STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 6, 2012

Idd Azan ajitosa kuisaidia Villa Squad




MBUNGE wa Jimbo la Kinondoni, Idd Azan naye amejitosa kuiokoa timu ya Ligi Kuu Tanzania Bara, Villa Squad ambayo ipo katika hali mbaya kiuchumi kwa lengo la kuona inafanya vema katika duru lijalo la ligi hiyo litakaloanza wiki mbili zijazo.
Azan, aliyewahi kuwa Mwenyekiti wa Chama cha Soka wilayani humo, KIFA na kile cha mkoa wa Dar es Salaam, DRFA, amejitolea kuigharamia timu hiyo posho za wachezaji wanaojifua ufukweni pamoja na kulipoa gym ya kuwajengea stamina.
Kaimu Katibu Mkuu wa Villa, Frank Mchaki alisema licha ya kwamba Mbunge huyo amekuwa akijitolea mara kwa mara kuipiga tafu timu yao, lakini safari hii ameonyesha dhamira yake ya kutaka kuona Villa haishuki daraja kwa kuigharamia mazoezi.
Mchaki alisema uongozi wao umefarijika na itikio la viongozi na wadau wa soka wilaya ya Kinondoni wanavyojitolea kuisaidia timu yao, akiahudi kwamba misaada wanayotoa haitapotea bure kwani watahakikisha timu hiyo haishuki daraja msimu huu.
"Bada ya DC wa Kinondoni, Jordan Rugimbana kuahidi kutuingiza kambini wiki ijayo, naye Mbunge wa Jimbo hilo, Idd Azan amejitolea kuigharamia timu yetu mazoezi ya kuwapa stamina wachezaji na tunawashukuru mno kwa misaada yao," alisema Mchaki.
Aliongeza kutoa wito kwa wadau wengine wajitokeze zaidi kuisaidia timu hiyo akidai kuporomoka kwa Villa Squad kutaifanya wilaya yao ya Kinondoni kukosa timu za Ligi Kuu kama ilivyokuwa misimu kadhaa iliyopita baada ya kutowekwa kwa Twiga Sports na kushuka daraja kwa Villa ilipopanda daraja msimu wa 2008-2009.
Mchaki alisema, kujitokeza kwa viongozi hao wakuu wa Kinondoni na wadau wengine kunawapa moyo wachezaji wao ambao walikuwa katika hali ngumu kutokana na Villa kukabiliwa na hali mbaya ya ukata.

Mwisho

No comments:

Post a Comment