STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, November 21, 2013

Simanzi tupu rufaa ya Babu Seya

MSANII JOSEPH MARA AKIONGEA NA WAANDISHI WA HABARI MARA BAADA YA KUTOLEWA HUKU NA KUTUPILIA MBALI
WATU MBALIMBALI PAMOJA NA JAMAA ZAO WAKICHUNGULIA KWENYE  CHUMBA CHA MAHAKAMA MARA BAADA YA KUTUPILIA MBALI KWA KUTUMIA MLANGO WA VIOO
BAADHI YA NDUGU WAKILIA WAKATI NGUZA NA  MWANAE WAKIPANDA GARI LA MAGEREZA LEO
BAADHI YA NDUGU WAKILIA WAKATI NGUZA NA  MWANAE WAKIPANDA GARI LA MAGEREZA LEO
BAADHI YA NDUGU WAKILIA WAKATI NGUZA NA  MWANAE WAKIPANDA GARI LA MAGEREZA LEO
BAADHI YA WATU MBALIMBALI WALIOFIKA KATIKA MAHAKAMA YA RUFAA LEO
NDUGU NA JAMAA WAKILIA KWA HUZUNI KATIKA MAHAKAMA HIYO LEO
BAADHI YA NDUGU WAKIMUAGA NGUZA VIKING NA MWANAE JOHNSON NGUZA 'PAPII KOCHA'
WANAMUZIKI NGUZA VIKING NA JOHNSON NGUZA 'PAPII KOCHA'  WAKIWAAGA NDUGU NA MASHABIKI NA JAMAA WALIOFIKA KWENYWE MAHAKAMA YA RUFAA LEO BAADA YA KUTUPIWA MBALI

WAKIPANDA KWENYE GARI LA MAGEREZA

WATUI MBALIMBALI PAMOJA NA JAMA WAKIMUAGA BABU SEYA WAKATI GARI LA MAGEREZA LIKONDOKA LEO MAHAKAMA YA RUFAA

WAKIPANDA KWENYE GARI LA MAGEREZA

WAKITOKA KATIKA CHUMBA CHA MAHAKAMA YA RUFAA LEO

BAADHI YA JAMAA ZAO WAKILIA HUKU WAKIWAPIGIA SIMU JAMAA ZAO LEO

Kilimanjaro Stars kwenda Kenya J'3 Kim ataja silaha 23um

Kocha Kim Poulsen
KOCHA Mkuu wa Kilimanjaro Stars, Kim Poulsen ametaja kikosi cha wachezaji 23 watakaoshiriki michuano ya Kombe la CECAFA Challenge inayofanyika nchini Kenya kuanzia Novemba 27 mwaka huu.
Kilimanjaro Stars iliyotwaa kombe hilo mara ya mwisho mwaka 2010 chini ya Kocha Jan Poulsen, na ambayo imepangwa kundi B katika michuano ya mwaka huu itacheza mechi yake ya kwanza Novemba 28 mwaka dhidi ya Zambia kwenye Uwanja wa Machakos.
Wachezaji wanaounda kikosi hicho cha Tanzania Bara ni makipa Deogratius Munishi (Yanga), Ivo Mapunda (Gor Mahia, Kenya) na Aishi Manula (Azam). Mabeki ni Erasto Nyoni (Azam), Himid Mao (Azam), Ismail Gambo (Azam), Kelvin Yondani (Yanga), Michael Pius (Ruvu Shooting) na Said Moradi (Azam).
Viungo ni Amri Kiemba (Simba), Athuman Idd (Yanga), Frank Domayo (Yanga), Haruna Chanongo (Simba), Hassan Dilunga (Ruvu Shooting), Ramadhan Singano (Simba) na Salum Abubakar (Azam).
Safu ya ushambuliaji inaundwa na Elias Maguli (Ruvu Shooting), Faridi Musa (Azam), Joseph Kimwaga (Azam), Juma Liuzio (Mtibwa Sugar), Mbwana Samata (TP Mazembe, DRC), Mrisho Ngasa (Yanga) na Thomas Ulimwengu (TP Mazembe, DRC).
Kilimanjaro Stars inatarajia kuondoka Jumatatu (Novemba 25 mwaka huu) kwenda Nairobi kushiriki michuano hiyo itakayoanza Novemba 27 mwaka huu na kumalizika Desemba 13 mwaka huu. 
Katika hatua nyingine; Mechi ya kirafiki ya kimataifa ya FIFA Date kati ya Tanzania (Taifa Stars) na Zimbabwe (The Warriors) iliyochezwa juzi (Novemba 19 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam imeingiza sh. 50,980,000 kutokana na watazamaji 7,952.
Tiketi za kushuhudia mechi hiyo ziliuzwa kwa sh. 5,000, sh. 10,000, sh. 15,000, sh. 20,000 na sh. 30,000.
Mgawanyo wa mapato hayo ulikuwa kama ifuatavyo; asilimia 18 ya Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) ni sh. 7,776,610.17 wakati wa gharama za uchapaji tiketi ni sh. 3,682,560.
Asilimia 15 ya uwanja sh. 5,928,124, asilimia 20 ya gharama za mechi sh. 7,904,166 na asilimia 5 ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) sh. 1,976,041.
Asilimia 60 ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) sh. 17,784,373 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 889,219 ambayo ni asilimia 5 kutoka kwenye mgawo wa TFF.

