STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, August 10, 2013

Utata sakata la Sheikh Ponda, Polisi waruka kimanga

clip_image001
TUKIO la kupigwa risasi na kujeruhiwa kwa Sheikh Ponda Issa Ponda mjini Morogoro ni utata mtupu wakati baadhi ya waumini wa kiislam wa mjini humo wakithibitisha taarifa hizo kwamba Sheikh wao kapigwa risasi begani, jeshi la Polisi mkoani humo limekanusha tukio hilo, japo linalikiri walitaka kumkamata jioni hii.
Kamanda wa Polisi wa mkoani humo, Faustine Shilogile, amenukuliwa hivi punde na Radio One Stereo na kudai jeshi lake lilikuwa likimvizia kumkamata Sheikh Pondaa ya kuhudhuria Kongamano la Wahadhiri wa Kiislam mkoani Morogoro na kuhutubia, lakini wakazidiwa ujanja na waumini waliomkinga na kumtorosha Sheikh wao huyo machachari asiishie mikononi mwa dola.
Kamanda Shilogile, alisema suala la Ponda kupigwa risasi na kujeruhiwa au kuuwawa kama habari hizo zilivyozagaa mjini humo ni uzushi kwa vile sheikh huyo hajafikishwa kituo chochote cha polisi au hospitali kama ni kweli kajeruhiwa.
Kamanda Shilogile

"Hizi ni habari zilizozagaa mjini hapa wengine wakidai ameuwawa, ila ukweli ni kwamba Polisi hawajafanya kitendo chochote dhidi ya Ponda zaidi ya kwamba tulitaka kumkamata mara baada ya kuhutubia kwa dakika kama 5 kwa kutambua kuwa anasakwa," alisema Shilogile.
Aliongeza wakati wanamvizia Sheikh Ponda liyechelewa kwenye kongamano hilo likliwa kama dakika 10 limalizike waumini wa kiislam aliodai walikuwa wengi mno walimtorosha na hivyo wao kumkosa na kudai kuwa wanafuatilia mahali alipofichwa na kama ni kweli alijeruhiwa wajue anatibiwa wapi.
Utata unakuja wakati Shilogile akisema hawakufanya tukio lolote la kupiga risasi, je wanafuatilia mahali anapotibiwa kwa sababu zipi? Kadhalika waumini waliozungumza kwa njia ya simu na MICHARAZO wamedai tukio hilo limetokea wakati Polisi walipovamia taksi iliyomleta Sheikh Ponda na katika purukshani walifyatua mabomu ya machozi na risasi za moto ambapo ilimpata begani na kumjeruhi.
"Hawa watu wanatuchokoza Waislam ili tuonekane wakorofi tunasherehekea sikukuu yetu kwa amani wanatuletea mambo ya kihuni walitaka kumkamata Sheikh wetu nasi tukasimamia kidete na kuwagomea ndipo wataamua kutumia nguvu kupiga risasi na kwa bahati ikampiga risasi ya bega na kumjeruhi wanakanusha nini," alisema mmoja wa mashuhuda hao.
Hata hivyo bado imekuwa vigumu kujua mahali alipo sheikh huyo inayedaiwa alikimbizwa Hospitali ya mkoa na kabla ya kuanza kupata matibabu baada ya kubainiwa Polisi wanamfuatiliwa alitoroshwa na waumini hao na kutofahamika kapelekwa hospitali gani kupata matibabu, japo Polisi wanasema wameanza upelelezi wa mahali alipo kupata ukweli wa uvumi huo ambao umesambaa nchi nzima kama moto wa nyikani.
MICHARAZO bado inafuatilia kujua ukweli wa taarifa hizi na kila tukipata habari mpya tutawapenyezea.

No comments:

Post a Comment