STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 6, 2012

Hassanal ajitosa Bongo Movie




MBUNIFU maarufu wa mitindo na mavazi nchini, Mustafa Hassanali, amejitosa kwenye fani ya uigizaji wa filamu za Kibongo baada ya kushirikishwa ndani ya filamu mpya iitwayo 'Glamour' inayotarajiwa kuachiwa hivi karibuni.
Hassanal amecheza filamu hiyo inayohusiana na masuala ya mapenzi na kijamii, pamoja na wakali wa fani hiyo kama Tecla Mjata.
Mbali na Mjata wengine waliopo ndani ya kazi hiyo ambayo ni miongoni mwa kazi mpya zinazotarajiwa kufungulia mwaka mpya wa 2012 kwa filamu za Kibongo ni' Eva Isaac, Edward Chogula, Amitabh Aurora na wengineo.
Wasambazaji wa filamu za Kibongo, wametoa taarifa kwamba tofauti na watu wanavyomchukulia Hassanal kwamba ni mkali wa ubunifu wa mavazi na mitindo, katika filamu hiyo ya Glamour ameonyesha uwezo wa hali juu kuthibitisha kuwa ana vipaji vingi.
"Huwezi amini kama aliyecheza ndani ya filamu hiyo ni Hassanal aliyezoeleka kwenye masuala ya ubunifu wa mitindo na mavazi, ni kazi inayotarajiwa kuachiwa hivi karibuni na kampuni yetu kwa ajili ya kuunza mwaka mpya wa 2012," alisema taarifa hizo inasomeka hivyo.
Mbali na filamu hiyo nyingine zinazotarajiwa kuachiwa mwezi huu ni 'My Son', 'I Hate My Birthday', 'DNA' na nyinginezo.

No comments:

Post a Comment