STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, October 22, 2013

Kuiona Twiga Stars, Msiumbiji Buku tu, TFF yamlilia Mhango


Na Boniface Wambura
KIINGILIO cha chini kwenye mechi ya wanawake chini ya miaka 20 katika ya Tanzania na Msumbiji itakayochezwa Jumamosi (Oktoba 26 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kitakuwa sh. 1,000.

Mechi hiyo itachezwa kuanzia saa 10 kamili jioni, na kiingilio hicho ni kwa ajili ya viti vya rangi ya kijani, bluu na chungwa. Viingilio vingine ni sh. 2,000 kwa VIP C, sh. 5,000 kwa VIP B wakati VIP A itakuwa sh. 10,000.

Timu ya Msumbiji inatarajiwa kuwasili nchini kesho (Oktoba 23 mwaka huu) saa 8 kamili mchana kwa ndege ya LAM. Msumbiji yenye msafara wa watu 25 itafikia kwenye hoteli ya Sapphire.
***
UCHAGUZI TPL BOARD KUFANYIKA IJUMAA
Uchaguzi wa Bodi ya Ligi Tanzania (TPL Board) utafanyika Oktoba 25 mwaka huu kwenye ukumbi wa mikutano uliopo Golden Jubilee Tower.
Kwa mujibu wa Kamati ya Uchaguzi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) wajumbe wanaounda Mkutano wa Uchaguzi ni wenyeviti kutoka klabu 24 za Ligi Daraja la Kwanza (FDL), na 14 wa klabu za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL).

Wagombea kwenye uchaguzi huo ni Hamad Yahya Juma (Mwenyekiti), Said Muhammad Said Abeid (Makamu Mwenyekiti) wakati wanaoumba ujumbe wa Kamati ya Uendeshaji ni Khatib Omari Mwindadi na Kazimoto Muzo.
 ***
RAMBIRAMBI MSIBA WA JIMMY MHANGO
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko taarifa za kifo cha mjumbe wa Bodi ya klabu ya Ashanti United, Jimmy Mhango kilichotokea jana (Oktoba 21 mwaka huu).

Msiba huo ni mkubwa kwa wadau wa mpira wa miguu kwani Mhango aliutumikia mpira wa miguu kwa muda mrefu, tangu akiwa mchezaji, kocha na baadaye kiongozi.

Kabla ya kuingia kwenye Bodi ya Ashanti United, enzi za uchezaji wake alichezea timu za Mapinduzi ya Dodoma, Ushirika ya Moshi na Pan African ya Dar es Salaam. Pia aliwahi kuwa Kocha Mkuu wa Ashanti United.

TFF inatoa pole kwa familia ya marehemu Mhango, klabu ya Ashanti United na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA), na kuwataka kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba huo mzito.

Maziko yamefanyika leo mchana katika makaburi ya Abeid (Mchikichini) Dar es Salaam. Mungu aiweke roho ya marehemu Mhango mahali pema peponi. Amina.

