STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, February 5, 2015

Real Madrid waitumia salamu Atletico Madrid La Liga

The Colombia playmaker wheels away in celebration after scoring a delightful opener for Real during Wednesday's encounter
James Bond akishangilia bao la kwanza la Madrid
Real doubled their lead on 36 minutes when substitute Jese (left) finished from close-range against Sevilla
Jesse akifunga bao la pili la wenyeji Santiago Bernabeu
Gareth Bale (left) was a constant menace to the Sevilla defence throughout the match at the Santiago Bernabeu
Gareth Bale akiwajibika uwanjani
VINARA wa Ligi Kuu ya Hispania, Real Madrid imetuma salamu kwa wapinzani wao wa jadi Atletico Madrid watakaovaana nao siku ya Jumamosi baada ya kuicharaza Sevilla kwa mabao 2-1 katika mfululizo wa ligi hiyo maarufu kama La Liga.
Mabao ya  James 'Bond' Rodriguez la dakika ya 12 na lingine la Jesse dakika ya 36 yalitosha kuwapa ushindi muhimu vijana wa Santiago Bernabeu kwenye uwanja wao wa nyumbani kabla ya kuwafuata Atletico katika mechi ya kisasi.
Wageni walijipatia bao la kufutia machozi dakika 10 kabla ya kumalizika kwa pambano hilo kupitia kwa Iago Aspas.
Ushindi huo umeifanya Real Madrid ambayo iliwakosa nyota wake kadhaa kiwamo nahodha Cristiano Ronaldo anayetumikia adhabu.ya kadi nyeekundu, kufikisha pointi 54 na kujikita kileleni huku nyuma yao wakiwa ni Barcelona wenye pointi 50, na saba zaidi ya wapinzani wao wa Jumamosi walipo nafasi ya tatu.


Asamoah Gyan aleta hofu Ghana wakiwavaa wenyeji Afcon

http://megasignals.net/wp-content/uploads/2014/06/Asamoah-Gyan-Ghana-World-Cup-2014-Wallpaper.jpg
Nahodha wa Ghana, Asamoah Gyan
MALABO, Guinea ya Ikweta
MSHAMBULIAJI wa timu ya taifa ya Ghana, Christian Atsu anaweza kuwa nguzo muhimu katika mechi ya nusu-fainali ya Mataifa ya Afrika (AFCON) dhidi ya Guinea ya Ikweta leo kama Asamoah Gyan atashindwa kucheza kutokana na majeraha, mchezaji mwenzake Jonathan Mensah alisema juzi.
"Sote tunafahamu nini Atsu anaweza kukifanya, inasaidia sana kuwa na wachezaji ambao wanaweza kuleta tofauti mchezoni," beki Mensah aliwaambia waandishi wa habari.
"Ana nafasi muhimu katika timu, anafanya kile anachotaka kufanya na anaongezeka ubora siku hadi siku. Tuna furaha yuko katika makali yake hivi sasa na ataisaidia timu."
Atsu (23), alifunga goli kali wakati kikosi cha Avram Grant kilipotinga katika hatua ya nusu-fainali kwa ushindi wa 3-0 dhidi ya Guinea mjini Malabo Jumapili lakini ni lazima wajiandae kuwakabili wenyeji leo bila ya nahodha wao mwenye ushawishi kikosini Gyan.
Baada ya kupona malaria na kufunga goli la dakika za lalasalama la ushindi wa Ghana katika mechi yao ya pili ya hatua ya makundi dhidi ya Algeria, Gyan aliumizwa kwa teke la kurukiwa tumboni kutoka kwa kipa wa Guinea, Naby Yattara.
Wakati Gyan akiwa shakani katika mechi ya nusu-fainali leo, Mensah anaamini Atsu, ambaye yuko kwa mkopo Everton akitokea katika klabu yake ya Chelsea, anaweza kufunika kutong'aa kwake kwenye ngazi ya klabu na kutamba kwenye timu ya taifa.
"Hisia inakuwa ni tofauti anapoichezea Everton. Tunamuachia anafanye kile anachoweza vyema, ni timu tofauti kabisa," alisema Mensah.
"Timu hii ya Ghana haina mfungaji maalum wa magoli, sote tunafunga tunapopewa nafasi, hilo ni jambo ambalo linalotusaidia sana."
Huku akisifu kuongezeka ubora kwa Atsu, Mensah pia alielezea umuhimu wa Gyan kwenye kikosi cha Black Stars.
"Ndani na nje ya uwanja Gyan ni kiongozi, yeye ni nahodha wa timu na wakati wowote anaokuwapo uwanjani huthibitisha yeye ni kiongozi wa kweli," alisema.
"Yeye ni mshambuliaji bora barani Afrika hivyo wakati wowote anaokuwapo uwanjani ni kama jumlisha mbili kwenye timu.
"Anajisikia maumivu. Amefadhaika sana, kwa sababu ndiyo kwanza alikuwa ameanza kurejea katika makali na kisha majeraha haya yamekuja. Tumezungumza na morali yake iko juu, lakini wakati huohuo hayuko fiti kwa asilimia 100.
"Yeye ni bonge la kiongozi na hata pale asipofunga, au kupata fursa ya kufunga, wakati wote hufanya kazi kwa ajili ya timu. Yeye ndiye kinara wetu na tuna furaha kuwa naye," aliongeza.
Iwapo Ghana wanaing'oa Guinea ya Ikweta na kukutana na Ivory Coast watarejesha kumbukumbu ya Fainali za mwaka 1992 zilizozikutanisha timu hizi na Ivory Coast kushinda kwa mikwaju ya penati.

