STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, August 10, 2013

Arsenal yaikamua Man City 3-1, Liver ikizama kwa Celtic

Hands on: Carl Jenkinson accidentally catches Samir Nasri in the face with an arm
Wachezaji wa Arsenal na Manchester City
KLABU ya Arsenal jioni hii imeizabua Manchester City kwa mabao 3-1 katika pambano lililofanyika  kwenye Uwanja wa Olimpiki mjini Helsinki ukiwa ni mchezo wa kirafiki.
Arsenal inayohaha kumsaka mshambuliaji wa Liverpool, Luis Suarez, walipata mabao yao kupitia kwa Theo Walcott dk ya 9, Aaron Ramsey dk 59 na Olivier Giroud dk 62.
Bao la kufutia machozi la City liliwekwa kimiani 'jioni' kabisa na Negredo dk 80.
Nayo Liverpool imejikuta ikiwashwa bao 1-0 na Celtic ya Scotland huku Tottenham ikitoshana nguvu na Espaniol katika mechi zingine za kirafiki zilizochezwa leo.

Utata sakata la Sheikh Ponda, Polisi waruka kimanga

clip_image001
TUKIO la kupigwa risasi na kujeruhiwa kwa Sheikh Ponda Issa Ponda mjini Morogoro ni utata mtupu wakati baadhi ya waumini wa kiislam wa mjini humo wakithibitisha taarifa hizo kwamba Sheikh wao kapigwa risasi begani, jeshi la Polisi mkoani humo limekanusha tukio hilo, japo linalikiri walitaka kumkamata jioni hii.
Kamanda wa Polisi wa mkoani humo, Faustine Shilogile, amenukuliwa hivi punde na Radio One Stereo na kudai jeshi lake lilikuwa likimvizia kumkamata Sheikh Pondaa ya kuhudhuria Kongamano la Wahadhiri wa Kiislam mkoani Morogoro na kuhutubia, lakini wakazidiwa ujanja na waumini waliomkinga na kumtorosha Sheikh wao huyo machachari asiishie mikononi mwa dola.
Kamanda Shilogile, alisema suala la Ponda kupigwa risasi na kujeruhiwa au kuuwawa kama habari hizo zilivyozagaa mjini humo ni uzushi kwa vile sheikh huyo hajafikishwa kituo chochote cha polisi au hospitali kama ni kweli kajeruhiwa.
Kamanda Shilogile

"Hizi ni habari zilizozagaa mjini hapa wengine wakidai ameuwawa, ila ukweli ni kwamba Polisi hawajafanya kitendo chochote dhidi ya Ponda zaidi ya kwamba tulitaka kumkamata mara baada ya kuhutubia kwa dakika kama 5 kwa kutambua kuwa anasakwa," alisema Shilogile.
Aliongeza wakati wanamvizia Sheikh Ponda liyechelewa kwenye kongamano hilo likliwa kama dakika 10 limalizike waumini wa kiislam aliodai walikuwa wengi mno walimtorosha na hivyo wao kumkosa na kudai kuwa wanafuatilia mahali alipofichwa na kama ni kweli alijeruhiwa wajue anatibiwa wapi.
Utata unakuja wakati Shilogile akisema hawakufanya tukio lolote la kupiga risasi, je wanafuatilia mahali anapotibiwa kwa sababu zipi? Kadhalika waumini waliozungumza kwa njia ya simu na MICHARAZO wamedai tukio hilo limetokea wakati Polisi walipovamia taksi iliyomleta Sheikh Ponda na katika purukshani walifyatua mabomu ya machozi na risasi za moto ambapo ilimpata begani na kumjeruhi.
"Hawa watu wanatuchokoza Waislam ili tuonekane wakorofi tunasherehekea sikukuu yetu kwa amani wanatuletea mambo ya kihuni walitaka kumkamata Sheikh wetu nasi tukasimamia kidete na kuwagomea ndipo wataamua kutumia nguvu kupiga risasi na kwa bahati ikampiga risasi ya bega na kumjeruhi wanakanusha nini," alisema mmoja wa mashuhuda hao.
Hata hivyo bado imekuwa vigumu kujua mahali alipo sheikh huyo inayedaiwa alikimbizwa Hospitali ya mkoa na kabla ya kuanza kupata matibabu baada ya kubainiwa Polisi wanamfuatiliwa alitoroshwa na waumini hao na kutofahamika kapelekwa hospitali gani kupata matibabu, japo Polisi wanasema wameanza upelelezi wa mahali alipo kupata ukweli wa uvumi huo ambao umesambaa nchi nzima kama moto wa nyikani.
MICHARAZO bado inafuatilia kujua ukweli wa taarifa hizi na kila tukipata habari mpya tutawapenyezea.

