STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, February 5, 2015

JAHAZI LA BORUSSIA DORTMUND LAZIDI KUZAMA UJERUMANI

Borussia Dortmund keeper Roman Weidenfeller
Wachezaji wa Dortmund hawaamini kama wamezama teena nyumbani
Augsburg's Raul Bobadilla
Bobadilla akimtungua kipa wa Dortmund, Roman Weidenfeller
Borussia Dortmund coach Jurgen Klopp (centre)
Kocha Jurgen Kloop akiwa na wachezaji wake vichwa chini
JAHAZI la mabingwa wa zamani wa Ujerumani na wana fainali wa Ligi ya Mabingwa Ulaya za mwaka juzi, Borussia Dortmund limezidi kutota baada ya usiku wa jana kugongwa nyumbani bao 1-0 na Augsburg na kuzidi kujichimbia mkiani mwa Ligi Kuu ya Ujerumani, Bundesliga.
Bao pekee lililofungwa na Raul Bobadilla dakika tano baada ya kuanza kwa kipindi cha pili lilitosha kuwaacha vijana wa kocha Jurgen Kloop wakisalia mkiani wakiwa na pointi 16 tu baada ya kucheza mechi 19 huku wapinzani wao wakichupa hadi nafasi ya nne katika msimamo wakiwa na pointi 33.
Katika mechi 19 ilizocheza Dortmund imeshinda mechi nne tu na kuambulia sare nne huku ikipoteza mechi 11 na kuwa na wakati mgumu katika kupigana kusalia katika ligi hiyo, matoke ambayo ni  mabaya kwa timu hiyo kuwahi kutokea katika misimu ya karibuni.
Kloop ameiongoza timu yake katika mechi nane na kupata ushindi mmoja tu, kitu ambacho kimeacha maswali mengi kwa mashabiki wa timu hiyo iliyotetemesha ligi ya Ujerumani na Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa ujumla, japo ipo kwenye mechi za mtoano zitakazoanza wiki mbili zijazo ambapo Wajerumani hao watavaana na Juventus.
Katika mechi nyingine za ligi hiyo zilizochezwa jana Hoffenheim ilikubali kichapo nyumbani dhidi ya WErder Bremen kwa kulazwa mabao 2-1,  Hertha Berlin nayo ikalala 1-0 nyumbani mbele ya Bayer Leverkusen, huku FC Koln  na Stuttgart wakitoshana nguvu kwa suluhu isiyo na mabao na Paderborn ikanyukwa mabao 3-0 nyumbani na Hamburger SV.

No comments:

Post a Comment