STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 6, 2012

Msondo kugawa zawadi Zenji




MASHABIKI wa bendi ya Msondo Ngoma wa visiwani Zanzibar wanatarajiwa kushindanishwa kuimba na kucheza nyimbo na miondoko ya bendi hiyo katika kuwania zawadi mbalimbali kama shamrashamra za kusherehekea miaka 48 ya Mapinduzi.
Zawadi hizo ikiwemo fulana, kanda za kaseti na cd za albamu za bendi hiyo kongwe, zitatolewa kwa mashabiki watakaomudu kuimba na kucheza vema nyimbo za Msondo katika onyesho maalum litakalofanyika wiki ijayo visiwani humo.
Shindano la mashabiki hao wa Msondo litafanyika kwenye ukumbi wa Gym Khan, wakati bendi hiyo itakapotumbuiza kuadhimisha miaka 48 ya Mapinduzi ambayo yatafikia kilele chake Alhamis ijayo.
Makamu Mwenyekiti wa Maseneta wa Msondo, ambaye ndiye mratibu wa onyesho hilo, Wazir Dewa, aliiambia MICHARAZO kwamba wameamua kuwaandalia mashabiki wao zawadi hizo kama njia ya kuwashukuru kwa ushirikiano wanaipa bendi yao.
Dewa alisema, pia wanawapelekea zawadi hizo mashabiki hao katika kuungana nao kusherehekea Mapinduzi ya Zanzibar yaliyofanyika Januari 12, 1964.
"Tumewaandalia zawadi mbalimbali mashabiki wetu wa Msondo watakashiriki kwenye onyesho letu ambapo tutawashindanisha kucheza na kuimba nyimbo za bendi hiyo na watakaofanya vema watatunukiwa fulani, cd na kanda za kaseti," alisema.
Aliongeza, kwamba licha ya kupambanishwa, pia mashabiki hao watapata fursa ya kupigiwa nyimbo za zamani zilizoifanya bendi hiyo kuwa 'Baba ya Muziki' nchini.
***

No comments:

Post a Comment