Simba yawapa raha mashabiki wao 'Simba Day' wapiga mtu 4-1

Kiungo wa Simba, Amri Kihemba akimtoka beki wa Sports Club Villa ya Uganda katika mchezo wa kirafiki uliofanyika kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam leo., Siomba imeshinda 4-1. (Picha na Habari Mseto Blog) 
 Kipa wa Sports Club Villa ya Uganda, Elungat Martins akiota mpira katika nyavu la lango lake baada ya mshambuliaji wa Simba, Betram Mombeki kuifungia timu yake bao la tatu katika mchezo wa kirafiki uliofanyika kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam
Tunda Man, akitumbuiza katika tamasha hilo.

Breaking News: Sheikh Ponda kapigwa risasi Morogoro

Sheikh Ponda katika harakati zake za kidini


TAARIFA zilizotufikia muda huu kutoka Morogoro ambazo hata hivyo bado hazijathibitishwa rasmi zinasema kuwa Katibu wa Kutetea Haki za Waislam Tanzania na Sheikh maarufu nchini, Sheikh Ponda Issa Ponda amepigwa risasi.
Habari zilizotumwa kwa njia ya ujumbe mfupi toka mkoani humi zinadai kuwa Sheikh Ponda alipigwa risasi hiyo na wanaodaiwa askari Polisi na kujeruhiwa.
MICHARAZO ilijaribu kuwasiliana na masheikh kadhaa ili kuthjibitisha taarifa hizo, ambapo mmoja wa viongozi wa Baraza la Habari za Vijana la Kiislam (BAHAKITA) Sheikh Sadick Godegode alisema hata yeye kazipata taarifa hizo ila bado anaendelea kuzifuatilia toka Morogoro.
"Ni kweli hata mimi nimezipata taarifa hizo kwamba Sheikh wetu, Ponda Issa Ponda kapigwa risasi ya bega, ila bado hatujathibitisha japo jana alikuwa mmoja wa walihudhuria Baraza la Idd lililofanyika msikiti wa Kichangani," alisema Sheikh Sadick.
Blogu hii inafanya jitihada za kupata ukweli wa taarifa hizo ambazo huenda zisiwe nzuri kwa waumini wa Kiislam ambao wapo katika sherehe za sikukuu ya Eid.

Zaidi ya Mil 100 kutumika mazishi wa Bilionea na Tanzanites

Mwili wa Erasto Msuya baada ya kupigwa risasi.
 

IKIWA ni takribani siku tatu zimepita tokea mfanyabiasha wa madini ya Tanzanite na mmiliki wa hotel kitali ya S.G Resort iliyopo jijini Arusha aliyefahamika kwa jina la Erasto Msuya kupigwa risasi 21 na kumsababishia kifo papo hapo katika eneo la njia panda ya KIA wakati akitoka Mirerani kuelekea Arusha mjini majira ya mchana.
Habari kutoka katika kamati ya mazishi inayoundwa na wafanyabiashara wa madini ya Tanzanite, ikiongozwa na kaka mkubwa marehemu Gady Msuya, anasema zaidi ya shilingi milioni mia moja (100,000,000/=) inatarajiwa kutumika kugharamia mazishi ya mfanyabiashara huyo bilionea wa madini yav Tanzanite. Na kaka wa Marehemu  (Gady) aliendelea kusema kuwa gari maalumu la kubeba mwili wa marehemu na jeneza vimeagizwa kutoka Nairobi, nchini Kenya kwa gharama ya Shilingi milioni nane (8,000,000/=).
 Kiasi hicho cha zaidi ya milioni mia moja kinarajiwa kuchangwa na wafanyabiashara wenzake wa madini . Pia wanatarajia kulipia magari maalumu yatakayotumika kwenye msafara wa mazishi ya Erasto Msuya yanayotarajiwa kufanyika nyumbani kwake Mirerani, wilayani Simanjiro siku ya jumanne ya tarehe 13 August 2013. 

