STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 6, 2012

Kicheko Hawezi Kulala videoni


Picha:Kicheko


MCHEKESHAJI maarufu nchini anayetamba katika kipindi cha Ze Comedy Show, Rogers Richard 'Massawe Mtata' ameuweka wimbo wake mpya wa 'Kulala Siwezi' kwenye video huku akijiandaa kupakua albamu yake binafsi ya tatu itakayokuwa na nyimbo nane.
Akizungumza na MICHARAZO, msanii huyo ambaye hufahamika kama Kicheko, alisema video ya kibao hicho kilichoanza kurushwa hewani wiki hii, imerekodiwa na kampuni yake ya Kausha Production yenye makao yake eneo la Magomeni, Dar es Salaam.
Kicheko, alisema kwa sasa video hiyo inafanya uhariri kabla ya kuanza kusambazwa kwenye vituo vya runinga ili kuanza kurushwa hewani, wakati akiendelea kumalizia nyimbo nyingine za albamu yake mpya ya tatu aliyopanga kuitoa mwaka huu.
"Baada ya kusambaza kibao changu cha Kulala Siwezi, nimekamilisha kufyatua video yake ambayo inahaririwa kwa sasa, nadhani hadi wiki ijayo nitaanza kuisambaza ili irushwe hewani wakati nikiendelea kurekodi nyimbo nyingine," alisema.
Kicheko alisema albamu yake hiyo mpya itakuwa na nyimbo nane na atashirikiana na wasanii kadhaa nyota nchini, na itakuwa katika miondoko aliyoibuni iitwayo 'Bongo Tecno'.
Hiyo itakuwa ni albamu ya tatu kwa msanii huyo, aliyewahi kutamba na kundi la Kidedea lililorushwa michezo yake hewani kupitia kiyuo cha ITV baada ya awali kufyatua 'Say Ye' au 'Unanipenda Mimi' na 'Mirinda Nyeusi' iliyofahamika pia kama 'Kicheko.com'.
Kicheko alisema amepania ndani ya mwaka huu wa 2012 kuweza kufanya mambo matatu kwa mkupuo, kuchekesha, kufanya muziki na filamu kudhihirisha vipaji alivyojaliwa.
***

No comments:

Post a Comment