Makamu wa Rais awaongoza waombolezaji kuuaga mwili wa Julius Nyaisangah


  Sehemu ya Wanakamati wa Kamati ya maziko....
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akitia saini katika Kitabu cha maombolezo ya Kifo cha aliyewahi kuwa mtangazaji wa Redio Tanzania, ITV na Redio One na Redio Aboud, marehemu Julius Nyaisanga, aliyefariki dunia mwishoni mwa wiki iliyopita huko mjini Morogoro kutokana na kusumbuliwa na ugonjwa wa shinikizo la damu. Marehemu Nyaisanya ameagwa leo katika viwanja vya Leaders Club Kinondoni na anasafirishwa leo hii kuelekea Tarime kwa ajili ya maziko.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akitoa heshima za mwisho mbele ya jeneza lenye mwili wa aliyewahi kuwa mtangazaji wa Redio Tanzania, ITV na Redio One na Redio Aboud, marehemu Julius Nyaisanga, aliyefariki dunia mwishoni mwa wiki iliyopita huko mjini Morogoro kutokana na kusumbuliwa na ugonjwa wa shinikizo la damu. Marehemu Nyaisanya ameagwa leo katika viwanja vya Leaders Club Kinondoni na anasafirishwa leo hii kuelekea Tarime kwa ajili ya maziko.
 Leah Nyaisanga, ambaye ni mke wa marehemu wa aliyewahi kuwa mtangazaji wa Redio Tanzania, ITV na Redio One na Redio Aboud, marehemu Julius Nyaisanga, akitoa heshima za mwisho mbele ya jeneza lenye mwili wa marehemu mumewe, aliyefariki dunia mwishoni mwa wiki iliyopita huko mjini Morogoro kutokana na kusumbuliwa na ugonjwa wa shinikizo la damu, wakati wa shughuli za kuagwa mwili huo zilizofanyika kwenye viwanja vya Leaders Club Kinondoni na anasafirishwa leo hii kuelekea Tarime kwa ajili ya maziko.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimfariji mfiwa Leah Nyaisanga, ambaye ni mke wa marehemu wa aliyewahi kuwa mtangazaji wa Redio Tanzania, ITV na Redio One na Redio Aboud, marehemu Julius Nyaisanga, aliyefariki dunia mwishoni mwa wiki iliyopita huko mjini Morogoro kutokana na kusumbuliwa na ugonjwa wa shinikizo la damu. Marehemu Nyaisanya ameagwa leo katika viwanja vya Leaders Club Kinondoni na anasafirishwa leo hii kuelekea Tarime kwa ajili ya maziko.
Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri, Absalom Kibanda akisema machache
Menyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP  Dkt. Reginald Mengi, akizungumza machache....
 Mwenyekiti wa Chadema na Mbunge wa Hai, Freeman Mbowe akisema machache
Makamu wa Rais, Dkt. Bilal, akizungumza kutoka salam za rambirambi kwa wafiwa.
  Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri, Absalom Kibanda (kulia) akiteta jambo na Mwenyekiti wa Chadema na Mbunge wa Hai, Freeman Mbowe, wakati wa shughuli hiyo Viwanja vya Leaders.
 Sehemu ya waombolezaji waliojitokeza kumuaga marehemu Nyaisanga, katika Viwanja vya Leaders Club.
 Sehemu ya waombolezaji waliojitokeza kumuaga marehemu Nyaisanga, katika Viwanja vya Leaders Club. Picha Zote na Ofisi ya Makamu wa Rais

Kamanda Kombe hatunaye duniani

Picture:  James Kombe, SACP
James Kombe
Na Frank Geofray-Jeshi la Polisi.
ALIYEKUWA kuwa Kamanda wa Polisi Kikosi cha usalama barabarani, Kamishna Msaidizi Mwandamizi (SACP) mstaafu James Kombe amefariki dunia wakati akipatiwa matibabu katika hospitali ya Ocean Road jijini Dar es Salaam.

Akizungumzia kifo hicho Msemaji wa Jeshi la Polisi Nchini, Mrakibu Mwandamizi wa Polisi (SSP) Advera Senso alisema, 
Kombe alifariki Oktoba 22 mwaka huu na taratibu za mazishi  zinaendelea.

Aidha Senso alisema Marehemu Kombe alizaliwa mwaka 1950 huko Mwika mkoani Kilimanjaro na alijiunga na Jeshi la Polisi tarehe 15 mwezi machi mwaka 1970 baada ya kuhitimu elimu ya sekondari mwaka 1969 nchini Uganda ambapo alipandishwa vyeo na kupewa madaraka mbalimbali.

Baadhi ya vyeo alivyopitia na miaka ya kupata vyeo hivyo katika mabano ni pamoja na Sagenti wa Polisi (1973) Mkaguzi Msaidizi wa Polisi (1977), Mkaguzi wa Polisi (1984), Mrakibu Msaidizi (1986), Mrakibu wa Polisi(1991), Mrakibu Mwandamizi (1995), Kamishna Msaidizi wa Polisi (1998) na Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (2002) hadi alipostaafu mwaka 2010.

Baadhi ya nafasi alizowahi kuzitumikia katika Jeshi la Polisi ni pamoja na kuwa Mkuu wa Polisi wa Wilaya (OCD) katika wilaya za Dodoma, Tarime, Serengeti na Arusha pamoja na Kuwa Mkuu wa Polisi wa Mkoa (RPC) katika mikoa ya Lindi, Arusha, Kigoma pamoja na Mkuu wa Kikosi cha Kutuliza ghasia Tanzania na hadi anastaafu alikuwa mkuu wa kikosi cha Usalama barabarani Tanzania.

