STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, May 4, 2013

Bale aipa Spur ushindi wa jioni EPL

Gareth Bale akiwajibika dimbani
BAO la dakika ya 88 lililofungwa na Mchezaji Bora wa Mwaka England, Gareth Bale limeiwezesha Tottenham Hotspur kupata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Southampton katika pambano la Ligi Kuu ya England na kuiengua Arsena iliyopo dimbani kwa sasa ikiumana na QPR katika nafasi ya nne.
Hata hivyo huenda Tottenham inayowania kumaliza kwenye Nne Bora na kupata nafasi ya kushiriki Ligi ya Mabingwa Ulaya mwakani itakali nafasi hiyo kwa muda kwani mpaka sasa Arsenal iliyopo ugenini inaongoza kwa bao 1-0.
Katika mechi nyingine zilizochezwa jioni na kumalizika waliokuwa mabingwa watetezi wa ligi hiyo, Manchester City imelazimishwa suluhu ugenini na Swansea City, huku Reading iliyokwisha kushuka daraja ikimaliza hasira kwa Fulham kwa kuikandika nyumbani kwao mabao 4-2.
Nao vijana wa Paul Lambert , Aston Villa waliendelea kupigana kuepuka kushuka daraja kwa kupata ushindi ugenini wa mabao 2-1 dhidi ya wenyeji wao Norwich City, huku West Ham ikiwa nyumbani ililazimishwa suluhu na Newcastle United na Wigan Athletic ikiitambia West Bromwich Albion ikiwa kwao kwa mabao 3-2.
Kitimtim cha ligi hiyo kinatarajiwa kuendelea tena kesho kwa mechi inasubiriwa kwa hamu kati ya Mabingwa wa ligi hiyo, Manchester United itawakaribisha Chelsea uwanja wa Old Traffod huku wapinzani wa jadi Liverpool na Everton zitapepetana kwenye uwanja wa Anfield.

Hull City yarejea Ligi Kuu England



KLABU ya Hull City imefanikiwa kuungana na Cardiff City kupanda Ligi Kuu ya England msimu ujao baada ya jioni hii kutoshana nguvu katika pambano la kufungia msimu wa Ligi Daraja la Kwanza England.
Hull City ikiwa kwenye dimba lake la nyumbani, Kingston Communications  vijana hao wa kocha Steve Bruce walifungana mabao 2-2 na Cardiff City iliyokuja kusawazisha bao dakika za lala salama kwa mkwaju wa penati.
Sare hiyo imeifanya Hull City kufikisha jumla ya pointi 79 na kung'ang'ania nafasi ya pili nyuma ya Cardiff iliyokuw ameshatawaza mabingwa wa ligi hiyo wiki iliyopita ilimaliza msimu ikiwa na pointi 83.
Timu hizo mbili zimeziachia timu za Watford, Leichester City, Crystal Palace na Brighton & Have Albion kuchuana zenyewe kuwania nafasi moja ya kuungana nao kwenye Ligi Kuu ya England msimu ujao.
Watford imemaliza ligi leo kwa kichapo, lakini ikisalia nafasi ya tatu ikiwa na pointi 77 ambapo kama ingeshinda ingeweza kuipiku Hull City, Brighton wamekamata nafasi ya nne klwa kufikisha pointi 75 baada ya leo kuibuka na ushindi, kisha kufuatiwa na Crystal Palace iliyokusanya pointi 72 baada ya jioni hii pia kupata ushindi kama ilivyokuwa kwa Leichester City iliyoshinda na kushika nafasi ya sita kwa pointi zake 68 sawa na timu ya Bolton Wanderers iliyolazimisha sare na kushuka nafasi nafasi ya sita kwa tofauti na uwiano wa mabao ya kufunga na kufungwa.
Tayari timu mbili zilizoshuka daraja kutoka Ligi Kuu ya England zimeshafahamika ambazo ni Reading na Queen Park Rangers, huku timu ya mwisho ikiwa inasubiriwa wakati ligi hiyo ikielekea kufikia ukingoni.

Sababu za Azam kuing'oa As Far Rabat leo ni hizi

Mkali John Bocco 'Adebayor'

Mnafanya hivi! Kocha John Stewart Hall akiwalekeza wachezaji wake

Hakutuja kuuza sura kazi tu! Vifaa vya Azam vikijifua Rabat

Na Patrick Kahemela
Azam FC leo inatupa karata yake ya sita kwenye michuano ya CAF Confederations Cup huku ikiwa na rekodi ya kucheza michezo mitano tayari pasi na kupoteza hata mmoja. ikumbukwe kuwa tangia kuumbwa kwa taifa la Tanzania hakuna klabu ya soka iliyowahi kucheza zaidi ya michezo mitano pasi na kupoteza hata mmoja. Azam FC ikishinda au kutoka sare leo itakuwa imefikia rekodi hiyo huku ikiwa inawakilisha nchi kwa mara ya kwanza.

