STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 6, 2012

Margareth Somy afyatua mpya za Injili



BAADA ya kimya kirefu tangu alipoachia albamu yake iliyofanya vema sokoni ya 'Tenda Wema', muimbaji wa muziki wa Injili ambaye pia ni muigizaji wa filamu, Margareth Somy, ameanza maandalizi ya kupakua albamu yake ya pili.
Akizungumza na MICHARAZO, Somy, alisema albamu hiyo ya pili mpya itafahamika kwa jina la Yesu Ndiye Maarufu na itakuwa na jumla ya nyimbo nane.
Somy alizitaja nyimbo ambazo zimeshaanza kurekodiwa kwa ajili ya albamu hiyo ni 'Yesu Ndiye Maarufu', 'Jerusalem', 'Nitainua Macho Yangu' na 'Yatima'.
"Nimeanza kurekodi nyimbo za albamu yangu mpya itakayokuwa ya pili, ambayo nimepanga kuitoa ndani ya mwaka huu," alisema Somy.
Somy alisema nyimbo nyingine za kujazia albamu hiyo ameshaziandikia mashairi yake ingawa hajazipa majina, hadi atakapozirekodi," alisema.
Muimbaji huyo, ambaye kitaaluma ni muuguzi akifanya kazi katika hospitali moja iliyopo Ilala-Bungoni, jijini Dar es Salaam, alisema anadhani kabla ya Juni albamu hiyo itakuwa sokoni, ingawa anatarajia kusambaza baadhi ya nyimbo ili zianze kusikika mapema.
Alisema wakati akianza kusambaza nyimbo hizo ataingia mzigoni kufyatua video zake ili mashabiki wake wapate uhondo kupitia kwenye vituo vya runinga.

No comments:

Post a Comment