STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, February 6, 2014

Kanembwa watatakiwa kuwasilisha utetezi TFF

WACHEZAJI tisa wa Kanembwa JKT pamoja na timu yao wanaolalamikiwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kwa kumpiga mwamuzi Peter Mujaya wanatakiwa kujitetea mbele ya Kamati ya Nidhamu itakayokutana Jumapili (Februari 9 mwaka huu).

Utetezi huo unaweza kuwa wa mdomo kwa walalamikiwa kufika wenyewe mbele ya kamati itakayokutana saa 4 kamili asubuhi au kuuwasilisha kwa njia ya maandishi.

Kamati ilikutana jana Jumatano (Februari 5 mwaka huu) kusikiliza malalamiko dhidi ya wachezaji hao na timu yao kwa tukio hilo lililotokea Novemba 2 mwaka jana kwenye mechi ya Ligi Daraja la Kwanza (FDL) dhidi ya Stand United FC iliyochezwa Uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga.

Wachezaji hao ni Abdallah Mgonja, Bariki Abdul, Philipo Ndonde, Mbeke Mbeke, Mkuba Clement, Mrisho Mussa, Nteze Raymond, Ntilakigwa Hussein na Uhuru Mwambungu. Mlalamikiwa mwingine ambaye naye anatakiwa kujitetea ni timu ya Kanembwa JKT.

Ikiwa chini ya Mwenyekiti wake Tarimba Abbas, Kamati hiyo baada ya kusikiliza malalamiko dhidi ya wahusika na kupokea ushahidi wa aina mbalimbali kutoka kwa mlalamikaji imesema ili iweze kutenda haki katika shauri hilo ni lazima walalamikiwa wapate fursa ya kusikilizwa.

Katika hatua nyingine, Kamati hiyo iliyokutana kwa mara ya kwanza tangu ilipoundwa imesema imesikitishwa na vitendo vya fujo ndani ya mpira wa miguu, na kuwataka watu wasijihusishe na aina yoyote ya fujo

Simanzi! Ajali nyingine tena Singida

WASOMAJI WETU TUNAOMBA RADHI KAMA UTAKWAZIKA NA PICHA ZIFUATAZO.
DSC06423
Mtoto mmoja aliyelalaliwa na kusababisha kifo chake na basi la Zuberi T.119 AZZ lilokuwa likitokea Mwanza kuelekea jijini Dar-es-salaam na kupinduka katika eneo la kijiji cha Tumaini kata ya Issuna wilaya ya Ikungi wakati likimkwepa bibi aliyekuwa akikatisha barabara.(Picha na Nathaniel Limu).
DSC06430
Mmoja wa majeruhi akiwa amelazwa katika Hosptali ya Mkoa ya Singida.
DSC06438
Mmoja wa majeruhi akiongea na waandishi wa habari katika Hospitali ya mkoa mjini Singida.
DSC06410
Basi la Zuberi T.119 AZZ lilokuwa likitokea Mwanza kuelekea jijini Dar-es-salaam na kupinduka katika eneo la kijiji cha Tumaini kata ya Issuna wilaya ya Ikungi wakati likimkwepa bibi aliyekuwa akikatisha barabara.(Picha na Nathaniel Limu).
DSC06407
Na Nathaniel Limu, Singida
BASI la kampuni ya Zuberi T.119 AZZ lililokuwa linatokea jijini Mwanza likielekea jijini Dar-es-salaam,limepinduka na kusababisha vifo vya abiria  wawili na kujeruhi vibaya wengine arobaini wakati likimkwepa bibi mmoja aliyekuwa anakatisha barabara.
 Ajali hiyo imetokea jana saa 7.30 mchana katika barabara kuu ya Sindida –Dodoma eneo la kijiji cha Tumaini kata ya Issuna wilaya ya Ikungi mkoani Singida.
Afisa wa makosa ya jinai mkoa wa Singida (RCO), Thobias Sedoyeka amesema kuwa basi hilo lililokuwa likiendeshwa na Fadhili Kalembo (35),lilipofika eneo la tukio,bibi mmoja alijitokeza akiwa anavuka barabara.
Amesema dereva wa basi alijitahidi kumkwepa bibi huyo lakini ghafla bibi alirudi tena barabarani kitendo kilichosababisha basi hilo kupinduka na kuserereka hatua zaidi ya 50 wakati likimkwepa kwa mara ya pili.
 “Basi hili lilimlalia mtoto mdogo ambaye aliweza kutolewa baada ya basi la Zuberi kunyanyuliwa na wichi ya lori ambalo lilikuwa linapita katika barabara hiyo”,amesema.
Kwa upande wake Mganga Mfawidhi wa hospitali ya mkoa ya mjini Singida, Deogratus Banuba amesema kuwa wamepokea maiti moja iliyotokana na ajali ya basi la Zuberi na kwamba bado wanaendelea kusubiri mwili wa mtoto aliyefia eneo la ajali.
 “Kwa upande wa majeruhi,tumepokea majeruhi 40 ambao wameumia vibaya sehemu mbalimbali ya miili yao ikiwemo kuvunjika mikono na miguu.Kati yao wanne,mikono yao imesagika vibaya na tumejitahidi kuirudisha katika hali yake”,amesema Dk.Banuba.
Amesema kuwa majeruhi wengine wanne,wao wamewapa  rufaa ya kwenda hospitali ya KCMC Moshi mjini mkoa wa Kilimanjaro.
Chanzo: Mo blog