JAHAZI LA BORUSSIA DORTMUND LAZIDI KUZAMA UJERUMANI

Borussia Dortmund keeper Roman Weidenfeller
Wachezaji wa Dortmund hawaamini kama wamezama teena nyumbani
Augsburg's Raul Bobadilla
Bobadilla akimtungua kipa wa Dortmund, Roman Weidenfeller
Borussia Dortmund coach Jurgen Klopp (centre)
Kocha Jurgen Kloop akiwa na wachezaji wake vichwa chini
JAHAZI la mabingwa wa zamani wa Ujerumani na wana fainali wa Ligi ya Mabingwa Ulaya za mwaka juzi, Borussia Dortmund limezidi kutota baada ya usiku wa jana kugongwa nyumbani bao 1-0 na Augsburg na kuzidi kujichimbia mkiani mwa Ligi Kuu ya Ujerumani, Bundesliga.
Bao pekee lililofungwa na Raul Bobadilla dakika tano baada ya kuanza kwa kipindi cha pili lilitosha kuwaacha vijana wa kocha Jurgen Kloop wakisalia mkiani wakiwa na pointi 16 tu baada ya kucheza mechi 19 huku wapinzani wao wakichupa hadi nafasi ya nne katika msimamo wakiwa na pointi 33.
Katika mechi 19 ilizocheza Dortmund imeshinda mechi nne tu na kuambulia sare nne huku ikipoteza mechi 11 na kuwa na wakati mgumu katika kupigana kusalia katika ligi hiyo, matoke ambayo ni  mabaya kwa timu hiyo kuwahi kutokea katika misimu ya karibuni.
Kloop ameiongoza timu yake katika mechi nane na kupata ushindi mmoja tu, kitu ambacho kimeacha maswali mengi kwa mashabiki wa timu hiyo iliyotetemesha ligi ya Ujerumani na Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa ujumla, japo ipo kwenye mechi za mtoano zitakazoanza wiki mbili zijazo ambapo Wajerumani hao watavaana na Juventus.
Katika mechi nyingine za ligi hiyo zilizochezwa jana Hoffenheim ilikubali kichapo nyumbani dhidi ya WErder Bremen kwa kulazwa mabao 2-1,  Hertha Berlin nayo ikalala 1-0 nyumbani mbele ya Bayer Leverkusen, huku FC Koln  na Stuttgart wakitoshana nguvu kwa suluhu isiyo na mabao na Paderborn ikanyukwa mabao 3-0 nyumbani na Hamburger SV.