Watatu wafa katika ajali Ruaha

AJALI hii imetokea jana maeneo ya kona za Ruaha ukiwa mwanzo mwanzo kuelekea Iringa, Kwa mujibu wa vyanzo vya habari hii vilidai kuwa ni watu watatu walikufa na kati yao mmoja alifariki papo hapo chanzo mwendo wa kasi wa dereva wa basi ktk kuovateki na
ghafla akakutana na lori lililoharibi katika kona.

Simba kurejea kileleni kesho, Yanga kuvuna nini kwa Rhion Rangers

Yanga inayodaiwa baadhi ya wachezaji kesho wakawekwa benchi baada ya sare ya 3-3 ma Simba
Simba iliyolazimisha sare na Yanga Jumapili
Coastal Union watakaivaa Simba kesho Mkwakwani

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjfKSZcZys5ESjlNhn6Du0VkOqGFVkb8gUCv3UzZirPkcebsNYfANbRVhAOAl1OqftHcSm5puEpVqo5axdm__Ah1pbye4T7d3Eg-l_zw18-_m9V3fncdtkMQFlUkVN689pvjUj0mNOjNsc/s1600/TIMU+YA+RHINO.JPG
Vijana wa Rhino Rangers watakaoivaa Yanga Taifa
BAADA ya kulazimisha sare ya maajabu ya 3-3 na watani zao Yanga, Simba kesho itakuwa na kibarua cha kutaka kurejea kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara watakapoikabili Coastal Unioni nyumbani kwao.
Pambano hilo la Wagosi wa Kaya na Wekundu wa Msimbazi litakalofanyika kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani Tanga ni kati yua mapambano matatu yatakayochezwa kesho katika mfululizo wa ligi hiyo.
Simba yenye pointi 19 iwapo itaikwangua Coastal ambayo imerejea jijini humo ikitoka kupoteza mechi mbili mfululizo, itakwea kileleni na kuziondoa Azam na Mbeya City zenye pointi 20 kila mmoja.
Hata hivyo Simba haipaswi kuchukulia kirahisi mchezo huo wa kesho kutokana na ukweli Coastal ipo nyumbani na isingependa kufanywa asusa kwa mara ya tatu tena katika ligi hiyo.
Simba iliyotua salama jijini humo ikiwa imewaacha baadhi ya nyota wake kwa sababu mbalimbali wakiwemo Abdulhalim Humud 'Gaucho' na Haruna Chanongo waliopewa adhabu ya kujiunga na timu ya vijana, itakuwa na kazi kubwa ya kusaka ushindi kwa Wagosi wa Kaya.
Mbali na mechi hiyo, mabingwa watetezi Yanga wenyewe watakuwa dimba la Taifa kupepetana na Rhino Rangers katika pambano linalotarajiwa kuwa gumu kutokana na maafande hao wa JWTZ kufanya vibaya hivi karibuni.
Ushindi wowote kwa Yanga utawafanya wafikishe pointi 19 na kuendelea kusalia kwenye nafasi yake ya nne, japo inategemea na matokeo ya mechi nyingine inayochezwa hiyo kesho kati ya Kagera Sugar na Prisons-Mbeya.
Iwapo Yanga itazembea katika mechi hiyo ya Rhino kama ilivyofanywa ilipocheza na Simba, kisha Kagera ikashinda mchezo huo wa ugenini basi inaweza kuwang'oa mabingwa hao watetezi katika nafasi hiyo.
Kagera yenyewe ina pointi 14 na kama itailaza Prisons itafikisha pointi 17, japo hakuna anayeamini Yanga kama itakubali kufa kwa Rhino Rangers.
Kocha wa Yanga Ernie Brandts amenukuliwa na mtandao wa klabu yake kwamba amesikitishwa sana na sare dhidi ya Yanga na kwamba anajipanga kwa ajili ya mechi ya kesho akiamini vijana wake hawatamuangusha tena.

Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara 2013-2014      
                                  P    W   D   L    F    A   GD   PTS
1.   Azam                   10   5    5   0   15   6    9     20
2.  Mbeya City           10   5    5   0   13   7   6     20
3.  Simba                     9    5    4    0   20  8  12    19
4.  Yanga                     9    4    4    1   18  11  7    16
5. Mtibwa Sugar        10   4    4    2   16  12  4    16
6.  Ruvu Shooting       10   4    3    3    12   9   3    15
7. Kagera Sugar          9    4    2    3    10   7   3    14
8.  JKT Ruvu              10   4    0    6     9   11 -2   12
9.  Coastal Union         9    2    5    2     7    6    1   11
10.Ashanti                  10   2    3    5    10  19 -9     9
11.Rhino Rangers        9    1     4    4     8   12 -4     7
12.Prisons                   9     1    4    4     5    12 -7    7
13. Oljoro                  10    1    3    6     8    16 -8    6
14.Mgambo               10    1    2    7     3    18 -15  5
 
Wafungaji:

8- Tambwe Amisi (Simba)
7- Elias Maguri (Ruvu Shooting), Juma Luizio ( Mtibwa Sugar)
5- Tumba Sued (Ashanti Utd), Hamis Kiiza (Yanga)
4-
Didier Kavumbagu (Yanga), Peter Michael (Prisons), Kipre Tchetche (Azam),
3- Jerry Tegete, Mrisho Ngassa (Yanga), Haruna Chanongo, Jonas Mkude (Simba), Bakar Kondo (JKT Ruvu), Themi Felix (Kagera), Paul Nonga (Mbeya City), Salum Machaku (JKT Ruvu), Jerry Santo (Coastal Union),
2- Haruna Moshi (Coastal Union), Saady Kipanga (Rhino Rangers), Mwagani Yeya, Jeremiah John (Mbeya City), Godfrey Wambura (Kagera Sugar), Shaibu Nayopa, Amir Omary (JKT Oljoro), Khamis Mcha (Azam), Shaaban Nditti (Mtibwa Sugar), Betram Mombeki (Simba)

Ticha auwawa kwa risasi akiwaokoa wanafuzni wake

http://l1.yimg.com/bt/api/res/1.2/6U.OXapeIcyKY7TLvn4VUA--/YXBwaWQ9eW5ld3M7Zmk9ZmlsbDtoPTY4MjtweW9mZj0wO3E9NzU7dz05NjA-/http://media.zenfs.com/en_us/News/ap_webfeeds/65fc60ba808adb23400f6a706700c0c6.jpg
SPARKS, Nev. (AP) — Students at a Nevada middle school were filing off buses and reuniting with friends on the playground after a weeklong vacation when the pop of gunfire shattered the morning calm. Children fled the campus for their lives before the first bell rang.

Police said a Sparks Middle School student was the lone gunman who injured two young classmates, killed himself and took the life of an 8th-grade math teacher who tried to stop the rampage. 


The teacher, former serviceman Michael Landsberry, 45, was being hailed for trying to protect students from a shooting that was witnessed by 20 or 30 children.

"We have a lot of heroes today, including our children ... and our fallen hero, an amazing teacher," Washoe County School District Superintendent Pedro Martinez said.

Authorities did not provide a motive for the shooting, and it's not known where he got the gun. The 12-year-old wounded students were listed in stable condition. One was shot in the shoulder, and the other was hit in the abdomen.

http://l2.yimg.com/bt/api/res/1.2/ejj3UbfEwLugOAHSMaAoEg--/YXBwaWQ9eW5ld3M7Zmk9ZmlsbDtoPTYzNztweW9mZj0wO3E9NzU7dz05NjA-/http://media.zenfs.com/en_us/News/ap_webfeeds/223f6d7b8053da23400f6a706700a7f7.jpgParents clung to their teary-eyed children at an evacuation center, while the community struggled to make sense of the latest episode of schoolyard violence to rock the nation less than a year after the massacre in Newtown, Conn. Sparks, a city of roughly 90,000 that sprung out of the railway industry, lies just east of Reno.

"It's not supposed to happen here," said Chanda Landsberry, the slain teacher's sister-in-law. "We're just Sparks — little Sparks, Nevada. It's unreal."

Investigators were still trying to piece together the chain of events that began around 7:15 a.m. Monday, 15 minutes before classes were set to begin for roughly 700 students in the 7th and 8th grades.

"As you can imagine, the best description is chaos," Reno Deputy Police Chief Tom Robinson said. "It's too early to say whether he was targeting people or going on an indiscriminate shooting spree."

It was no shock to family members that Landsberry — a married military veteran with two stepdaughters — would take a bullet.

"To hear that he was trying to stop that is not surprising by any means," said Chanda Landsberry. She added his life could be summed up by his love of family, his students and his country.

On his school website, Michael Landsberry posted a picture of a brown bear and took on a tough-love tone, telling students, "I have one classroom rule and it is very simple: 'Thou Shall Not Annoy Mr. L.'"

