STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, August 10, 2013


JIMMY MASTER NA UJIO MPYA WA DOUBLE J FINAL

Nguli wa filamuza (Action) nchini Jimmy Master akiwa ameshika
moja ya tuzo yake katika tuzo zilizoandaliwa na kampuni maarufu ya filamu 
nchini Steps.
YULE muongozaji na mwigizaji Jimmy Mponda 'Jimmy Master' aliyetikisa na mfululizo wa filamu za misuko iliyotoka sehemu ya kwanza hadi ya tatu na baadaye kujiongezea jina lingine akiitwa
J Plus.
Kwa sasa nyota huyo amefunguka  kuwa yukombioni kutoa muvi ya mwisho inayoitwa Doble J Final  huku ujio huo ukiwa ni wa mwisho kutoka baada ya kutangulia  na Doble J sehemu ya kwanza na yapili zilizotoka mwaka jana.
"Mwaka jana nilifanikiwa kukonga nyoyo za mashabiki wa filamu hususani wanaopagawa 
na filamu za mapigano na kujawa mambo ya  kipelelezi,"alisema J Plus.
Alisema Doble J Final pia ni ujio wake wa filamu nyingine ya mapigano na kuna heka heka za kipelelezi ndani. J Plus aliyezoeleka sasa katika kuonesha ubabe wa kufa mtu , kwa sasa ujio wake huo unao tazamiwa kuingia sokoni mapema tu , mwezi ujao .
Pia amemshirikisha mbabe mwingine katika filamu za mapigano Ibrahim Mbwana  'Bad Boy' na pia wamo nyota wengine katika dulu la filamu kama Charles Magari , Hashim Kambi na Veronica Viankero.

No comments:

Post a Comment