Mwenyekiti BASATA awaasa wasanii nchini


Mwenyekiti wa Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA), Profesa Penina Mlama akikagua nyumba za wasanii katika kijiji cha Mwanzega, Mkuranga jana, kulia ni Mwenyekiti wa Mtandao wa Wasanii Tanzania (SHIWATA),Cassim Taalib na Katibu Mtendaji wa BASATA, Godfrey Mngereza

Mwenyekiti wa Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA), Profesa Penina Mlama akikagua nyumba za wasanii katika kijiji cha Mwanzega, Mkuranga jana, kulia ni Mwenyekiti wa Mtandao wa Wasanii Tanzania (SHIWATA),Cassim Taalib na Katibu Mtendaji wa BASATA, Godfrey Mngereza


Na Peter Mwenda, Mkuranga

MWENYEKITI wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA), Profesa Penina Mlama ametoa wito kwa wasanii kuchangamkia kuchangia ujenzi wa nyumba unaratibiwa na Mtandao wa wasanii Tanzania (SHIWATA) ili kujiandalia makazi.


Akizungumza baada ya kutembelea mradi wa ujenzi wa nyumba za wasanii katika kijiji cha Mwanzega, wilaya ya Mkuranga mkoani Pwani, Profesa Mlama alisema makazi ni sehemu ya maisha ya binadamu hivyo wasidharau mradi huo ni faida kubwa kwao.



Alisema nyumba ambazo ameziona ni nzuri, imara na zinauzwa bei ya chini ambayo huwezi kuzipata sehemu nyingine yoyote nchini Tanzania na kuongeza kuwa kujenga kwa lengo la kuishi pamoja kunatoa fursa ya wasanii kubuni njia nyingine ya kuanzisha miradi mbalimbali.



Profesa Mlama alitaka SHIWATA isikate tamaa bali iendelee kuwashawishi wasanii wajiunge na kuchangia ujenzi wa nyumba ili baadaye wasitafute visingizio kuwa hawakupewa fursa hiyo.



Naye Katibu Mtendaji wa BASATA,Godfrey Mngereza alisifu SHIWATA kubuni njia ya kuwasainia wasanii kupata makazi na kuahidi kuwa baraza hilo litatoa ushirikiano na kutoa ushauri kila unapohitajika.



Mwenyekiti wa SHIWATA, Cassim Taalib alisema mpango wa ujenzi wa nyumba za wasanii utaendelea kote nchini na kuwataka wasanii waungane kufanya kazi zao kwa pamoja.



Alisema mpaka sasa nyumba 38 zimekabidhiwa kwa wasanii waliochangia ujenzi katika kijiji cha Mwanzega Mkuranga na nyingine 21 zinatarajiwa kukabidhiwa Machi mwaka huu.



SHIWATA mbali ya kusimamia ujenzi wa nyumba za wasanii inasimamia matamasha ya wasanii wachanga (Underground) kuendesha makongamano ya kupambana na kuzuia dawa za kulevya na kutoa elimu na maadili kwa wasanii.

