STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, June 23, 2013

Mbunge Sugu amuomba radhi Waziri Mkuu, kisa...!

Mhe Sugu
Waziri Mkuu, Mhe. Pinda
BAADA ya kauli yake iliyoibua mjadala mkubwa nchini dhidi ya Waziri Mkuu, Mhe. Mizengo Pinda kufuatia majibu yake aliyoyatoa wiki iliyopita Bungeni kwa kutaka Polisi kuendelea kuwapiga raia, Mbunge wa Mbeya Mjini, Mhe Joseph Mbilinyi 'Sugu', aomba radhi.
Sugu amemuomba radhi mhe Pinda na watanzania kwa ujumla kwa lugha aliyotumia katika kuonyesha hisia zake juu ya kauli aliyoitoa mhe Pinda bungeni.
Kupitia akaunti yake ya Facebook, Mbunge huyo machachari amenukuliwa akiwaomba radhi Watanzania waliokerwa na kauli yake iliyodai kwamba Tanzania haijawahi kuwapata Waziri Mkuu kama Mhe. Pinda kwa kusema;
"Ndugu watanzania, naombeni radhi kwa tusi nililolitoa kwa mhe Pinda, kwani nilikua nimeghafirika, halikuwa kusudio langu kumtukana mmoja wa viongozi wa nchi."

Kiemba, Sure Boy ndiyo Wanasoka Bora Tanzania 2012

Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah akimpa tuzo ya Mchezaji Bora Chipukizi, Salum Abubakar 'Sure Boy' wa Azam

KIUNGO nyota wa timu ya Simba na Taifa Stars, Amri Kiemba amefanikiwa kutwaa tuzo ya Mwanasoka Bora wa Mwaka wa Tanzania iliyotolewa na Chama cha Wanasoka Tanzania, SPUTANZA, katika hafla iliyofanyika jana kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es salaam.
Kiemba amenyakua tuzo hiyo iliyodhaminiwa na kampuni ya Pepsi kwa ufanisi wake kwa msimu uliopita ambapo amekuwa katika kiwango cha juu akiisaidia kuifungia simba mabao 8 kwa msimu uliopita huku akiibeba Stars katika mechi zake za kimataifa.
Naye kiungo mwenye mapavu ya mbwa, Abubakar Salum 'Sure Boy' alinyakuwa tuzo ya Mwanasoka Bora Chipukizi, tuzo ambayo alistahili kutokana na umahiri wa mchezaji huyo anayeichezea Azam na Taifa Stars.
Wengine walionyakua tuzo katika hafla hiyo ni kipa wa Mtibwa, Hussein Sharrif 'Casillas' aliyekuwa Kipa Bora wa Mwaka na kocha Mecky Mexime wa Mtibwa.
MICHARAZO inawapa pongezi wote waliotwaa tuzo hizo na kuwatakia mafanikio mema, kadhalika inawapa heko SPUTANZA na wadhamini wa tuzo hiyo ya kwanza kuandaliwa na chama hicho.

Orodha nyingine ya Form 6 wanaotrakiwa kwenda JKT



JESHI LA KUJENGA TAIFA (JKT) LINAWATANGAZIA VIJANA WALIOMALIZA KIDATO CHA SITA 2013 NA KUCHAGULIWA KUJIUNGA NA JKT KATIKA MAKAMBI YA RUVU PWANI, MGAMBO TANGA, MSANGE TABORA, BULOMBORA KIGOMA, MARAMBA TANGA, RWAMKOMA MARA, MLALE RUVUMA NA KANEMBWA KIGOMA KURIPOTI KATIKA MAKAMBI HAYO TAREHE 24 JUNI 2013 KAMA ILIVYOTANGAZWA AWALI.

VIJANA HAO WARIPOTI KATIKA MAKAMBI WALIYOPANGIWA KAMA ILIVYOONYESHA KATIKA TOVUTI YA JKT WWW.JKT.GO.TZ. 