"The kids loved him," Chanda Landsberry said.

Sparks Mayor Geno Martini said Landsberry served two tours in Afghanistan with the Nevada National Guard and was well known in the school community.

"He proudly served his country and was proudly defending the students at his school," he said. The mayor praised the quick response from law officers who arrived at the scene within 3 minutes of the initial 911 calls to find the gunman with a self-inflicted gunshot wound to the head.

"They got it under control very quickly and shut down the scene," said Martini, who urged listeners on a local radio station hours after the shooting to be sure all guns in their homes are locked away safely.

"I couldn't understand how this kid got a gun," he said. "I'm sure his parents didn't give it to him."

Students from the middle school and neighboring elementary school were evacuated to the nearby high school, and classes were canceled. The middle school will remain closed for the week along with an adjacent elementary school.

"We came flying down here to get our kids," said Mike Fiorica, who came to the evacuation center to meet up with his nephew, a Sparks Middle school student. "You can imagine how parents are feeling. You don't know if your kid's OK."

The violence erupted nearly a year after a gunman horrified the nation by opening fire in Sandy Hook Elementary School in Newtown, Conn., leaving 26 dead. The Dec. 14 shooting ignited debate over how best to protect the nation's schools and whether armed teachers should be part of that equation.

The Washoe County School District, which oversees Sparks Middle School, held a session in the spring in light of the Connecticut tragedy to educate parents on what safety measures the district takes.

The district has its own 38-officer police department. No officers were on campus at the time of the shooting.

 

Associated Press writer Michelle Rindels in Las Vegas and news researcher Rhonda Shafner in New York City contributed to this report.

Hivi ndivyo wakzzi Dar walivyojitokeza kumuaga Uncle J

 Msafara wa Magari ambao moja wapo (la mbele) likiwa limebeba jeneza lenye mwili wa marehemu Julius Nyaisanga ukiingia kwenye viwanja vya leaders muda huu kwaajili ya wakazi wa jiji la Dar kuweza kutoa heshima zao za mwisho kwa Mwili wa Marehemu Julius Nyaisanga kabla ya Kusafirisha Kwao Tarime Mkoani Mara

Baadhi ya Ndugu, Jamaa na marafiki wakibeba jeneza lenye Mwili wa Marehemu Julius Nyaisanga Kwaajili ya kupeleka sehemu husika tayari kwa kutoa heshima za mwisho kwa wakazi wa jiji la Dar waliofika katika viwanja vya leaders muda huu
Sehemu Jeneza lenye Mwili wa Marehemu Julius Nyaisanga litakapowekwa kwaajili ya wakazi wa jiji la dar kuweza kutoa heshima zao za mwisho kabla ya kusafirishwa kwenda Tarime Mkoani Mara
 Baadhi ya wakazi wa jiji la dar waliojitokeza katika viwanja vya leaders muda huu
Baadhi ya Wakazi wa Jiji la Dar wakisubiria Kutoa Heshima zao za Mwisho kwa Mwili wa Marehemu Julius Nyaisanga Kabla haujasafirishwa kupelekwa Kwao Tarime Mkoani Mara.Picha zote na Josephat Lukaza wa Lukaza blog

Wafuasi wa Sheikh Ponda kidedea


Sheikh Ponda Issa Ponda katika harakati zake

MAHAKAMA Kuu Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam imewaachia huru watu 52 wanaodaiwa kuwa wafuasi wa Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Ponda Issa Ponda, baada ya kuona kwamba sheria ilikosewa kwa kuwafunga kifungo cha mwaka mmoja.
Mahakama hiyo imesema kuwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ilipaswa kuwahukumu kifungo cha miezi mitatu tu.

Uamuzi huo ulitolewa jana na Jaji Salvatory Bongole baada ya kusikiliza hoja za rufaa iliyokatwa na wafuasi hao kupitia wakili wa utetezi, Mohammed Tibanyendera.

“Mahakama hii imeona kwamba washtakiwa kukutwa na hatia ya kosa la kula njama adhabu yake siyo sahihi, nimeifutilia mbali, lakini nakubaliana na kosa la pili na la tatu wana hatia,” alisema na kuongeza:

“Adhabu ya mwaka mmoja mliyopewa naibatilisha, mtakwenda jela miezi mitatu kama sheria ya Jeshi la Polisi inavyosema au faini Shilingi  50,000.”