Mbunge Mchungaji Msigwa mahakamani kwa kujeruhi

Mbunge wa Jimbo la Iringa Mjini, Mch Peter Msigwa sambamba na mtuhumiwa mwingine
akiwa ndani ya mahakama ya wilaya ya Iringa jana kabla ya kuahirishwa kwa kesi yakeya kujeruhi mtu
Mbunge wa Jimbo la Iringa Mjini, Mch Peter Msigwa akizungumza na wakili anayemtetea
katika kesi yake ya kujeruhi mtu kwenye kampeni za siasa, Lwezaula Kaijage 
Mbunge wa Jimbo la Iringa Mjini, Mch Peter Msigwa sambamba na mtuhumiwa mwingine akiingizwa mahakama ya wilaya ya Iringa jana kujibu mashataka ya kujeruhi yanayomkabili

48 wanaswa vurugu za Morogoro


  Wakazi wa doma wilayani Mvomero wakiwa mbaroni kwa tuhuma za kufunga barabara ya Morogoro na Iringa wakishinikiza wafugaji kuondolewa eneo hilo.
WATU 48 wanashikiliwa na polisi mkoani hapa kwa tuhuma za kufunga barabara ya Morogoro na Iringa wakishinikiza wafugaji wa jamii ya Kimasai kuhamisha katika eneo la Doma wilayani Mvomero.
Kamanda wa polisi mkoani hapa Faustine Shilogile alisema kuwa tukio hilo limetokea Februari 6 mwaka huu majira ya saa 3 asubuhi.
Kamanda huyo alisema kuwa katika tukio hilo walifanikiwa kuwatia mbaroni wanawake 24 na wanaume 24 ambao wanadaiwa kufanya vurugu hizo.
Alisema kuwa fujo hizo zilitokea baada ya watu hao kudai kuwa wafugaji hao waliwapiga na fimbo wananchi wenzao waliokwenda porini kukata mkaa jambo lililowafanya nao kuamua kufunga barabara hiyo.
Hata hivyo kamanda huyo alisema kuwa walifanikiwa kufungua barabara hiyo majira ya saa 7 mchana baada ya kupiga mabomu ya mchozi kwa lengo la kuwatawanya wananchi hao.
Alisema kuwa hakuna madhara yeyote ya kibinadamu yaliotokea ingawa watu hao walijaribu kuwapiga mawe polisi hao .
Alisema kuwa kufanya hivyo ni kinyume cha sheria na kwamba watu hao wanatarajiwa kufikishwa mahakamani kesho ili kuweza kujibu tuhuma hizo.
Kwa upande wao wananchi hao wamalalamikia wafugaji hao kitendo chao cha kuingiza mifugo mashambani na kuharibu mazao njambo ambalo linawarudisha nyuma kimaendeleo.
Pia walilalamikia uongozi wa kijiji hicho cha Doma kwa kuwaingiza wafugaji kinyemela hali inayofanya kuwa wengi huku eneo la malisho likiwa dogo hali inayofanya wafugaji hao kuingiza mifugo yao mashambani.
Ibrahim Ndegalo alisema kuwa mbali na wafugaji hao kuwapiga lakini pia wamakuwa wakiwanyang’anya mali zao bila sabababu na kwamba maisha yao yamekuwa hayana amani.
 Credit:MACHAKU

FF watumia mabomu kutawanya wakulima Morogoro


Askari wa Kikosi cha kutuliza Fujo Akizima  Moto uliowashwa na wakulima waliofunga barabara ya Morogoro Iringa Leo Asubuhi.Wakulima hao walifunga Barabara hiyo kwa Lengo la kushinikiza kuonana na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dk Joel Bendera  Ili kutatua Mgogoro uliopo kati ya wakulima na wafugaji uliopo katika vijiji hivyo.Askari wa jeshi la Polisi walilazimika Kutumia Mabomu ya Machozi mara baada ya Wananchi wao kugoma Kuonana na Kamati ya ulinzi ya Wilaya ya Mvomero Ikiongozwa na Mkuu Wa Wilaya ya  mvomero


 Wananchi wa Kijiji cha Mangae wakiwa wamefunga Barabara wakiwa wamishika mawe na Silaha za Jadi wakikataa kabisa kufungua barabara hiyo wakitaka Mkuu wa Mkoa kuja Kuoanana Nao.