ATAKAYERIPOTI KAMBI AMBAYO HAKUPANGIWA HATAPOKELEWA. VIJANA HAO WALIPOTI WAKIWA NA VYETI VYA LEAVING VYA KIDATO CHA NNE AU CHA SITA KWA UTHIBITISHO.

INASISITIZWA KUWA KUJIUNGA NA JKT KWA MUJIBU WA SHERIA NI LAZIMA, ATAKAYESHINDWA KURIPOTI ATAKUWA AMEVUNJA SHERIA NA ATACHUKULIWA HATUA ZA KISHERIA

VIJANA WATUNZE TIKETI ZAO WALIZOTUMIA KWENDA KATIKA MAKAMBI YA JKT. NAULI ZAO ZITAREJESHWA NA JKT WATAKAPORIPOTI KAMBINI.

VIJANA WALIOCHAGULIWA KATIKA AWAMU YA PILI NI WALE WALIOFAULU KWA DIVISION I, II NA BAADHI YA DIVISION III MCHEPUO WA SAYANSI.

VIJANA WA KIDATO CHA SITA 2013 AMBAO MAJINA YAO HAYAKUORODHESHWA KATIKA TOVUTI HIYO, WATAJIUNGA NA JKT AWAMU YA TATU MWEZI SEPTEMBA 2013.



Kwa taarifa zaidi (imenukuliwa kutoka): JKT.go.tz

bulombora.pdf
File Size: 826 kb
File Type: pdf
Download File


kanembwa.pdf
File Size: 674 kb
File Type: pdf
Download File


maramba.pdf
File Size: 342 kb
File Type: pdf
Download File


mgambo.pdf
File Size: 810 kb
File Type: pdf
Download File


mlale.pdf
File Size: 729 kb
File Type: pdf
Download File


msange.pdf
File Size: 1262 kb
File Type: pdf
Download File


ruvu.pdf
File Size: 903 kb
File Type: pdf
Download File


rwamkoma.pdf
File Size: 569 kb
File Type: pdf
Download File

Zola D aachia za zamani

Zola D katika pozi
MKALI wa miondoko ya Hip Hop nchini, David Michael 'Zola D', ameachia 'audio' za nyimbo zake za zamani baada ya kuombwa na mashabiki wake.
Zola D alisema nyimbo hizo zilizoachiwa video zake na kufanya mashabiki kutaka kusikia 'audio' ni zile zilizorekodiwa kati ya mwaka 2007 mpaka mwaka juzi na tayari baadhi zipo kwenye mitandao ya kijamii.
"Nimeachia 'audio' za nyimbo kama tano hivi za zamani ukiwemo nilioimba na Baby Madaha baada ya kuombwa na mashabiki waliotaka kuusikia baada ya kuiona video yake, " alisema.
Zola D alisema kwa sasa baada ya kutoka kwenye misiba ya wasanii wenzake, Albert Mangweha aliyewahi kuimba naye wimbo na Langa Kileo anajipanga kutoa kazi mpya kwa mashabiki na kufuatiwa na albamu kamili itakayokuwa na jumla ya nyimbo 21.

MAAJABU: HII NDIYO KAZI YA UUMBAJI YA MUNGU


Maajabu  ya  uumbaji  yamemfanya  mama  mzazi  wa  Xiao Wei  ambaye  ni  mchina amwage  machozi  akiomba  msaada  wa  kunusuru  maisha  ya  mwanae   mwenye  umri  wa  miezi  7 aliyezaliwa  na  makalio  matatu...
Kalio  la  tatu  lipo  kama  mkia  mfupi, wenye  urefu  wa   sentimita  8  ( 8 cm ), katikati  ya  makalio  mengine  mawili.
Akiongea   kwa  uchungu, mama  mzazi  wa  mtoto  huyo  amedai  kuwa  kwa  muda  mrefu  amekuwa  akiwaomba  madaktari  wafanye  upasuaji  wa  tako  hilo  lakini  wao  wamekuwa  wakimjibu   kuwa  hiyo  si  kazi  nyepesi  kama  anavyodhani....
"Tukilikata  litaota  tena, hivyo  hatutakiwi  kukurupuka  na  badala  yake  tutakiwa  kupata  muda  wa  kupitia  vitu  vingi  ukiwemo  mrija  wa  uti  wa  mgongo  ambapo  kalio  hilo  limejiegesha"...Alisema  daktari  mmoja  akimjibu  mama  huyo.
 