Liverpool wafanya kweli Kombe la FA,

The Brazilian midfielder points to the sky after his goal put Liverpool into the FA Cup fifth round
Coutinho akimshukuru Mungu kwa kuifungia Liverpool bao lililowavusha Raundi ya Tano ya Kombe la FA usiku wa jana
Alberto Moreno (left) jumps for joy with Coutinho as Liverpool secure an FA Cup fifth round tie against Cyrstal Palace
Coutinho akipongezwa na Moreno
Clough, making just his third Bolton start, is tripped by Skrtel as referee Roger East looks on in the distance
Martin Skrtel akimchezea dogo wa Bolton rafu iliyozaa bao pekee la wenyeji wa mchezo huo wa marudiano
Eidur Gudjohnsen (left) puts Bolton into a 1-0 lead against Liverpool with a penalty in the 59th minute 
Eidur Gudjohnsen akifunga penati ya Bolton
KLABU ya Liverpool ilitoka nyuma dhidi ya Bolton Wanderers na kufanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 na kutinga Raundi ya Tano ya Kombe la FA.
Mechi hiyo ya marudiano ilichezwa usiku wa jana kwenye uwanja wa Macron nyumbani kwa Bolton ambao waliwashtua wageni wao kwa kutangulia kupata bao la kuongoza kupitia kwa EidurGudjohnsen katika dakika ya 59 baada ya dakika 45 za awali kumalizika timu hizi zikiwa nguvu sawa ya kutofungana.
Bao hilo lilifungwa kwa mkwaju wa penati baada ya Martin Skrtel kumchezea rafu Zach Clough, hata hivyo dakika nne kabla ya kumalizika kwa pambano hilo na huku wenyeji wakiamini wameungana na timu nyingine zilizowatoa nishai vigogo katika michuano hiyo, Raheem Starling aliisawazishia Liverpool bao hilo.
Sekunde chache kabla ya kumalizika kwa pambano hilo pengine wenyeji ambao walimpoteza mmchezaji wao mmoja baada ya kuonyesha kadi ya pili ya njano iliyofuatana na nyekundu, wakiamini wataenda kwenye muda wa ziada, Phillipe Coutinho aliiandikia bao la ushindi Liverpool na kuwafanya kusonga mbele na kukabiliana sasa na Crystal Palace Siku ya Wapendanao uwanja wa ugenini.
Kabla ya mechi hiyo ya FA, Liverpool  itakuwa na kibarua wikiendi hii kuvaana na wapinzani wao wa jadi Everton uwanja wa ugenini Goodson Park kisha kuwakaribisha Vijogoo wenzao wa London, Tottenham Hotspur uwnaja wa Anfield Jumanne ijayo.

Yanga yawabutua Coastal Union kwao, mkwakwani kimyaaaaa!

Cannavaro 6
Wachezaji wa Yanga wakimpongeza nahodha wao Cannavaro kwa kufunga bao pekee la Yanga dhidi ya Coastal