Katika makala mbili za nyuma tulijadili sababu sita kwa nini Azam FC leo ina nafasi ya kushinda mchezo huu, katika mjadala huo kipengele pekee ambacho hatukukimalizia ni wasifu wa washambuliaji wetu.

Hapa tutawaletea dondoo kuhusu washambuliaji wanaotarajia kuongoza safu ya ushambuliaji ya Azam FC hii leo.

Kipre Tchetche, Khamis Mcha Viali na Braian Umony ndiyo washambuliaji wa pembeni ambao mwalimu Stewart Hall atalazimika kuchagua wawili ili kuanza kesho huku John Bocco akicheza katikati hiyo kesho… lakini Azam FC inao viungo wengine wa pembeni na washambuliaji ambao imesafiri nao kama Uhuru Selemani, Abdallah Seif karihe na Gaudence Mwaikimba.

Kwa jinsi timu inavyocheza mazoezini, ni wazi kuwa John Bocco atasimama katikati akipewa sapoti na Kipre Tchetche na Brian Umony. Watatu hawa ni wachezaji wa kiwango cha juu sana kwa sasa. Umony ni mchezajo bora wa CECAFA Challenge Cup. Bocco ni mfungaji bora wa Ligi Kuu Tanzania Msimu uliopita na CECAFA Challenge Cup huku Kipre Tchetche akiwa mfungaji bora wa msimu huu ligi kuu Tanzania.

Unapokuwa na wachezaji wenye sifa hizi huku kwenye benchi ukiwa na akiba ya watu kama Uhuru Selemani, Abdallah Seif karihe, Khamis Mcha Viali wa Unguja na Gaudence Mwaikimba unapata nini zaidi ya ushindi?

Ni dhahiri kuwa unapokuwa na kikosi kama hiki lazima utajiamini.



Kocha Stewart Hall anaweza kuwapanga khamis Mcha na Kipre Tchetche pembeni mwa Bocco… ama anaweza kuwaanzisha Brian Umony na Kipre Tchetche pembeni mwa Bocco machaguo hayo mawili yatampa aina tofauti za kushambulia na kulinda goli.

Mcha Khamis Viali yeye ni mzuri sana kwenye kukaba na aina yake ya kushambulia ni ya kipekee kabisa kiasi kwamba ni vigumu kumdhibiti. Mcha hucheza na nafasi, hapotezi muda na mpira na anapoingia kwenye eneo la kufunga basi hupasia mpira kambani kwa utulivu.

Ukimuangalia alivyo usoni huwezi kudhani kuwa anaweza kuwa na madhara lakini awapo uwanjani ni mchezaji aliyekamilika. Ana balance, anajua kumiliki mpira, miguu yake ina macho na anajua kusoma ramani ya namna mchezo unavyokwenda na jinsi gani aifanyie kazi.

Ukiachana na Mcha, Kipre Tchetche yeye kwa sasa ni “Deadly Killer”… Kipre anapokuwa na mpira wapinzani wanapata homa, chenga zake anapowatoroka mabeki huwafanya makae chini na anapofika kwenye eneo la adui huwa hana masihara. Kutamba kote kwa Azam FC kunatokana na kuwana na nyota huyu wa Ivory Coast ambaye ana miaka miwili sasa tangia atue Azam FC.

Brian Umony ambaye alitamba na Uganda Cranes kama mshambuliaji wa kati sasa amehamishiwa pembeni na spidi yake anaposhambulia na akili nyingi alizonazo anapoichambua kama karanga ngome ya maadui ndiyo silaha kuu inayotegemewa na Azam FC hapo kesho.

Brian ambaye amekuwa akisumbuliwa na majeruhi kwa muda mrefu kwa sasa yupo fiti 100% na inshallah kama atapata nafasi ya kuanza tutarajie makubwa toka kwake.

Kwa mashabiki wa ukweli wa Azam FC huhitaji kumuelezea John Bocco, Bocco anapokuwa majeruhi basi Azam FC hupooza na kwa sasa nahodha huyu anaonekana kuwa si kiongozi wa wachezaji wenzake tuu kama nahodha bali pia roho ya klabu.

John Bocco ana nguvu sana na anajua kucheza kama screen man akiwafanya wapinzani wamuwekee ulinzi wa watu watutu hivyo kutoa mwanya kwa wenzake kucheza. Unaweza ukadhani Bocco hachezi vizuri anapotimiza majukumu yake… lakini matokeo ya mwisho ya ushindi ndiyo yatakayokupa majibu. Timu nyingi huingia kwenye mtego wa John Bocco wa kucheza naye kidali poo na kufukuzana bila mpira huku Kipre Tcheche na wenzake wakifanya mambo na kuipa Azam FC ushindi. Ngoja tuone nini kitatokea.

