STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, June 23, 2013

Zola D aachia za zamani

Zola D katika pozi
MKALI wa miondoko ya Hip Hop nchini, David Michael 'Zola D', ameachia 'audio' za nyimbo zake za zamani baada ya kuombwa na mashabiki wake.
Zola D alisema nyimbo hizo zilizoachiwa video zake na kufanya mashabiki kutaka kusikia 'audio' ni zile zilizorekodiwa kati ya mwaka 2007 mpaka mwaka juzi na tayari baadhi zipo kwenye mitandao ya kijamii.
"Nimeachia 'audio' za nyimbo kama tano hivi za zamani ukiwemo nilioimba na Baby Madaha baada ya kuombwa na mashabiki waliotaka kuusikia baada ya kuiona video yake, " alisema.
Zola D alisema kwa sasa baada ya kutoka kwenye misiba ya wasanii wenzake, Albert Mangweha aliyewahi kuimba naye wimbo na Langa Kileo anajipanga kutoa kazi mpya kwa mashabiki na kufuatiwa na albamu kamili itakayokuwa na jumla ya nyimbo 21.

No comments:

Post a Comment