Una tatizo la nguvu za kiume au za kike? Soma hapa!

KITABU AMBACHO KINATOA TIBA ZA UKOSEFU WA NGUVU ZA KIUME NA KIKE KWA KUTUMIA VYAKULA VYA ASILI IKIWEMO MATUNDA NA MBOGA MBOGA ZA MAJANI SASA KIPO MITAANI KINAPATIKANA MITAA YA UHURU NA MSIMBAZI KWA MAHITAJI YA KITABU HIKI NA DAWA MBALIMBALI ZA KUTIBU MARADHI PAMOJA NA MATATIZO PIGA SIMU  0787406938

Vumbi awataka Choki, Asha Baraka kumaliza tofauti zao

Ally Choki

Asha Baraka

Alain Dekula Kahanga 'Vumbi'
MWANAMUZIKI wa zamani wa bendi ya Marquiz Original, Alain Dekula 'Vumbi' anayefanya shughuli zake za muziki nchini Sweden, amewasihi wakurugenzi wa bendi za Extra Bongo, Ally Choki na mwenzake wa African Stars 'Twanga Pepeta' Asha Baraka kumaliza tofauti zao.
Vumbi alisema amekuwa akifuatiliwa malumbano baina ya wakurugenzi hao kupitia mitandao ya kijamii na kushangazwa kusikia wawili hao wakiapiana kutozikana wala kuhudhuria mazishi ya mwenzake akidai hadhani ni jambo zuri au lenye tija kwa muziki wa Tanzania.
Mcharaza gitaa la solo huyo, alisema ni vyema wawili hao wakaa chini na kumaliza tofauti zao kwa masilahi ya muziki wa Tanzania ambao alidai bado una kazi pevu kuweza kujitangaza nje ya mipaka ya Tanzania kama alivyoutangaza marehemu Dk Remmy na kundi la Tatu Nane.
"Sifurahishwi na uhasama unaoendelea baina ya Asha Baraka na Ally Choki, ningependa wakae chini na kuzika tofauti zao kwa masilahi ya muziki wa Tanzania, malumbano kati ya makundi siyo jambo jipya, lakini haikuwahi kufikia watu kukataliana kuzikana," alisema Vumbi.
Vumbi alisema anafahamu 'bifu' za kisanii hufanywa kokote duniani kwa lengo la kuongeza soko na kuvuna mashabiki, lakini siyo kama uhasama uliopo baina ya watu hao wawili ambao ni moja ya mihimili mikubwa ya muziki wa dansi Tanzania kwa kusaidia ajira ya watu wengi.
"Naomba unifikishie salamu zangu wakae chini na kusameheana kama kuna tatizo baina yao, ili kusaidia dansi lizidi kusonga mbele, malumbano na 'bifu' zitumike kuinua soko la muziki na sio  kuwekeana kinyongo kama ninachosikia na kukisoma mitandaoni," alisema.
Kauli ya Vumbi imekuja baada ya wakurugenzi hao kunukuliwa wakiapiana kwamba 'hawapendani' na katu mmoja wao asihudhurie wala kumzika mwenzake akitangulia kufa kutokana na kutofautiana mara baada ya kuachana kufanya kazi sehemu moja.
Choki alikuwa mmoja wa wanamuziki wa Twanga Pepeta akiingia na kutoka kabla ya kuanzisha Extra Bongo ambayo imekuwa ikiwanyakua wanamuziki toka kwa wapinzani wao hao, huku yeye akifikishwa mahakamani akidai gari analodai alipewa kwa makubaliano.