Leo ni Simba Day, Msimbazi kutambulisha mpya ikiivaa SC Villa ya UgandaSimba kutambulishja

Kikosi kipya cha Simba
Kocha Kibadeni akisalimiana na wadau wa Simba
TIMU ya soka ya Simba leo itatambulisha nyota wake wapya wakati itakapocheza mechi ya kirafiki ya kimataifa dhidi ya SC Villa ya Uganda.
Mechi hiyo itakayochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ni sehemu ya maadhimisho ya tamasha la Simba Day, ambalo hufanyika kila mwaka kabla ya kuanza kwa ligi kuu.

Katibu Mkuu wa Simba, Evod Mtawala alisema jana kuwa, wachezaji watakaotambulishwa leo ni pamoja na mshambuliaji wa kimataifa wa Burundi, Hamisi Tambwe na beki wa kimataifa wa nchi hiyo, Kaze Gilbert.

Wachezaji wengine wapya watakaotambulishwa leo ni beki Joseph Owino na mshambuliaji, Betram Mombeki.

Mtawala alisema mechi hiyo itapambwa na burudani kutoka kwa wasanii wa muziki wa kizazi kipya wa kundi la TMK Wanaume Family na Snura, anayetamba kwa kibao chake kipya cha Majanga.

Wakati huo huo, Coastal Union ya Tanga leo itawatambulisha nyota wake wapya wakati itakapocheza mechi ya kirafiki dhidi ya kombaini ya Polisi.

Mkurugenzi wa Ufundi wa Coastal Union, Nassor Bin Slum alisema jana kuwa,mechi hiyo itapigwa kwenye Uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga.

Aliwataja wachezaji wapya watakaotambulishwa leo kuwa ni Haruna Moshi 'Boban', Juma Nyoso, Yayo Lutimbi kutoka URA ya Uganda na Crispin Odula kutoka Bandari ya Kenya.

Sheikh ashambuliwa msikitini wakati wa Swala ya Eid, kisa....!


