STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 17, 2014

Huyu ndiye Amri Kiemba; Kiungo asiyechuja Msimbazi

Amri Kiemba akipowatungua Yanga na kutega sikio kusikiliza kelele za mashabiki wa Msimbazi
WAPO wanaoamini kadri umri wa makipa unavyozidi kusonga mbele ndivyo wanavyozidi kuwa mahiri langoni, tofauti na wachezaji wa nafasi nyingine hasa ya kiungo, beki au ushambuliaji.
Hata hivyo, kwa kiungo mshambuliaji Amri Kiemba, ni tofauti, kwani ujuzi wake wa kucheza na mpira na kufumania nyavu unazidi kuongezeka kadri siku zinavyozidi kusonga mbele na kushangaza mashabiki wa soka.
Msimu mmoja uliopita, kiungo huyo alikuwa akionekana siyo lolote ndani ya Simba kiasi cha kufungashiwa virago na kutakiwa kwenda kwa mkopo katika timu ya Polisi Dodoma iliyokuwa ikichechemea katika ligi msimu wa 2011/12.
Hata hivyo, mchezaji huyo akijiamini bado analiweza soka aliamua kuchomoa kwenda Polisi na kukubali kukaa nyumbani kabla ya kurejeshwa tena Msimbazi msimu uliopita na kuonyesha kiwango kikubwa kiasi cha kuwa 'lulu' ndani ya timu ya Taifa, Taifa Stars.
Katika msimu huo uliopita, Kiemba pia alikuwa gumzo kubwa ndani ya Simba, iliyokuwa imemuona amekwisha kwa kuifungia mabao muhimu na kuziba vilivyo pengo lililokuwa limeachwa na nyota wa Kimataifa wa Rwanda mwenye asili ya DR Congo, Patrick Mafisango aliyefariki kwa ajali ya gari.
Kasi yake uwanjani, akili ya kuwatoka mabeki na kufumua mashuti makali yaliyolenga lango la mpinzani na kuipa ushidi Simba na Taifa Stars, ilimfanya Kiemba anyakue tuzo ya Mwanasoka Bora kwa msimu wa 2012/13.
Tuzo hiyo iliyoandaliwa na Chama cha Wanasoka Tanzania (SPUTANZA) ilikuwa kama faraja kwa mchezaji huyo mpole na mcha Mungu kwa jinsi ilivyomfuta machozi kutoka kwenye misukosuko klabuni kwake.
Msimu huu pia mchezaji huyo ameendelea kuonyesha ni moto wa kuotea mbali akiisaidia timu yake kwenye mechi za Ligi Kuu Tanzania Bara duru la kwanza na hata sasa kwenye michuano ya Kombe la Mapinduzi iliyotarajiwa kumalizika jana.
Mabao yake mawili, moja dhidi ya AFC Leopards na jingine dhidi ya KMKM yaliisaidia kuivusha Simba hatua ya Robo Fainali kutoka Kundi B kabla ya kufunga jingine na kutengeneza jingine lililoipeleka Wekundu wa Msimbazi kucheza fainali na kulala bao 1-0 kwa KCCA.
Amri Kiemba (kulia) akiitumikia timu ya taifa, Taifa Stars
MKALI
Kiemba aliyewahi kung'ara na Klabu za Kagera Sugar, Moro United, Yanga na Miembeni, licha ya kwamba hana makeke, lakini ni mkali na anayejua majukumu yake uwanjani.
Ingawa amekuwa mkimya na asiyependa kuzungumza na vyombo vya habari, Kiemba anasema siri ya mafanikio yake ni kujituma, kusikiliza makocha na kushirikiana na wenzake mbali na kumtegemea Mungu kwa kila kitu.
Kiemba anayependa kula wali kwa marahage na vinywaji visivyo na kileo, anasema japo amekuwa hapendi kufichua mambo yake hadharani, lakini anashukuru soka kumsaidia kwa mengi na kumuomba Mungu amzidishie umri na kipaji chake aendelee kusakata kandanda.
