STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, June 21, 2015

Argentina yaifumua Jamaica kidude, yatinga robo fainali

Argentina
Safi sana kijana, Higuain (kulia) akipongezwa na Messi na Di Maria baada ya kufunga bao la mapema

Argentina 4
Messi akikikusanya kijiji kama kawaida yake
Argentina 5
Gonzalo Higuain akishangilia bao lililoivusha Argentina robo fainali za Copa America
BAO la dakika 11 ya Gonzalo Higuain kutokana na pazi murua ya Angel di Maria imeiwezesha Argentina kusonga mbele katika kundi lake kwenye michuano ya Copa America, huku Chile ikiitafanua Bolivia 5-0 na Uruguay na Paraguay wakitoshana nguvu katika mechi nyingine.
Argentina kwa ushindi huo imeongoza kundi lake la B kwa kufikisha pointi saba mbili zaidi ya Paraguay na zote zimesonga mbele hatua ya robo fainali.
Bolivia licha ya kupigwa mkono na Chile, lakini timu hizo mbili zimefuzu hatua ya robo fainali kutoka kundi A, huku kundi C likitarajiwa kutua washindi wao leo sambamba na timu mbili zitakazoungana na zilizofuzu moja kwa moja. Timu tatu za Uruguay, Venezuela na Ecuador zinawania nafasi ya Best Looser katika michuano hiyo.

No comments:

Post a Comment