STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, December 25, 2013

Breaking News: James Kisaka is no more

James Kisaka enzi za uhai wake
HABARI zilizotufikia muda mfupi uliopita zinasema kuwa aliyekuwa kocha wa makipa wa Simba, Jamse Kisaka amefariki dunia.
Kisaka aliyewahi kung'ara katika nafasi ya ukipa ndani ya Simba na klabu nyingine alikuwa amelazwa hospitali wiki kadhaa sasa kutokana na kusumbuliwa na ugonjwa wa kupooza na kutoona na aliakuwa akiendelea kuimariksa.
MICHARAZO inaendelea kufuatilia tarataibu za mazishi za kipa huyo nyota wa zamani na kocha aliyejizolea sifa kemkem za ufanisi wa kazi yake.
James Kisaka alizaliwa mwaka 1955 mjini Dar es Salaam na alipata elimu yake ya Msingi katika shule ya Oysterbay na baadaye sekondari za Mzizima na Tambaza, Dar es Salaam pia.

Alianza kupata umaarufu wa soka tangu anasoma na haikushangaza aliposajiliwa na Sigara akiwa nba umri mdogo.

Baadaye alichezea Nyota Nyekundu, Simba kabla ya kwenda Small Simba ya Zanzibar na baadaye Volcano ya Kenya alipokwenda pamoja na Zamoyoni Mogella na Lilla Shomari na kisha kutua Ndovu ya Arusha.
Alikuwemo kwenye kikosi cha Simba kilichokwenda ziara ya mafunzo nchini Brazil mwaka 1981.
Kisaka atakumbukwa kwa upole wake na ufanyaji kazi kwa bidii enzi za uhai wake. 
Mungu aiweke roho ya marehemu mahali pema. Ameen

.

Mtawala amshafisha Rage fedha za Okwi


Mtawala (kushoto) akiteta jambo na Rage

Emmanuel Okwi
ALIYEKUWA Katibu Mkuu wa Klabu ya Simba, Evodius Mtawala, amesema amefurahi kuiacha klabu hiyo ikiwa na rekodi nzuri ya kumfunga mtani wake Yanga mabao 3-1 na kuweka wazi kwamba mwenyekiti wa klabu hiyo, Ismail Aden Rage, hajatafuna fedha za usajili wa mshambuliaji wao wa zamani, Emmanuel Okwi.
Mtawala jana alitangazwa rasmi kuwa Mkurugenzi mpya wa Vyama, Wanachama na Masuala ya Kisheria wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).
Hata hivyo, Mtawala aliweka wazi kwamba Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili na Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Simba, Hanspoppe Zacharia, ndiye mtu anayeidai klabu hiyo kiasi kikubwa cha fedha.
Mtawala alisema yeye na Hanspoppe walikwenda Tunisia kukutana na viongozi wa Klabu ya Etoile du Sahel kuzungumzia malipo ya Dola za Marekani 300,000 za mauzo ya Okwi na hakuna mahali walipoonyesha kwamba kuna kiasi cha fedha walilipwa.
"Kuhusiana na fedha za Okwi, hazijaliwa, hilo hata mimi namtetea," alisema Mtawala.
Kiongozi huyo mpya wa TFF anayeshika nafasi ya Mtemi Ramadhani, alisema katika kipindi cha uongozi wake alijitahidi kulipa madeni mbalimbali yaliyokuwa yanawakabili ili kuendeleza uhusiano mzuri na taasisi walizokuwa wanafanya nazo kazi.
Alisema amefurahi kuona anaiacha Simba ikiwa na rekodi mbili nzuri za kuwafunga Yanga na kuendelea kuwaumiza vichwa viongozi, wanachama na mashabiki wao.
Aliweka wazi kuwa hakutaka kujihusisha na mgogoro wa uongozi ndani ya Simba na alihakikisha timu inaandaliwa vyema ili kupata matokeo mazuri.
"Watanikumbuka, kuna mambo mengi nilikuwa ninamshauri mwenyekiti (Rage) na wajumbe, kama wangenisikiliza, huu mvutano uliopo sasa usingekuwepo," alisema Mtawala.
Alifafanua kuwa, akiwa TFF atahakikisha anatekeleza majukumu yake kwa kufuata taratibu na muongozo kama ilivyoelezwa kwenye katiba ya shirikisho hilo.
Alisema yuko tayari kukabiliana na changamoto mbalimbali kwenye nafasi hiyo mpya na anaahidi kuwa mwadilifu na kufuata misingi ya kazi hiyo.
Mtawala ambaye kitaaluma ni mwanasheria, aliwasilisha barua yake ya kujiuzulu Simba jana Desemba 24.

NIPASHE

Msondo, Sikinde kumaliza ubishi leo TCC-Chang'ombe

Safu ya uimbaji wa Sikinde
Msondo Ngoma wakionyesha makeke yao

MABINGWA na wakongwe wa muziki wa dansi nchini Msondo Ngoma 'Baba ya Muziki' na Mlimani Park Orchestra 'Wana Sikinde' leo mchana watachuana vikali katika viwanja vya TCC Club  Chang’ombe, Temeke.
Mpambano huo wa kusherekea sikukuu ya Krismasi utakuwa wa kufunga mwaka 2013 na pia utaamua ni bendi gani bora kati ya magwiji hao wa muziki wa dansi nchini mwaka huu.
Mratibu wa mchuano huo Joseph Kapinga amesema mpambano huo utaanza saa nane alasiri hadi majogoo.
Kapinga alisema Sikinde wataingia TCC wakitokea Bagamoyo walipokuwa wakipiga kambi wakati kambi ya Msondo Ngoma imebaki kuwa siri kwa muda wote.
Mratibu huyo alisema kila bendi itapiga kwenye jukwaa lake ili kuondoa shaka ya hujuma.
Kapinga alisema kila bendi itatapewa muda wa saa moja kupiga jukwaani kabla ya kuipisha nyingine.
Kiongozi wa Msondo Ngoma, Saidi Mabera alisema jana kuwa watapiga nyimbo zao zote kali ili kuhakikisha wanaibuka kidedea.
Alitaja baadhi ya nyimbo watakazopiga kuwa ni  'Nimuokoe Nani', 'Zarina', 'Mwanaidi', 'Kanjelenjele', 'Bahati', 'Sesilia', 'Usiue Usiibe', 'Asha Mwana Seif', 'Kauka Nikuvae', Chuma Chikoli Moto', 'Kilio cha Mzima', 'Ajali' na  'Suluhu'.
Naye kiongozi wa Sikinde Hamisi Mirambo alijigamba kuwa wataibuka na ushindi mnono.
“Tuna waimbaji wazuri na hakuna itakachotuzuia kushinda,” alisema Mirambo.
Alitaja baadhi ya nyimbo ambazo watazipiga kuwa ni 'Selina', Wikiendi', 'Penzi la Fukara', 'Hiba', 'MV Mapenzi’, 'Supu Umelitia Nazi' na 'Jinamizi la Talaka'.
Pambano limeandaliwa na Bob Entertainment na Keen Arts chini ya udhamini wa Konyagi, gazeti la NIPASHE, CXC Africa na tovuti ya Saluti5.com.