STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 6, 2012

BFT yateua 25 kushiriki kozi ya kimataifa ya ukocha

SHIRIKISHO la Ngumi za Ridhaa Tanzania, BFT, limetangaza majina ya makocha 25 walioteuliwa kushiriki kozi ya kimataifa ya mchezoitakayofanyika kati ya Januari 16-24.
Awali kozi hiyo ilipangwa kufanyika Novemba mwaka jana ikishirikisha makocha 30, lakini ilikwama kutokana na mkufunzi wa kimataifa toka Algeria aliyekuwa aiendeshe kushindwa kuwasili na kufanya BFT kuwapunguza washiriki watano safari hii.
Taarifa ya BFT inasema imewapunguza makocha hao watano kutokana na agizo la TOC linalosimamia kozi hiyo kufuatia hasara iliyopata awali wakati wa maandalizi ya awali ambayo hata hivyo haikufanyika.
Katibu wa BFT, Makore Mashaga, alisema idadi hiyo ya makocha hata hivyo inaweza kupunguzwa kulingana na bajeti iliyopo ambayo itawagharamia washiriki mwanzo mwisho katika kozi hiyo.
Mashaga aliwataja washiriki hao kuwa ni Rajabu Mhamila 'Super D', Anord Ngumbi,
Moses Lema, Anthon Mwang'onda na Edward Emmanuel kutoka Dar es Salaam, Yahya Mvuvi (Tabora), Joseph Mayanga na Zakaria Mwaseba wote wa Morogoro.
Wengine ni Omari Saady na Mussa Bakari (Mwanza), Ally Ndee (JKT-Mbeya), Emilio Moyo na Gaudence Uyaga (Pwani) Juma Lisso (Magereza-Kigoma), Lyinda Kalinga (Dodoma) na Abdallah Bakar (Tanga).
Washiriki wengine ni Mohammed Hashim (Polisi Dar es Salaam), Haji Abdallah, Said Omar na David Yombayomba (JWTZ), Mazimbo Ally, Rogated Damian na Fatuma Milanzi (JKT), Musa Maisori na Hamisi Shaaban (Magereza Dar es Salaam).
Katibu huyo alisema kozi hiyo itakayofanyika kwenye majengo ya Shule ya Sekondari Filbert Bayi, Kibaha-Pwani itaendeshwa na mkufunzi wa kimataifa Josef Diouf kutoka Shirikisho la Dunia la mchezo huo, AIBA atakayeshirikiana na Makamu wa Rais wa BFT, Michael Changarawe.

Mwisho

No comments:

Post a Comment