STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, August 10, 2013

Polisi Zanzibar watangaza 'bingo' kwa waliowajeruhi Waingereza


 
KAMANDA wa Polisi, Kamishna Musa Ali Musa amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imeahidi kutoa Shilingi milioni 10/= kwa mtu yeyote atakayetoa taarifa zitakazofanikisha kukamatwa kwa watu waliowashambulia mabinti wawili kutoka Londona, Uingereza,  Kirstie Trup na Katie Gee.

Mabinti hao walishambuliwa kwa tindikali usoni, kifuani na mikononi siku ya Jumatano walipokuwa njiani kuelekea kwenye chakula cha jioni.


Kwa sasa raia hao wameshapelekwa kwa Uingereza kwa ajili ya matibabu zaidi huku vyombo vya habari nchini humo vikilitia chumvi tukio hilo kiasi cha kuitia doa Tanzania mbele ya uso wa dunia.

No comments:

Post a Comment