STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, August 10, 2013

Breaking News: Sheikh Ponda kapigwa risasi Morogoro

Sheikh Ponda katika harakati zake za kidini


TAARIFA zilizotufikia muda huu kutoka Morogoro ambazo hata hivyo bado hazijathibitishwa rasmi zinasema kuwa Katibu wa Kutetea Haki za Waislam Tanzania na Sheikh maarufu nchini, Sheikh Ponda Issa Ponda amepigwa risasi.
Habari zilizotumwa kwa njia ya ujumbe mfupi toka mkoani humi zinadai kuwa Sheikh Ponda alipigwa risasi hiyo na wanaodaiwa askari Polisi na kujeruhiwa.
MICHARAZO ilijaribu kuwasiliana na masheikh kadhaa ili kuthjibitisha taarifa hizo, ambapo mmoja wa viongozi wa Baraza la Habari za Vijana la Kiislam (BAHAKITA) Sheikh Sadick Godegode alisema hata yeye kazipata taarifa hizo ila bado anaendelea kuzifuatilia toka Morogoro.
"Ni kweli hata mimi nimezipata taarifa hizo kwamba Sheikh wetu, Ponda Issa Ponda kapigwa risasi ya bega, ila bado hatujathibitisha japo jana alikuwa mmoja wa walihudhuria Baraza la Idd lililofanyika msikiti wa Kichangani," alisema Sheikh Sadick.
Blogu hii inafanya jitihada za kupata ukweli wa taarifa hizo ambazo huenda zisiwe nzuri kwa waumini wa Kiislam ambao wapo katika sherehe za sikukuu ya Eid.

No comments:

Post a Comment