STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, October 22, 2013

Gaucho, Vialli waitwa Znz Heroes, Cannavaro, Morris watemwa


 
KIKOSI cha wachezaji 30 cha timu ya taifa ya Zanzibar (Zanzibar Heroes) kimetangazwa na kocha mkuu wa timu hiyo Salum Bahusi bila ya jina la nahodha wa Yanga, Nadir Haroub 'Cannavaro' na Aggrey Morris wa Azam.

Kwa mujibu wa habari kutoka Zanzibar, kikosi hicho ambacho kinatarajiwa kushiriki Kombe la Chalenji kuanzia Novemba 27 mwaka huu jijini Nairobi Kenya, Kocha wa Zanzibar Heroes, Bausi amesema kikosi hicho kitaingia kambini Oktoba 27 mwaka huu na kesho Jumatano wachezaji wote walioitwa watafanyiwa vipimo.

Kikosi kamili kilichoitwa na Bausi ni; MAKIPA ni Mwadini Ali (Azam), Abdallah Rashidi (Ruvu Shooting), Ali Suleiman (KMKM).

MABEKI ni Mohamed Azan (Polisi), Waziri Salum (Azam), Shafi Hassan (Malindi), Mohamed Faki (Zimamoto), Salum Haji (Miembeni), Said Yussuf (Mtende), Mohamed Othman (Jamhuri), Mussa Said (Chwaka Stars), Nassor Masoud ‘Chollo’ kutoka Simba.

VIUNGO ni Abdulhalim Humud 'Gaucho' (Simba), Sabri Ali (JKT Oljoro), Adeyum Saleh (Simba), Isihaka Othman (JKU), Ali Kani (JKT Oljoro), Hamad Mshamata (Chuoni), Suleiman Hamad (Miembeni), Awadh Juma na Masoud Ali wote wa Mtibwa Sugar.

WASHAMBULIAJI ni Seif Karihe (Azam), Suleiman Kasim Selembe (Coastal Union), Khamis Mcha 'Vialli' (Azam), Amour Omary (Miembeni), Amir Hamad (JKT Oljoro), Jaku Joma (Mafunzo), Faki Nahoda (Kimbunga), Hassan Seif (Mtibwa Sugar), Juma Ali Yussuf wa New Generation.

No comments:

Post a Comment