Nyota huyo, aliyewahi kuzichezea kwa nyakati tofauti timu za taifa kuanzia za vijana U-17 na U-20 kabla ya kuitwa timu ya wakubwa anayoichezea mpaka sasa, anaseme hakuna mechi ngumu aliyowahi kuicheza au kukutana nayo kama ile ya Yanga dhidi ya Esperance ya Tunisia waliposhiriki Ligi ya Mabingwa Afrika.
Anasema anaikumbukwa kwa jinsi wapinzani wao walivyowafunika na ugenini kuwazabua mabao 3-0 kabla ya kutoshana nao nguvu ya kufungana bao 1-1 nyumbani na kung'olewa mashindanoni mwaka 2007.
Kiemba aliyekuwa akicheza soka kama beki wa kati, anasema licha ya kufunga mabao mengi, bao tamu kwake ni lile alililoifungia Kagera Sugar 2004 dhidi ya Polisi iliyosaidia timu yao kupanda Ligi Kuu.
"Nalikumbuka bao lile kwa jinsi nilivyolifunga kiufundi, mbali na kuisaidia kuipandisha Kagera Ligi Kuu msimu wa 2005/2006 tulipowafunga Polisi mabao 3-0," anasema.
Mkali huyo anayependa kutumia muda wake mwingi kusikiliza taarifa mbalimbali za habari kupitia redio na kufanya ibada, anasema soka la Tanzania bado linahitaji mabadiliko makubwa kuweza kufikia kwenye kilele cha mafanikio kwa kuwapo kwa mipango ya kuendeleza vipaji vya vijana.
Kiemba akiwajibika uwanjani kwenye mechi za Ligi Kuu
Kiemba akionyesha manjonjo yake
CHIMBUKO
Kiemba anaitaja Klabu ya Kagera Sugar kama ya mafanikio kwake, huku akiwataja walimu Malume na Kabuta waliomnoa kwenye michezo ya Umishumta na Idd Kipingu aliyempokea Shule ya Sekondari Makongo, kuwa ni watu asiowasahau kwa kukuza kipaji chake.
"Siwezi kuwasahau watu hawa kwa walivyosaidia kukuza na kuendelea soka langu," anasema.
Nyota huyo aliyewaasa wachezaji wenzake kuzingatia miiko na maadili ya uchezaji ili wacheze kwa muda mrefu, alizaliwa mwaka 1983 mjini Kigoma akiwa ni mtoto wa pili kati ya watano wa familia yao iliyokuwa na watoto wa kiume watatu na wa kike wawili.
Alisoma Shule ya Msingi Burka, Arusha alipoanza kuonyesha kipaji chake cha soka akiteuliwa katika timu ya shule na timu za Mkoa wa Arusha kwenye michuano ya Umishumta akishiriki fainali tatu za taifa kuanzia 1997-1999.
Chandimu alicheza katika timu ya Small Tiger na timu yake ya kwanza ya ligi ni Home Boys ya Arusha kabla ya kujiunga Shule ya Makongo alipoteuliwa kwa mara ya kwanza katika kikosi cha timu ya Taifa ya Vijana ya U-17, wakati akiwa anaichezea pia Karume Rangers.
Aliondoka Karume iliyokuwa na maskani yake Mbeya ikifahamika pia kama 44 KJ na kwenda kwa muda Pallsons ya Arusha, kisha kukimbilia Kagera Sugar aliyosaidia kuipandisha Ligi Kuu mwaka 2005 na kuonwa na Yanga iliyomnyakua msimu wa 2006/2007.
Aliachana na Yanga na kwenda Zanzibar kuichezea Miembeni kwa muda na kurejea Bara kujiunga na Moro United hadi msimu wa 2009/2010 aliponyakuliwa na Simba aliko hadi sasa.
Mafanikio yake kama mchezaji, Kiemba anasema ni kutwaa mataji kadhaa yakiwamo ya Ligi Kuu, Mapinduzi na Tusker akiwa na timu za Simba na Yanga.

