STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, February 5, 2015

Liverpool wafanya kweli Kombe la FA,

The Brazilian midfielder points to the sky after his goal put Liverpool into the FA Cup fifth round
Coutinho akimshukuru Mungu kwa kuifungia Liverpool bao lililowavusha Raundi ya Tano ya Kombe la FA usiku wa jana
Alberto Moreno (left) jumps for joy with Coutinho as Liverpool secure an FA Cup fifth round tie against Cyrstal Palace
Coutinho akipongezwa na Moreno
Clough, making just his third Bolton start, is tripped by Skrtel as referee Roger East looks on in the distance
Martin Skrtel akimchezea dogo wa Bolton rafu iliyozaa bao pekee la wenyeji wa mchezo huo wa marudiano
Eidur Gudjohnsen (left) puts Bolton into a 1-0 lead against Liverpool with a penalty in the 59th minute 
Eidur Gudjohnsen akifunga penati ya Bolton
KLABU ya Liverpool ilitoka nyuma dhidi ya Bolton Wanderers na kufanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 na kutinga Raundi ya Tano ya Kombe la FA.
Mechi hiyo ya marudiano ilichezwa usiku wa jana kwenye uwanja wa Macron nyumbani kwa Bolton ambao waliwashtua wageni wao kwa kutangulia kupata bao la kuongoza kupitia kwa EidurGudjohnsen katika dakika ya 59 baada ya dakika 45 za awali kumalizika timu hizi zikiwa nguvu sawa ya kutofungana.
Bao hilo lilifungwa kwa mkwaju wa penati baada ya Martin Skrtel kumchezea rafu Zach Clough, hata hivyo dakika nne kabla ya kumalizika kwa pambano hilo na huku wenyeji wakiamini wameungana na timu nyingine zilizowatoa nishai vigogo katika michuano hiyo, Raheem Starling aliisawazishia Liverpool bao hilo.
Sekunde chache kabla ya kumalizika kwa pambano hilo pengine wenyeji ambao walimpoteza mmchezaji wao mmoja baada ya kuonyesha kadi ya pili ya njano iliyofuatana na nyekundu, wakiamini wataenda kwenye muda wa ziada, Phillipe Coutinho aliiandikia bao la ushindi Liverpool na kuwafanya kusonga mbele na kukabiliana sasa na Crystal Palace Siku ya Wapendanao uwanja wa ugenini.
Kabla ya mechi hiyo ya FA, Liverpool  itakuwa na kibarua wikiendi hii kuvaana na wapinzani wao wa jadi Everton uwanja wa ugenini Goodson Park kisha kuwakaribisha Vijogoo wenzao wa London, Tottenham Hotspur uwnaja wa Anfield Jumanne ijayo.

No comments:

Post a Comment