Maafisa 77 wa Jeshi la Polisi waula...Soma majina yao

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
JESHI LA POLISI TANZANIA


RAISs wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe. Dkt Jakaya Mrisho Kikwete, amewapandisha vyeo maafisa 77 wa Jeshi la Polisi kutoka cheo cha Kamishina Msaidizi wa Polisi (ACP) kuwa Kamishina Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP).

Miongoni mwa maafisa waliopandishwa vyeo kutoka cheo cha Kamishina Msaidizi wa Polisi kuwa Kamishina Msaidizi Mwandamizi wa Polisi ni pamoja na Mkuu wa Upelelezi Kanda Maalum ya Dar es Salaam Kamishina msaidizi wa Polisi ACP Ahmed Msangi, Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Temeke Kamishina Msaidizi wa Polisi (ACP) Engelbert Kiondo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala ACP. Marietha Minangi, Kamanda wa Polisi mkoa wa Mbeya ACP. Diwani Athumani na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida Geofrey Kamwela.

Wengine ni Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kigoma ACP. Frasser Kashai, Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro ACP. Faustine Shilogile, Kamanda wa Polisi mkoa wa Dodoma ACP. David Misime, Kamanda wa Polisi mkoa wa Mara ACP. Ferdinand Mtui, Kamanda wa Polisi mkoa wa Tanga ACP. Costantine Massawe, Kamanda wa Polisi mkoa wa Geita ACP. Leornad Paul, Kamanda wa Polisi mkoa wa Pwani ACP. Ulrich Matei na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Lindi ACP. George Mwakajinga.


Zaidi ya hao wengine ni, Kamanada wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP. Evarist Mangala, Kamanda wa Polisi mkoa wa Ruvuma Deusedit Nsimeke, Kamanada wa Polisi mkoa wa Njombe ACP. Fulugence Ngonjani, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi Dhahiri Kidavashari na baadhi ya Makamanda wa vikosi, Wakuu wa vitengo, Mkuu wa Chuo cha Taaluma ya Polisi Moshi na Mkuu wa Chuo cha Taaluma ya Polisi Dar Es salaam.


Kufuatia kupandishwa vyeo kwa Maafisa hao wa Jeshi la Polisi, Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Said Mwema, amemshukuru Rais wa Jamuhuru ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe. Dkt Jakaya Mrisho Kikwete kwa kutambua mchango wa Jeshi la Polisi katika kuimarisha ulinzi na usalama wa raia na mali zao.

Aidha, IGP Mwema amewapongeza wale wote waliopandishwa vyeo, na kuwataka kuendelea kufanya kazi kwa juhudi na weledi katika kuimarisha Usalama wa raia na mali zao kwa kuwa cheo ni dhamana.



Imetolewa na:
Advera Senso-SSP
Msemaji wa jeshi la polisi