City    v Man United

Liverpool         v Swansea City

Man City          v Southampton

Norwich City      v Arsenal

Sunderland v Stoke City

Tottenham   v Chelsea

West Ham          v West Brom



Jumamosi, Desemba 5, 2015

Arsenal           v Sunderland

Chelsea           v AFC Bournemouth

Everton           v Crystal Palace

Man United v West Ham

Newcastle  v Liverpool

Southampton       v Aston Villa

Stoke City        v Man City

Swansea City      v Leicester City

Watford           v Norwich City

West Brom   v Tottenham



Jumamosi, Desemba 12, 2015

AFC Bournemouth   v Man United

Aston Villa       v Arsenal

Crystal Palace    v Southampton

Leicester City    v Chelsea

Liverpool         v West Brom

Man City          v Swansea City

Norwich City      v Everton

Sunderland v Watford

Tottenham  v Newcastle

West Ham    v Stoke City



Januari, Desemba 19, 2015

Arsenal           v Man City

Chelsea           v Sunderland

Everton           v Leicester City

Man United v Norwich City

Newcastle   v Aston Villa

Southampton       v Tottenham

Stoke City        v Crystal Palace

Swansea City      v West Ham

Watford           v Liverpool

West Brom   v AFC Bournemouth



Jumamosi, Desemba 26, 2015

AFC Bournemouth   v Crystal Palace

Aston Villa       v West Ham

Chelsea           v Watford

Liverpool         v Leicester City

Man City          v Sunderland

Newcastle   v Everton

Southampton       v Arsenal

Stoke City        v Man United

Swansea City      v West Brom

Tottenham   v Norwich City



Jumatatu, Desemba 28, 2015

Arsenal           v AFC Bournemouth

Crystal Palace    v Swansea City

Everton           v Stoke City

Leicester City    v Man City

Man United v Chelsea

Norwich City      v Aston Villa

Sunderland v Liverpool

Watford           v Tottenham

West Brom   v Newcastle

West Ham    v Southampton



Jumamosi, Januari 2, 2016

Arsenal           v Newcastle

Crystal Palace    v Chelsea

Everton           v Tottenham

Leicester City    v AFC Bournemouth

Man United v Swansea City

Norwich City      v Southampton

Sunderland v Aston Villa

Watford           v Man City

West Brom   v Stoke City

West Ham    v Liverpool



Jumanne, Januari 12, 2016

AFC Bournemouth   v West Ham

Aston Villa       v Crystal Palace

Liverpool         v Arsenal

Swansea City      v Sunderland



Jumatano, Januari 13, 2016

Chelsea           v West Brom

Man City          v Everton

Newcastle   v Man United

Southampton       v Watford

Stoke City        v Norwich City

Tottenham   v Leicester City



Jumamosi, Januari 16, 2016

AFC Bournemouth   v Norwich City

Aston Villa       v Leicester City

Chelsea           v Everton

Liverpool         v Man United

Man City          v Crystal Palace

Newcastle   v West Ham

Southampton       v West Brom

Stoke City        v Arsenal

Swansea City      v Watford

Tottenham   v Sunderland



Jumamosi, Januari 23, 2016

Arsenal           v Chelsea

Crystal Palace    v Tottenham

Everton           v Swansea City

Leicester City    v Stoke City

Man United v Southampton

Norwich City      v Liverpool

Sunderland v AFC Bournemouth

Watford           v Newcastle

West Brom   v Aston Villa

West Ham    v Man City



Jumanne, Februari 2, 2016

Arsenal           v Southampton

Crystal Palace    v AFC Bournemouth

Leicester City    v Liverpool

Man United v Stoke City

Norwich City      v Tottenham

Sunderland v Man City

Watford           v Chelsea

West Brom   v Swansea City

West Ham    v Aston Villa



Jumatano, Februari 3, 2016

Everton           v Newcastle



Jumamosi, Februari 6, 2016

AFC Bournemouth   v Arsenal

Aston Villa       v Norwich City

Chelsea           v Man United

Liverpool         v Sunderland

Man City          v Leicester City

Newcastle  v West Brom

Southampton       v West Ham

Stoke City        v Everton

Swansea City      v Crystal Palace

Tottenham   v Watford



Jumamosi, Februari 13, 2016

AFC Bournemouth   v Stoke City

Arsenal           v Leicester City

Aston Villa       v Liverpool

Chelsea           v Newcastle

Crystal Palace    v Watford

Everton           v West Brom