MASHALI, MIYEYUSHO WAJIFUA KUWAVAA WAKENYA


Francis Miyeyusho (kulia) akimtupia konde Thomas Mashali wakati wa mazoezi jana

  Miyeyusho akijifua kumkabili bondia Shadrack Machanje kutoka Kenya.
  Mashali akipasha tayari kuzipiga na bondia Patrick Amote wa Kenya.
Mabondia hao katika pozi la kuzipiga wakati wa mazoezi ya jana Francis Miyeyusho (kulia) akimtupia konde Thomas Mashali wakati wa mazoezi jana
 Mashali (kushoto) akikwepa konde la Miyeyusho. ---
 Mabondia wa hapa nchini Thomas Mashali na Francis Miyeyusho Jana wamefanya mazoezi ya pamoja katika gym iliyopo Kijitonyama jijini Dar es Salaam. Mabondia hao wanajiandaa kuwakabili wenzao kutoka Kenya ambao ni Patrick Amote na Shadrack Muchenje kwenye Tamasha la Usiku wa Matumaini litakalofanyika Julai 7 mwaka huu katika Uwanja wa Taifa jijini Dar.PICHA NA MUSA MATEJA / GPL

Ommy Lax, PNC kupotezea videoni

Ommy Lax
MSANII anayekuja juu kwenye muziki wa kizazi kipya Iman Omar 'Ommy Lax' anajiandaa kurekodi video ya wimbo wake mpya uitwao 'Wapotezee' alioimba na mkali wa Watanashati, PNC.
Akizungumza na MICHARAZO, Ommy Lax alisema kuwa maandalizi ya kuanza kurekodi video hiyo imekamilika na kwamba zoezi hilo litafanyika wiki hii katika maeneo mbalimbali ya jijini Dar es Salaam.
Ommy Lax alisema kuwa 'audio' wa kibao hicho tayari imeanza kurushwa hewani na ameona ni vyema kukata kiu ya mashabiki wake kwa kuwatengenezea video ili waone kwa ukamilifu ujumbe wa wimbo huo.
"Baada ya kuachia 'audio' kwa sasa nafanya maandalizi ya kurekodi video ya wimbo wangu uitwao 'Wapotezee' ambao nimeimba kwa kumshirikisha PNC, nimepanga kurekodi wiki ijayo ili niisambaze mapema," alisema Ommy Lax.
Hicho ni kibao kingine toka kwa msanii huyo ambaye anatamba na wimbo wa Kioo Changu alioimba na Matonya 'Tonya Business'.

Miaka 13 ya Kikosi ilikuwa noumaa, Kalapina afunika, Chid ndani ya nyumba


 Chid Benz akikonga nyoyo za mashabiki wake wakati wa shoo ya Kikosi cha Mizinga kutimiza miaka 13 iliyofanyika katika ukumbi wa New Msasani jijini Dar es salaam. (Picha zote na Habari Mseto Blog).
 Chid Benz
 Fukuda akichana mistari
 Katibu wa CUF, Julius Mtatiro ambaye alikuwa mgeni rasmi  akizungumza wakati wa shoo maalumkundi la muziki wa Hip Hop la Kikosi cha Mizinga kutimiza miaka 13.
Baadhi ya watu waliotoa mchango mkuwa kwa wasanii wa Kikosi cha Mizinga walipewa vyeti, hapa mwandishi Joseph Zablon akionesha cheti chake baada ya kukabidhiwa ba mgeni rasmi. 
 Mwakilishi wa Clouds Radio akipokea cheti.
   
 Kala Pina 'Nabii Koko' akitumbuiza
 
 Afande Sele akipagawisha  mashabiki.