Kamanda wa Polisi mkoa wa Mbeya Diwani Athumani

WAUMINI wa dini ya Kiislamu waliokuwa katika ibada ya Swala ya Idd El Fitri katika msikiti mkuu wa Ijumaa uliopo Wilayani Kyela mkoani Mbeya jana walikumbwa na taharuki baada ya Shekhe wao aliyekuwa akiongoza ibada kuvamiwa kibla wakati akiendesha ibada na kujeruhiwa.
Tukio hilo la aina yake limetokea majira ya asubuhi ambapo Shekhe huyo aliyetambuliwa kwa jina la Nuhu Mwafilango alishambuliwa akiwa katikati ya sijida baada ya mtu mmoja aliyedaiwa kuwa ni mwanafunzi wa shule ya sekondari ya kutwa Kyela Ally Mwangosi kumpiga Shekhe huyo na kitu chenye ncha kali kichwani.
Taarifa kutoka msikitini hapo zinadai kuwa mara baada ya mwanafunzi huyo kupita upande wa Kibla na shekhe huyo na kupigwa chenye ncha kali alipiga ukelele wa kuomba msaada na hivyo kuibua taharuki miongoni wa waumini waliokuwa wakiswali msikitini hapo.
Mwenyekiti wa Baraza Kuu la Waislamu Wilayani Kyela Bw. Daudi Mwenda alisema kuwa mara baada ya Shekhe huyo kuvamiwa na kupigwa waumini walimuokoa na kumkimbiza katika Hospitali ya Wilaya kwa ajili ya kupatiwa matibabu.
Bw. Mwenda alisema kuwa Shekhe huyo ameumizwa vibaya eneo la kichwani ambapo damu nyingi zilivuja mara baada ya kupigwa na kwamba mbali na Shekhe huyo waumini wengine wawili waliokuwa wakijaribu kumuokoa walijeruhiwa kwa kuchomwa na visu.
Wengine waliojeruhiwa katika tukio hilo ni pamoja na mweka hazina wa BAKWATA wilaya Ustadhi Khamis Husein aliyejeruhiwa kichwani na sikioni.
Baadhi ya waumini waliokuwepo katika ibada hiyo walisema kuwa tukio hilo lilitokea wakati waumini wote wakiwa wamesujudu ndipo waliposikia kelele na vurugu ambapo aliinuka mtu mmoja aliyekuwa na kitu mfano wa nondo na kumpiga nayo Shekhe kichwani.
Mmoja wa waumini aliyejitambulisha kwa jina la Idd Husein alisema kuwa wakati kijana huyo aliyekuwa na kitu kinachofanana na nondo liliibuka kundi la watu wengine waliomsaidia na hivyo kuibuka vurugu kubwa iliyosababisha ibada ya swala ya Idd kuvunjika.
Akizungumzia tukio hilo Katibu wa BAKWATA mkoa wa Mbeya Shekhe Juma Killah alisema kuwa vurugu hizo zimetokea katika swala ya Idd na wahusika wa vurugu hizo ni waislamu ambao wanaipinga BAKWATA.
 ‘’Hiki ni kikundi cha waislamu waliotoka Jijini Dar es salaam kimekuja huku na kimesambaa katika wilaya zote za mkoa wa Mbeya kinashawishi watu kuipinga BAKWATA na  kinafanya mambo ambayo BAKWATA hatukubaliani nayo,’’alisema Shekhe Killah.
Alisema kuwa kikundi hicho kilikuwa kikimtuhumu Shekhe wa Wilaya kuwa ni mshirikina na kwamba kutokana na hali hiyo hakupaswa kuongoza ibada msikitini na badala yake wao ndio waliopaswa kuongoza ibada msikitini hapo.
Kwa upande wake Shekhe wa BAKWATA mkoa wa Mbeya Mohamed Mwansasu alisema kuwa kitendo hicho kimeudhalilisha Uislamu na kwamba kilichofanywa na kundi hilo la watu si mafundisho ya dini ya Kiislamu.
Hata hivyo Shekhe Mwansasu alienda mbali zaidi na kusema kuwa katika kikundi hicho wapo  baadhi ya waumini wanaodaiwa kuwa ni askari polisi ambapo inadaiwa kuwa katika moja ya swala ya Ijumaa wiki iliyopita imamu aliyekuwa akiswalisha alivutwa kanzu yake na kutakiwa kutoka eneo la kuongozea ibada ili kuwapisha wao waendeshe ibada hiyo.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Mbeya Bw. Athumani Diwani amekiri kutokea kwa tukio hilo ambapo alisema kuwa watu sita wanashikiliwa na Polisi kufuatia vurugu hiyo iliyotokea majira ya saa 2:30 katika msikiti mkuu wa Ijumaa wakati wa swala ya Idd el Fitri.
Kamanda Diwani alisema kuwa kundi la waislamu wanaojiita kuwa ni wenye itikadi kali walivamia msikitini wakati waumini wengine wakiwa wameinama wakisujudu na kumvaa imamu kwa kumpiga kwa mateke na ngumi huku wakiwa na nondo, mikasi na visu.
Alisema waumini hao walikuwa na madai kuwa hawamtaki Shekhe huyo na kwamba uwezo wake ni mdogo katika dini.
Alisema kuwa Shekhe huyo aliokolewa na baadhi ya waislamu ambapo aliwataja walioshikiliwa na polisi kuwa ni pamoja na Mashaka Kassim(30)Issa Juma(37),Ahmed Kassim Magogo(35) Ibrahimu Shaaban(17) ambaye ni mwanafunzi wa shule ya sekondari ya kutwa ya Kyela anayesoma kidato cha Nne,Ambokile Mwangosi,(19)mwanafunzi wa kidato cha tatu shule ya sekondari Kyela, Sadick Abdul(28).

Kamanda Diwani alisema kuwa taratibu zinafanyika ili watuhumiwa wafikishwe mahakamani.

Polisi Zanzibar watangaza 'bingo' kwa waliowajeruhi Waingereza


 
KAMANDA wa Polisi, Kamishna Musa Ali Musa amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imeahidi kutoa Shilingi milioni 10/= kwa mtu yeyote atakayetoa taarifa zitakazofanikisha kukamatwa kwa watu waliowashambulia mabinti wawili kutoka Londona, Uingereza,  Kirstie Trup na Katie Gee.

Mabinti hao walishambuliwa kwa tindikali usoni, kifuani na mikononi siku ya Jumatano walipokuwa njiani kuelekea kwenye chakula cha jioni.


Kwa sasa raia hao wameshapelekwa kwa Uingereza kwa ajili ya matibabu zaidi huku vyombo vya habari nchini humo vikilitia chumvi tukio hilo kiasi cha kuitia doa Tanzania mbele ya uso wa dunia.