Manchester City   v Tottenham

Norwich City      v West Ham

Sunderland v Man United

Swansea City      v Southampton



Jumamosi, Februari 27, 2016

Leicester City    v Norwich City

Liverpool         v Everton

Man United v Arsenal

Newcastle   v Man City

Southampton       v Chelsea

Stoke City        v Aston Villa

Tottenham   v Swansea City

Watford           v AFC Bournemouth

West Brom   v Crystal Palace

West Ham          v Sunderland





Jumanne, Machi 1, 2016

AFC Bournemouth   v Southampton

Arsenal           v Swansea City

Aston Villa       v Everton

Leicester City    v West Brom

Liverpool         v Man City

Man United v Watford

Norwich City      v Chelsea

Sunderland v Crystal Palace

West Ham          v Tottenham



Jumatano, Machi 2, 2016

Stoke City        v Newcastle



Jumamosi, Machi 5, 2016

Chelsea           v Stoke City

Crystal Palace    v Liverpool

Everton           v West Ham

Man City          v Aston Villa

Newcastle   v AFC Bournemouth

Southampton       v Sunderland

Swansea City      v Norwich City

Tottenham   v Arsenal

Watford           v Leicester City

West Brom   v Man United



Jumamosi, Machi 12, 2016

AFC Bournemouth   v Swansea City

Arsenal           v West Brom

Aston Villa       v Tottenham

Leicester City    v Newcastle

Liverpool         v Chelsea

Man United v Crystal Palace

Norwich City      v Man City

Stoke City        v Southampton

Sunderland v Everton

West Ham    v Watford



Jumamosi, Machi 19, 2016

Chelsea           v West Ham

Crystal Palace    v Leicester City

Everton           v Arsenal

Man City          v Man United

Newcastle   v Sunderland

Southampton       v Liverpool

Swansea City      v Aston Villa

Tottenham   v AFC Bournemouth

Watford           v Stoke City

West Brom   v Norwich City



Jumamosi, Aprili 2, 2016

AFC Bournemouth   v Man City

Arsenal           v Watford

Aston Villa       v Chelsea

Leicester City    v Southampton

Liverpool         v Tottenham

ManUnited   v Everton

Norwich City      v Newcastle

Stoke City        v Swansea City

Sunderland v West Brom

West Ham    v Crystal Palace





Jumamosi, Aprili 9, 2016

 Aston Villa      v AFC Bournemouth

 Crystal Palace   v Norwich City

 Liverpool        v Stoke City

 Man City         v West Brom

 Southampton      v Newcastle

 Sunderland       v Leicester City

 Swansea City     v Chelsea

 Tottenham  v Man United

 Watford          v Everton

 West Ham   v Arsenal



Jumamosi, Aprili 16, 2016

 AFC Bournemouth v Liverpool

 Arsenal          v Crystal Palace

 Chelsea          v Man City

 Everton          v Southampton

 Leicester City   v West Ham

 Man United       v Aston Villa

 Newcastle v Swansea City

 Norwich City     v Sunderland

 Stoke City       v Tottenham

 West Brom v Watford





Jumamosi, Aprili 23, 2016

AFC Bournemouth   v Chelsea

 Aston Villa      v Southampton

 Crystal Palace   v Everton

 Leicester City   v Swansea City

 Liverpool        v Newcastle United

 Man City         v Stoke City

 Norwich City     v Watford

 Sunderland       v Arsenal

 Tottenham v West Brom

 West Ham   v Manch United





Jumamosi, Aprili 30, 2016

Arsenal           v Norwich City

Chelsea           v Tottenham

Everton           v AFC Bournemouth

Man United v Leicester City

Newcastle   v Crystal Palace

Southampton       v Man City

Stoke City        v Sunderland

Swansea City      v Liverpool

Watford           v Aston Villa

West Brom   v West Ham





Jumamosi, Mei 7, 2016

AFC Bournemouth   v West Brom

Aston Villa       v Newcastle

Crystal Palace    v Stoke City

Leicester City    v Everton

Liverpool         v Watford

Man City          v Arsenal

Norwich City      v Man United

Sunderland v Chelsea

Tottenham   v Southampton

West Ham    v Swansea City

 

Jumapili, Mei 15, 2016

Arsenal           v Aston Villa

Chelsea           v Leicester City

Everton           v Norwich City

Man United v AFC Bournemouth

Newcastle   v Tottenham

Southampton       v Crystal Palace

Stoke City        v West Ham

Swansea City      v Man City

Watford           v Sunderland

West Brom   v Liverpool