Jaji Bongole alisema washtakiwa hao walihukumiwa kwenda jela kutumikia kifungo cha mwaka mmoja Machi 21, 2013 mpaka sasa wametumikia zaidi ya miezi mitatu.
“Kwa kuwa wameshatumikia zaidi ya miezi mitatu, natamka kwamba nawaachia huru wote, kwa sababu adhabu yenu mmeitumikia na zaidi,” alisema Jaji Bongole.

Jaji Bongole alisema washtakiwa waliotiwa hatiani na kufungwa mwaka mmoja jela kwa makosa ya kula njama, kufanya mkusanyiko usio halali na kukaidi amri ya Polisi iliyokuwa ikiwazuia kufanya maandamano kuelekea katika Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) kushinikiza Sheikh Ponda kuachiwa kwa dhamana ni Salum Makame na wenzake 51.

“Warufani mlipewa adhabu mbili katika kosa moja, mtu anapokula njama na kuiba, akitiwa hatiani kwa kosa la kuiba, kosa la kula njama linakufa,” alisema Jaji Bongole na kuongeza:

“Adhabu mliyopewa kwa kosa la kula njama na kukaidi amri ya Polisi haikuwa sahihi, kosa la pili nilipopitia ushahidi limethibitishwa kwamba mliandamana kwa kukaidi amri ya RPC (Kamanda wa Polisi wa Mkoa) iliyowakataza  kufanyahivyo.

“Kosa la pili na tatu nakubaliana na uamuzi wa Mahakama ya Kisutu uliowatia hatiani, kifungu namba 46 cha sheria za Polisi kilichotakiwa kutumika kuwapa adhabu hakikutumika, kifungu hicho kinatamka adhabu kwa makosa hayo ni kwenda jela miezi mitatu au faini ya Sh. 50,000.

“Kutiwa hatiani kwa kosa la kula njama na adhabu yake siyo sahihi, nimeifutilia mbali, kosa la pili na tatu nakubaliana na kutiwa hatiani, adhabu ya mwaka mmoja mliyopewa naibatilisha, mtakwenda jela miezi mitatu kama sheria ya Polisi inavyosema au faini Sh. 50,000.”

Jaji alisema: “Mlifungwa Machi 21, 2013 na Hakimu Mkazi Sundi Fimbo, mpaka sasa ni zaidi ya miezi mitatu, natamka kwamba nawaachia huru wote, mtoke gerezani sababu adhabu yenu mmeitumikia zaidi.”

Wafuasi hao walidaiwa kufanya maandamano Februari 15, mwaka huu wakishinikiza Sheikh Ponda kuachiwa kwa dhamana katika kesi ya uchochezi iliyokuwa ikimkabili katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mbele ya Hakimu Victoria Nongwa.

Machi 21, mwaka huu, Mahakama hiyo iliwahukumu kwenda jela mwaka mmoja kwa makosa hayo matatu waliyokuwa wakikabiliwa likiwamo la kukaidi amri ya Polisi iliyokuwa ikiwazuia kufanya maandamano kuelekea kwa DPP ili kushinikiza kiongozi wao apewe dhamana.

Akisoma hukumu hiyo, Hakimu Fimbo alisema kuwa katika shtaka la kula njama upande wa mashtaka ulithibitisha bila kuacha shaka kwamba washtakiwa walikutana, wakakubaliana kufanya maandamano hivyo mahakama inawatia hatiani kwa kosa hilo.

Katika shtaka la kukusanyika na kuandamana, alisema mahakama inawatia hatiani.

Kuhusu kosa la kukaidi amri halali ya polisi alisema mahakama inawatia hatiani kwa kuwa  washtakiwa walipeleka maombi ya kufanya maandamano ya amani na Polisi waliyazuia kwa sababu hawakuwa na askari wa kutosha, lakini maandamano hayo yalifanyika baada ya kutoka msikitini.

Katika kosa la kwanza aliwahukumu washitakiwa kwenda jela mwaka mmoja. Katika shtaka la pili pia aliwahukumu mwaka mmoja jela huku kosa la tatu wakihukumiwa tena kifungo cha mwaka mmoja jela.

Hakimu Fimbo alisema adhabu hizo zinatumikiwa kwa pamoja hivyo aliwahukumu washtakiwa kifungo cha mwaka mmoja jela kila mmoja.
 