Bomoabomoa ya maghorofa Dar yanza

ASKARI POLISI WAKIWA KATIKA DORIA WAKATI WA UBOMOAJI WA MAGOROFA KATIKA BARABARA YA SAMORA LEO


ENEO LA MAGOROFA YANAYOBOMOLEWA KATIKATI YA MJI BARABARA YA SAMORA JIJINI DAR ES SALAAM MAGOROFA HAYO YALE AMBAYO YAMESHA KUWA MAGOFU LEO

JIMMY MASTER NA UJIO MPYA WA DOUBLE J FINAL

Nguli wa filamuza (Action) nchini Jimmy Master akiwa ameshika
moja ya tuzo yake katika tuzo zilizoandaliwa na kampuni maarufu ya filamu 
nchini Steps.
YULE muongozaji na mwigizaji Jimmy Mponda 'Jimmy Master' aliyetikisa na mfululizo wa filamu za misuko iliyotoka sehemu ya kwanza hadi ya tatu na baadaye kujiongezea jina lingine akiitwa
J Plus.
Kwa sasa nyota huyo amefunguka  kuwa yukombioni kutoa muvi ya mwisho inayoitwa Doble J Final  huku ujio huo ukiwa ni wa mwisho kutoka baada ya kutangulia  na Doble J sehemu ya kwanza na yapili zilizotoka mwaka jana.
"Mwaka jana nilifanikiwa kukonga nyoyo za mashabiki wa filamu hususani wanaopagawa 
na filamu za mapigano na kujawa mambo ya  kipelelezi,"alisema J Plus.
Alisema Doble J Final pia ni ujio wake wa filamu nyingine ya mapigano na kuna heka heka za kipelelezi ndani. J Plus aliyezoeleka sasa katika kuonesha ubabe wa kufa mtu , kwa sasa ujio wake huo unao tazamiwa kuingia sokoni mapema tu , mwezi ujao .
Pia amemshirikisha mbabe mwingine katika filamu za mapigano Ibrahim Mbwana  'Bad Boy' na pia wamo nyota wengine katika dulu la filamu kama Charles Magari , Hashim Kambi na Veronica Viankero.

Miyeyusho amchapa Mzambia kwa KO Dar Live


Bondia Mtanzania Francis Miyeyusho (kulia)  akionyeshana kazi na Fidelis Lupupa wa Zambia wakati wa  mpambano wao wa kirafiki wa kimataifa uliofanyika wakati wa Idd katika ukumbi wa Dar Live Mbagal, ambapo Miyeyusho alishinda kwa K.O ya raundi ya nane.

Bondia Kassim Rajabu akiumana na Kelvin Fabian katika pambano lao uliofanyika jana Dar Live, ambapo Fabian aliibuka mshindi kwa pointi.
Bondia Godfrey Pancho kushoto akioneshana ufundi wa kutupiana makonde na Hamisi Mohamedi wakati wa mpambano wao uliofanyika sikukuu ya Idd mosi katika ukumbi wa Dar Live Mbagala
Bondia Godfrey Pancho kulia akioneshana ufundi wa kutupiana makonde na Hamisi Mohamedi wakati wa mpambano wao uliofanyika sikukuu ya Idd mosi katika ukumbi wa Dar Live Mbagala
Bondia Chipaki Chipindi akiwa na mashabiki wake baada ya kumkarisha raundi ya kwanza bondia Ramadhani Kido

Bondia Fidelis Lupupa wa Zambia akiwa chini amekaa akijifikilia kuwa aendelee au asienderee baada ya kupigwa na bondia Mtanzania Francis Miyeyusho wakati wa mpambano wao uliofanyika katika ukumbi wa Dar Live Mbagala Dar es salaam Miyeyusho alishinda kwa KO ya raundi ya nane 
Bondia Mtanzania Francis Miyeyusho kulia  akipambana na Fidelis Lupupa wa Zambia wakati wa  mpambano wao wa kirafiki wa kimataifa uliofanyika wakati wa Sikuku ya Iddi katika ukumbi wa Dar Live Mbagala Miyeyusho alishinda kwa K.O ya raundi ya nane 
Bondia Fidelis Lupupa wa Zambia akiwa chini amekaa akijifikilia kuwa aendelee au asienderee baada ya kupigwa na bondia Mtanzania Francis Miyeyusho wakati wa mpambano wao uliofanyika katika ukumbi wa Dar Live Mbagala Dar es salaam Miyeyusho alishinda kwa KO ya raundi ya nane 
Bondia Mtanzania Francis Miyeyusho kushoto  akipambana na Fidelis Lupupa wa Zambia wakati wa  mpambano wao wa kirafiki wa kimataifa uliofanyika wakati wa Sikuku ya Iddi katika ukumbi wa Dar Live Mbagala Miyeyusho alishinda kwa KO ya raundi ya nane 

MIYEYUSHO AKISHANGILIA USHINDI

MIYEYUSHO AKIWA KATIKA POZI