Timu itakayopangwa leo ni kama ifuatavyo
Mwadini Ally Mwadini (GK)
Himid Mao Mkami (RB)
Waziri Salum Omar (LB)
David John Mwantika (CB)
Jockins Atudo (CB)
Kipre Bolou Michael (MF)
Salum Abubakar (MF)
Humphrey Mieno(MF)
Kipre Tchetche Herman (RW)
John Bocco (STR)
Brian Umony (LW)

Ajali yapoteza uhai wa watu 7 papo hapo, 44 wakimbizwa hospitalini

BASI la Taqwa linalofanya safari zake kati ya Tanzania na Zimbabwe, limepata ajali na kusababisha vifo vya watu saba huku wengine 44 wakijeruhiwa.
Habari zilizopatika hivi karibuni zinasema kuwa ajali hiyo ilitokea katika eneo la kijiji cha Nyololo wilayani Mufindi mkoani Mufindi wakati basi hilo likitokea Dar kuelekea Zimbabwe.
Inaelezwa ajali hiyo ilihusisha magari matatu ambayo ni basi la Taqwa aina ya Nissan Diesel lenye namba za usajili T 273 CBR (Sniper), lori la mizigo aina ya Scania, mali ya Kampuni ya Nyati Transport Ltd lililokuwa limebeba shehena ya viazi pamoja na lori la mizigo lenye namba T 104 BZZ aina ya Scania, mali ya kampuni ya Sogea Satom.
majeruhi wa ajali hiyo inaelezwa wamekimbizwa hpsitalini kwa matitabu, ambapo Dk Bakuza wa hospitali ya Mufindi aliwataja watu waliofariki katika ajali hiyo na miili yao kuhifadhiwa hapo ni; Abrahaman Abduli (32) ambaye ni dereva wa basi la Taqwa, Nassoro Rashid (27) ambaye ni kondakta wa basi hilo, Omari Muhusin, Alli Mussa, Joseph Charles, Emmi Kafute na maiti moja haijafahamika jina lake.
MICHARAZO inawapa pole waliofikwa na msiba huo na pia kuwaombea tahfif majeruhi wote waweze kupona, kadhalika tukiwataka walioguswa na mkasa huu kuwa na moyo wa uvumilivu na subira kwa kukumbuka kuwa Kazi ya MUNGU haina makosa.
MUNGU aziweke roho za marehemu mahali Pema Ameen

Silaha za Azam za kuiua FAR Rabat hizi hapa

 
 Vialli (kati) na Sure Boy wakijifua kuwakabilia AS FAR Rabat
Kikosi cha Azam kinachotarajiwa kuwatoa kimasomaso Watanzania leo nchini Morocco.
WAWAKILISHI wa Tanzania katika michuano ya kimataifa, Azam jioni hii wanatarajiwa kushuka dimbani nchini Morocco kupepetana na wenyeji wao, AS FAR Rabat katika mechi ya marudiano ya Kombe la Shirikisho Afrika.
Azam ambayo ipo nchini humo karibu wiki nzima sasa katika mbinu za kuzoea mazingira ya kuwakabili wapinzani wao, inahitaji sare ya aina yoyote ya magoli kuweza kufuzu hatua ya 16 Bora.
Katika pambano la kwanza lililochezwa nchini Tanzania wiki mbili zilizopita, Azam walilazimishwa suluhu na maafande hao wa jeshi la Morocco licha ya kosakosa za hapa na pale katika mchezo huo.
Azam ina matumaini makubwa ya kuibuka na ushindi ugenini katika pambano hilo kwa kile kinachoelezwa ari waliyonayo wachezaji na maandalizi waliyoyafanya mpaka sasa.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka Morocco mechi hiyo itachezwa kuanzia saa 11:00 jioni kwa saa za Morocco sawa na saa 1 usiku kwa hapa Tanzania na tayari silaha za 'maangamizi' za Azam zimeshaanikwa tayari ya kufanya 'maafa' ugenini.
Kikosi kitakachoanza pambano hilo ambalo litatangazwa na kituo cha runinga cha Clouds na RFA Masafa ya Kati na Kiss FM ni kama kifuatavyo;
1. Mwadini 
2. Himidi Mao
3. Waziri Seif
4. David Mwantika
5. Atudo
6. Bolou
7. Umony
8. Salum 'sure boy'
9. Bocco (C)
10. Mieno
11. Kipre
Akiba
Aishi
Ibrahim Mwaipopo
Gaudence Mwaikimba
Abdi Kassim 'Babi'
Mcha Khamis 'Vialli'
Jabir Aziz Stima
Luckson Kakolaki
 
Mungu Ibariki Azam Mungu Ibariki Tanzania
Mungu