AIBU! Wanawake wawili wanaswa na bangi Arusha

GEDSC DIGITAL CAMERA
Mkuu wa kitengo cha kuzuia na kupambana na madawa ya kulevya Mkoa wa Arusha Mrakibu Msaidizi wa Polisi (ASP) Aben Mgode akiwaonyesha waandishi wa habari misokoto 5000 pamoja na baadhi ya magunia 16 ya madawa ya kulevya aina ya bangi yaliyokamatwa kutokana na misako mbalimbali iliyofanyika mkoani hapa. (Picha na Rashid Nchimbi wa Jeshi la
Polisi Arusha)
****
Na Rashid Nchimbi wa Jeshi la Polisi Arusha
WATU saba wakiwemo wanawake wawili wamekamatwa na misokoto 5000 ya madawa ya kulevya aina ya bangi pamoja na mirungi kilo 47. Tukio hilo lilitokea mwishoni mwa wiki iliyopita katika eneo la Mti mmoja lililopo wilaya ya Monduli.
Mafanikio hayo yalitokana na msako shtukizi uliofanywa na jeshi la polisi Mkoani hapa kuanzia saa 12:00 asubuhi mpaka saa 10:00 jioni baada ya kufanya upekuzi katika magari mbalimbali na kupata madawa hayo ambayo yalikuwa yanasafirishwa na watuhumiwa hao kupitia magari ya abiria yaliyokuwa yakielekea Manyara, Singida, Dodoma na Mwanza.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisi kwake, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Liberatus Sabas watuhumiwa hao walikuwa wanayahifadhi madawa hayo kwenye mifuko ya “plastic” ili yasitoe harufu na kisha kuweka kwenye mabegi.
Aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni pamoja na Godwina Munisi (31) Mkazi wa Sombetini , Mwajuma Kingu (48) Mkazi wa Mbauda,  Fidelis Joseph (48) Mkazi wa Ngarenaro, Selemani Ally (34) Mkazi wa Olmatejoo, Omari Ally (25) Mkazi wa Babati Mkoani Manyara Kasimu Ayubu (39) Mkazi wa Tarakea Rombo Mkoani Kilimanjaro na Yasini Talian (40) Mkazi wa Ngarenaro.
Kamanda Sabas alisema kwamba watuhumiwa hao wanatarajiwa kufikishwa mahakamani mara baada ya upelelezi kukamilika.
Wakati huo huo katika msako unaoendelea wilayani Longido, jumla ya magunia 16 ya madawa ya kulevya aina ya bangi yamepatikana katika eneo la kijiji cha Leboo baada ya askari Polisi kufanya msako na kufanikiwa kupata magunia hayo 16 yaliyokuwa yanasafirishwa .
Kamanda Sabas alisema kwamba, askari hao walikuwa wanafanya msako usiku na mara baada ya watuhumiwa hao kugundua kuwa wanafuatiliwa walitelekeza magunia hayo 16 na kukimbia. Inasemekana kwamba watuhumiwa hao walikuwa wanatumia wanyama aina ya Punda kusafirishia madawa hayo ambapo magunia yalikuwa yamefungwa mawili mawili.
Hata hivyo Jeshi la Polisi Mkoani hapa bado linaendelea kuwatafuta watuhumiwa hao ili wafikishwe mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili.

Hawa ni baadhi ya wasanii wanaodaiwa kuwa membaz wa Freemasons

Rihanna amekuwa akitajwa kama kinara kwa wasanii wa kike
Jay Z na Kanye West wakisalimiana kwa ishara inayodaiwa ya Freemason

 
CHINI ni baadhi ya wasanii wanaotajwa kujihusisha au waliokuwa waabudu mashetani (Freemason)
 
Tupac Shakur (2Pac) – (Murdered For Trying To Expose Satan)
Ke$ha
Katy Perry
Justin Bieber
Chief Keef
Snoop Dogg
Skrillex (Sonny Moore)
Amy Winehouse – (Blood Sacrifice)
Britney Spears
Jay-Z – (Illuminati Recruit)
Kanye West
Rhianna
Beyonce
Whitney Houston – (Murdered For Trying To Expose Satan)
Miley Cyrus
Billy Ray Cyrus
Nicki Minaj
Carly Rae Jepsen
Lady Gaga
Katy Perry
Michael Jackson – (Murdered For Trying To Expose Stan)
Bob Dylan
Dr. Dre
Eminem
Cypress Hill
David Bowie
Madonna
Lil Wayne
Nas
Notorious B.I.G. – (Murdered For Trying To Expose Satan)
T-Pain
Aayliah
Chris Brown
Rick Ross
P-Diddy
Justin Timberlake – (Illuminati Recruit)
Drake
Wiz Khalifa
Frank Sinatra
Elvis Presley
Bob Marley
Rebecca Black
Pitbull
David Guetta
Adelle
Alicia Keys
Jennifer Lopez
50 Cent
DMX (Ex Member)
Taylor Swift
Demi Lovato