CHANZO: NIPASHE

Mmoja afa, wawili wakijeruhiwa kwa risasi



MTU mmoja amefariki baada ya kupigwa risasi kifuani na mwingine kujeruhiwa mikono yote miwili baada ya watu wasiojulikana kuwavamia na kutaka kuwapora mali huko Manyoni, Singida.

Tukio hilo limetokea katika Kijiji cha Igwamadete Kata ya Iseke Tarafa ya Nkonko wilayani humo baada ya mtu aliyejulikana kwa jina la Alody Joshua, 29 kupigwa risasi na majambazi hao.
 
Kadhalika Daudi Azaliwa amejeruhiwa mikono yote miwili baada ya kupigwa risasi na majambazi hao wakati wakitoka kwenye mnada wa Mpapa kuelekea nyumbani ndipo majambazi hao walipoanza kuwapiga na kuwanyanganya fedha na kusababisha  kifo cha mtu huyo.

Jeshi la Polisi-Manyoni limethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kufafanua kuwa watu watatu wanashilikiwa kwa tuhuma za kuhusika na tukio hilo na kwamba wanatarajiwa kufikishwa mahakamani baada ya upelelzi kukamilika.
 
Chanzo Blog ya Singida.

Gaucho, Vialli waitwa Znz Heroes, Cannavaro, Morris watemwa


 
KIKOSI cha wachezaji 30 cha timu ya taifa ya Zanzibar (Zanzibar Heroes) kimetangazwa na kocha mkuu wa timu hiyo Salum Bahusi bila ya jina la nahodha wa Yanga, Nadir Haroub 'Cannavaro' na Aggrey Morris wa Azam.

Kwa mujibu wa habari kutoka Zanzibar, kikosi hicho ambacho kinatarajiwa kushiriki Kombe la Chalenji kuanzia Novemba 27 mwaka huu jijini Nairobi Kenya, Kocha wa Zanzibar Heroes, Bausi amesema kikosi hicho kitaingia kambini Oktoba 27 mwaka huu na kesho Jumatano wachezaji wote walioitwa watafanyiwa vipimo.

Kikosi kamili kilichoitwa na Bausi ni; MAKIPA ni Mwadini Ali (Azam), Abdallah Rashidi (Ruvu Shooting), Ali Suleiman (KMKM).

MABEKI ni Mohamed Azan (Polisi), Waziri Salum (Azam), Shafi Hassan (Malindi), Mohamed Faki (Zimamoto), Salum Haji (Miembeni), Said Yussuf (Mtende), Mohamed Othman (Jamhuri), Mussa Said (Chwaka Stars), Nassor Masoud ‘Chollo’ kutoka Simba.

VIUNGO ni Abdulhalim Humud 'Gaucho' (Simba), Sabri Ali (JKT Oljoro), Adeyum Saleh (Simba), Isihaka Othman (JKU), Ali Kani (JKT Oljoro), Hamad Mshamata (Chuoni), Suleiman Hamad (Miembeni), Awadh Juma na Masoud Ali wote wa Mtibwa Sugar.

WASHAMBULIAJI ni Seif Karihe (Azam), Suleiman Kasim Selembe (Coastal Union), Khamis Mcha 'Vialli' (Azam), Amour Omary (Miembeni), Amir Hamad (JKT Oljoro), Jaku Joma (Mafunzo), Faki Nahoda (Kimbunga), Hassan Seif (Mtibwa Sugar), Juma Ali Yussuf wa New Generation.

Rais Kikwete alilia Uncle J, kuagwa leo

Rais Jakaya Kikwete
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete amemtumia Salamu za Rambirambi Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Mheshimiwa Dkt. Fenella Mukangara kufuatia kifo cha Mtangazaji Mkongwe hapa nchini na aliyekuwa Mkurugenzi wa Abood Media inayomiliki Kituo cha Televisheni cha Abood, Bwana Julius Nyaisanga maarufu kwa jina la Uncle J. Nyaisanga.

Bwana Nyaisanga aliyewahi kufanya kazi Radio Tanzania Dar es Salaam (RTD) ambayo hivi sasa ni TBC Taifa, na katika
Kampuni ya IPP Media ambako alikuwa Mkurugenzi wa Radio One, alifariki dunia tarehe 20 Oktoba, 2013 katika Hospitali ya Mazimbu iliyoko katika Manispaa ya Morogoro alikopelekwa kupatiwa matibabu ya ugonjwa wa kisukari.