Cannavaro akishangilia bao lake
Match Report: Coastal Union 0 – 1 Yanga, Yanga yakwea kileleni
Oyooooooooo! Cannavaro akishangilia bao lake
BAO pekee la Nahodha Nadir Haroub 'Cannavaro' lilitosha kuwapa ushindi Yanga na kuwapeleka hadi kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara baada ya kuizima Coastal Union kwenye uwanja wao wa nyumbani wa CCM Mkwakwani Tanga.
Yanga walipata ushindi huo katika mechi iliyojaa ufundi na ubabe ya kiporo kilicholeta mvuto wa aina yake kutokana na tambo na majigambo ya viongozi wa pande mbili kwamba kabla ya kuchezwa kwake.
Cannavaro amekuwa mhimili mkubwa wa Yanga kwa uhamasishaji wake, kujituma na kufunga mabao muhimu pale washambuliaji wa timu hiyo wanapozembea, aliweka kimiani bao hilo dakika ya 11 kwa kichwa akiunganisha mpira wa kurushwa wa beki Mbuyu Twite ulioparazwa na Simon Msuva na kuipa Yanga pointi tatu zilizowafanya wafikishe 22, moja zaidi ya mabingwa watetezi ambao hata hivyo wana mchezo mmoja pungufu zaidi ya Yanga.
Licha ya Coastal Unio kucharuka kusaka bao la kusawazisha walienda mapumziko wakiwa nyuma na hata katika kipindi cha pili hali ilikuw ahivyo hivyo, huku Yanga ikimpoteza mshambuliaji wake Amissi Tambwe aliyeumizwa wakati wa mchezo kipindi cha kwanza na kushindwa kurudi uwanjani.
Kwa kipigo hicho Simba ambayo Jumamosi hii wana mtihani mwingine dhidi ya Simba, wamesaliwa na pointi zao 17 baada ya mechi 13 na kusalia kwenye nafasi ya saba mbele ya Simba wenye pointi 16 baada ya mechi 12.
Ligi hiyo itaendelea tena wikiendi hii kw amichezo kadhaa huku pambano la Yanga na Mtibwa Sugar likiwa limeahirishwa ili kutoa nafasi kwa wawakilishi wa Kombe la Shirikisho kujiandaa vema kabla ya kuvaana na BDF XI ya Botswana wiki ijayo kwenye uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Tembo wa Afrika watangulia fainali, waigonga Kongo 3-1


afcon
Gervinho akijaribu kumtungua kipa wa DRC, Kidiaba
Wachezaji wa Tembo wa Ivory Coast wakishangilia ushindi wao wa kutinga fainali za Afcon 2015
TEMBO wa Ivory Coast, wamedhihirisha dhamira yao ya kutaka ubingwa wa Kombe la Mataifa Afrika baada ya kugawa dozi nene kwa Chui wa DR Congo kwa kuwalaza mabao 3-1 katika mechi ya Nusu Fainali na kutinga Fainali za michuano hiyo itakayochezwa Jumapili.
Kikosi cha Ivory Coast kikiongozwa na nahodha wake, Yaya Toure kilifanikiwa kutinga hatua hiyo ya fainali kwa kulipa kiasi ilichowahi kupewa na wapinzani wao wakati wa mechi za makundi za kuwania kwenda Guinea ya Ikweta kwa kulazwa nyumbani kwao mabao 4-3.
Wafungaji wa mabao ya wanafainali wa mwaka 2012 walikuwa Yaya Toure katika dakika ya 21, Gervinho aliyeongeza la pili dakika ya 41 na  Kanon aliyemaliza udhia katika kipindi cha pili kwenye dakika ya 68.
Bao la kufutia machozi la Congo waliowang'oa watani zao wa jadi Congo-Brazzaville kwenye mechi ya robo fainali lilifungwa kwa mkwaju wa penati na Mbokani dakika ya 24.

Kwa matokeo hayo Ivory Coast wanasubiri mshindi wa mechi ya leo kati ya mabingwa mara nne Ghana dhidi ya Guinea ya Ikweta ili kuumana nao kwenye fainali ya Jumapili itakayoamua bingwa mpya wa Afrika baada ya taji kiutokuwa na mwenyewe kufuatia Nigeria waliokuwa mabingwa kukwa kwenda Afcon 2015.
DR Congo wenyewe watakuwa wakisubiri kujua wataumana na timu ipi itakayopoteza mchezo wa leo ili kumenyana naye katika mechi ya kusaka mshindi wa tatu itakayochezwa keshokutwa Februari 7.