Mabomu ya machozi yametumika kuwatawanya wakulima wa eneo la Melela, Mvomero mkoani Morogoro waliokuwa wamefunga barabara ya Iringa - Morogoro wakimtaka Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera aende kusuluhisha mgogoro uliopo baina yao na wafugaji. Wakulima wa kijiji cha Mangae wilaya Mvomero wamefunga barbara kuu ya Morogoro Wakulima hao ambao wanalima katika Mashamba yaliopo eneo la Mkangazi 
baada ya wananchi kuvamiwa na kupigwa wakulima hao walikusanyikajana usiku na kufikia maamuziWakulima hao wanadai kuwa wenzao watano jana wamevamiwa na wafugaji wa kabila la Wamasai na kuwajeruhi vibaya kwa vitu vyenye ncha kali na kupelekea kulazwa katika Hospitali ya Mkoa Morogoro.
Mkuu wa Wilaya ya Mvomero, Anthony Mtaka alifika eneo hilo ambapo wananchi hao walikuwa wamechoma matairi na kusababisha mgongamano mkubwa wa magari yaendayo Iringa na yale yaelekeayo Moro lakini wakulima hao walikataa kumsikiliza wakimtaka mkuu wa mkoa. Baada ya vurugu kuwa kubwa, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Faustine Shilogile aliwaaamuru vijana wake wawatawanye wakulima hao ambao waligoma na kuanza kuwapiga kwa mawe kitendo kilichopelekea polisi kupiga mabomu ya machozi na kufanikiwa kuwatawanya.Wananchi takribani 20 wamekamatwa na polisi katika vurugu hizo.Kwa sasa hali kidogo imetulia na magari yameanza kupita eneo hilo
Askari wa Jeshi la Polisi Wakiwa Onyo wakulima wa Kijiji Hicho Kabla ya Kuanza Kutumia Mabomu ya Kutoa Machozi kwa Lengo la Kuwatanya

Rais Kikwete ahutubia mkutano wa Baraza la Vyama vya Siasa

 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Shariff Hamad, Msajili wa vyama vya siasa Jaji Francis Mutungi na viongozi  wa vyama mbalimbali vya siasa na maafisa wa serikali wakitoka kupata chakula cha mchana baada ya kufungua  mkutano wa Baraza la Vyama vya Siasa leo Februari 6, 2014 katika Ukumbi wa Mikutano wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es salaam
  Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maali Seif Shariff Hamad  katika picha ya pamoja na wenyeviti wa vyama vya siasa baada ya kufungua  mkutano wa Baraza la Vyama vya Siasa leo Februari 6, 2014 katika Ukumbi wa Mikutano wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es salaam.
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maali Seif Shariff Hamad  katika picha ya pamoja na Makatibu Wakuu wa vyama vya siasa baada ya kufungua  mkutano wa Baraza la Vyama vya Siasa leo Februari 6, 2014 katika Ukumbi wa Mikutano wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es salaam.
  Sehemu ya viongozi wa vyama mbalimbali vya siasa wakiomba dua kabla ya kuanza kwa mkutano wa Baraza la Vyama vya Siasa leo Februari 6, 2014 katika Ukumbi wa Mikutano wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es salaam.
 Sehemu ya viongozi wa vyama mbalimbali vya siasa katika mkutano wa Baraza la Vyama vya Siasa leo Februari 6, 2014 katika Ukumbi wa Mikutano wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es salaam. Picha na Issa Michuzi

Mchungaji afa maji akiiga kutembea juu ya maji kama YESU

KUTEMBEA juu ya maji siyo kazi rahisi na pengine inaweza kugeuka kilio kama mtu huna imani ya kutosha. 
Huko Nigeria mwanzoni mwa mwezi uliopita ilikuwa sikitisho kubwa kwa waumini baada ya mchungaji wao kusombwa na maji baada ya kujaribu kutembea juu ya maji kama vile Nabii Yesu alivyofanya wakati wake alipokuwa duniani.

Pastor Frank Kabele mwenye umri wa miaka 35, aliwaambia waumini wake kuwa mtu mwenye imani anaweza kufanya miujiza yeyote ila tu uwe na imani. 
Aliwaahidi wafuasi wake kuwa atatembea juu ya maji pindi tu atakapomaliza maombi yake. 
Lakini mambo yalienda ndivyo sivyo baada ya pastor huyo kujaribu kutembea katika mto mkubwa, alididimia mtoni humo na ilikuwa vigumu kwa waumini wake kumsaidia kwani maji yalikuwa na nguvu nyingi.
chanzo-http://www.zimeye.org/