“Nimeshtushwa, nimesikitishwa na kuhuzunishwa kutokana na kifo cha Mtangazaji Maarufu na Mkongwe hapa nchini katika Tasnia ya Habari hususan upande wa Utangazaji, Bwana Julius Nyaisanga kwani kuondoka kwake kumeacha pengo kubwa katika Tasnia hiyo”, amesema Rais Kikwete katika Salamu zake.

Rais Kikwete amesema alimfahamu Marehemu Julius Nyaisanga enzi za uhai wake kama Mtangazaji aliyekuwa na bidii kubwa ya kazi na mwenye sauti iliyokuwa na mvuto mkubwa kwa wasikilizaji katika sehemu zote alizowahi kufanyia kazi.

“Kwa hakika mchango wa Marehemu Julius Nyaisanga kwa maendeleo ya Taifa letu kupitia Utangazaji, ni mkubwa na wa kupigiwa mfano ambao sote kama Taifa hatuna budi kujivunia”, ameongeza kusema Rais Kikwete katika Salamu zake.

“Kutokana na msiba huu mkubwa, ninakutumia wewe Waziri wa Habari,  Utamaduni na Michezo, Mheshimiwa Dkt. Fenella Mukangara Salamu zangu za Rambirambi kwa kumpoteza mmoja wa Watangazaji Maarufu na Wakongwe hapa nchini. Aidha kupitia kwako naomba unifikishie Salamu zangu za Rambirambi na pole nyingi kwa Familia ya Marehemu Julius Nyaisanga kwa kuondokewa na Mhimili na Kiongozi wa Familia”.

Rais Kikwete amewahakikishia Wanafamilia, ndugu na jamaa wa Marehemu kuwa yuko pamoja nao katika kuomboleza msiba huu mkubwa. Amewaomba wawe na moyo wa uvumilivu na subira wakati huu wanapopita katika kipindi kigumu cha kuomboleza kifo cha mpendwa wao. Namuomba Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema aipokee na kuilaza mahala pema peponi Roho ya Marehemu Julius Nyaisanga.

Vilevile Rais Kikwete ametoa pole kwa Waandishi wa Habari  na Watangazaji kote nchini kwa kumpoteza Mwanataaluma mwenzao ambaye kwa hakika kuondoka kwake kumesababisha pengo kubwa katika Taaluma ya Uandishi wa Habari na Utangazaji hapa nchini.

“Kutokana na juhudi alizokuwa nazo Marehemu, Waandishi wa Habari na Watangazaji kote nchini hawana budi kuiga mfano wake na kuendeleza yote mazuri aliyoyafanya kwa maendeleo ya nchi yetu na Taifa letu kwa ujumla”, amemalizia Salamu zake za Rambirambi Rais Kikwete.

Imetolewa na:

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
21 Oktoba, 2013

Visome vyuo 10 vilivyofutwa na serikali

Naibu Waziri wa Elimu, Phillip Mulugo

SERIKALI kupitia Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi imekunjua makucha yake kwa kutangaza kuvifuta vyuo 10 ambavyo havikusajiliwa na Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) .

Naibu Waziri wa wizara hiyo, Philip Mulugo, alitoa kauli hiyo jijini Dar es Salaama mbele ya Kamati ya Bunge ya Huduma za Jamii na kuongeza kuwa kufutwa kwa vyuo hivyo ni kutokana na kutokufuata utaratibu wa kusajiliwa.

Alivitaja vyuo hivyo ni Media and Research Center, Vision Hotel and Tourism College, East Africa College of Hospitality and Tourism, The Africa Institute of Business Management na Aspiration Training Center, vyote vya Dar es Salaam.

Vingine ni Dar es Salaam School of Hair Design, Media and Values Training Institute na Information Technology Training Center vya Dar es Salaam. Pia alikitaja Chuo cha Morogoro School of Medical Sciences cha Morogoro.

Katika hatua nyingine, Mulugo alikiri kuwa kuna upungufu katika kutoa mikopo kwa wanafunzi wa vyuo vikuu kupitia bodi ya mikopo.

Alisema kuna changamoto nyingi zinazoikabili bodi hiyo zikiwamo urejeshwaji wa mikopo kwa wanafunzi waliomaliza chuo, mfumo wa utoaji wa mikopo, ufinyu wa bajeti na makosa yanayotokana na wanafunzi kukosea kujaza fomu za mikopo.