STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 6, 2012

Afande Sele arudi na roho yake



MSANII nyota wa muziki wa kizazi kipya nchini, Seleman Msindi 'Afande Sele', amefyatua wimbo mpya uitwao NItarudi na Roho Yangu wakati akijiandaa kuiachia mtaani albamu yake ya tano.
Akizungumza na MICHARAZO kwa njia ya simu toka mjini Morogoro, Afande Sele, alisema kibao hicho kipya amefyatua kwa kushirikiana na Abbas Hamis '20 Percent' ikiwa ni miezi kadhaa tangu atangulize kibao cha 'Maskini Hafulii'
Afande, alisema kibao hicho kama ilivyo nyimbo zake zote kipo katika miondoko ya hip hop na ni utambulisho wa albamu yake mpya ambayo alipanga kuitoa mwaka jana, lakini alisita na kuamua kuitoa mwaka huu.
"Wakati najiandaa kuitoa hadharani albamu yangu ya tano tangu nijitose kwenye fani hii iitwayo 'Kingdom' ambayo itakuwa na jumla ya nyimbo 14 badala ya 10 nilizopanga kutoa awali," alisema.
Alizitaja nyimbo za albamu hiyo iliyowashirikisha wasanii mbalimbali nyota nchini ni; 'Kingdom', 'Maskini Hafulii', 'Soma Ule', 'Machozi ya Suzy', 'Nguvu' na Akili', 'Dume' na 'Nikupendeje'.
Albamu nne za mwanzo za mkali huyo ambaye pia ni Mfalme wa Rhymes ni 'Mkuki Moyoni' ya mwaka 2001, 'Darubini Kali' (2004), 'Nafsi ya Mtu' (2006) na 'Karata Dume' ya mwaka 2008.

Mwisho

1 comment:

  1. naomba link kama naweza kuupata tafadhali nautafuta sana tafadhali

    ReplyDelete