STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, October 10, 2013

Eid El Hajj kusherehekewa J'5 BAKWATA watoa taarifa


HATA hivyo wakati BAKWATA wakitoa taarifa hiyo ni kwamba kwa wale wanaofuata mwezi muandamo wa kimataifa ni kwamba Waislam watafunga Arafah kuwaunga mkono mahujaji siku ya Jumatatu na kuisherehekea sikukuu Jumanne itakayokuwa Oktoba 15, yaani siku moja kabla ya ile iliyotangazwa na BAKWATA.
Funga ya Arafah ni muhimu kwa waumini wa kiislam ambao hawakubahatika kwenda Hijja kwani kwa mujibu wa mafundisho ya Mtume Muhammad (SAW) kufunga Swawm siku ya 'Arafah kwa sababu ni kufutiwa madhambi ya miaka miwili; mwaka uliopita na baada yake (Hadiyth katika Swahiyh Muslim).
Hivyo MICHARAZO inawakumbusha waumini wa dini hiyo kutoisahau swaumu hiyo, japo tumesisitizwa kufunga tangu Mfungo tatu unapoingia katika makundi ya mwanzoni, lakini kwa wale walioshindwa kutekeleza ibada hiyo shime wasiiache Arafah kwa manufaa yao ya kidunia na Ahera Inshallah

Minziro:Msituchonganishe Yanga



Wachezaji wa Yanga wakishuka, mbele ni Mbuyu Twite wakishuka uwanja wa Ndege Bukoba
Nizar Khalfani nae yupo kwenye kikosi
Wachezaji wakiendelea kushuka kwenye ndege
Tayari wamekanyaga Ardhi ya Bukoba
Kama kawaida: kushoto ni Khalfan Ngassa kulia ni Niyonzima
Picha ya Pamoja Viongozi na wachezaji
Dida kushoto akipata picha ya pamoja na wenzake
Kocha mkuu wa timu ya Yanga
Asante tumefika salama kazi ni moja ...ushindi ni muhimu Kaitaba
Niyonzima akiwa na Mdau wake wa bukobasports.com
Kelvin Yondani akifurahia baada ya kutua Bukoba asubuhi hii.

Bw. Jamal kalumuna kushoto akiwa na kiongozi wa Yanga
Smart Hotel
Wachezaji wakiingia Smart Hotel
Bw. Ernest Nyambo na Jamal Kalumuna wadau wakubwa wa Yanga Bukoba. (Picha: Lenzi ya Michezo)
KOCHA Msaidizi wa Yanga, Fred Felix Minziro amewajia juu baadhi ya waandishi wa habari na kuwaambia 'msituchonganishe'.
Minziro alitoa kauli hiyo alipoigiwa simu na MICHARAZO kujua msafara mzima wa timu yao kuelekea Bukoba kuumana na Kagera Sugar siku ya Jumamosi na iwapo kama walimjumuisha beki wa kati Kelvin Yondani aliyeripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari kwamba alikirofichana na kocha mkuu, Ernie Brandts kiasi cha kuvua jezi na kutupa chini kisha kususia mazoezi.
Kocha huyo, nyota wa zamani wa Yanga na Taifa Stars, alisema hakuna tukio lolote lililotokea baina ya Yondani na kocha mkuu na ndiyo maana mchezaji huyo yupo kwenye msafara wa wachezaji 21 kwa ajili ya kuivaa Kagera Sugar kwenye uwanja wa Kaitaba.
"Ndugu yangu huyo aliyekuambia kwamba Yondani kagombana na kocha ana yake, na ningependa kuwaambia wazi Yanga hatutaki mtuchonganishe, tupo shwari na hivi sasa tumetua Bukoba salama," alisema Minziro.
Alisema Yondani ni miongoni mwa wachezaji 21 wa Yanga walioenda Bukoba kuhakikish Yanga itaibuka na ushindi dhidi ya wenyeji wao ambao anakiri huwa wasumbufu kwenye dimba lao la nyumbani.
"Msitugombanishe kabisa, tupo shwari tayari kwa kuisulubu Kagera, tumekuja kusaka ushindi huku hivyo tuacheni," alisisitiza Minziro.
Alidokeza kuwa kwa maandalizi waliyofanya dhidi ya mchezo huo ana imani kubwa ya kuibuka na ushindi Jumamosi licha ya kutarajia upinzani mkali wa wenyeji wao hao walkiowatungua katika mechi kama hiyo ya msimu uliopita iliyochezwa Oktoba 8, 2012 ambapo Yanga walilala kwa bao 1-0.

P Square kutua Bongo na wasanii 13

Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania, Kelvin Twissa,(kulia) akisisitiza jambo katika mkutano wake leo na wanahabari kuhusu ujio wa P Square. Kushoto ni Mtangazaji, Hillary Daud 'Zembwela'.
WASANII mapacha kutoka Nigeria, Peter na Paul Okoye, watatumbuiza kwenye viwanja vya Leaders Club jijini Dar es Salaam ambapo wanaletwa na East Africa Radio na TV chini ya udhamini wa Vodacom Tanzania.
Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika katika Hoteli ya Hyatt jijini Dar, mtangazaji wa kituo hicho, Hillary Daudi maarufu kama Zembwela alisema show hiyo itakuwa ya aina yake.
“Wote tunatambua namna kundi hili linavyofanya vizuri ndani na nje ya bara la Afrika, licha ya kutoa burudani kwa mashabiki, pia litatoa fursa kwa wasanii wa ndani kujifunza kutoka kwa wasanii hawa vijana ambao wamepata mafanikio makubwa kutokana na kazi yao ya muziki,” alisema.
“Hii itakuwa ni fursa ya kipekee kwa wasanii wetu wa Bongo kujifunza kwa kuangalia wenzao wanavyofanya kazi.”Kwa upande wake Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania, Kelvin Twissa, alisema Vodacom inafurahi kuendelea kuwa sehemu ya kutoa burudani kwa jamii ya Watanzania na safari hii ikiwaleta wasanii ambao ni kipenzi cha Watanzania wengi.
“Siku zote Vodacom imeendelea kuwa chaguo la kwanza kwa Watanzania, kuanzia katika burudani na hata huduma nyingine za mawasiliano na kijamii. Tunaendelea kuunga jitihada za kuwainua wasanii wetu wa ndani kwa kuwapatia fursa ya kujifunza kutoka kwa wasanii wenzao wakubwa waliofanyikiwa kufanya kazi zao Kimataifa,” alisema.
“Kwa wateja wa Vodacom ambao pia ni mashabiki wa wasanii hawa ambao wanatamba na kibao chao kitamu cha ‘Personally’ kwa sasa wanayo fursa ya kufurahia nyimbo hizi kwa kuzidownload au kuzitumia kama miito ya simu (RBT) na kuweza kujishindia tiketi za onesho hilo. Natoa wito kwa Watanzania wapenda burudani kutembelea ukurasa wetu wa Facebook na Twitter kwa taarifa zaidi na kujua namna ya kujishindia tiketi za onesho hilo.”

Henry, Redondo, Baba Ubaya kuwakosa Prisons

Henry Joseph



Redondo



NYOTA watatu wa Simba, Issa Rashid 'Baba Ubaya', Henry Joseph na Ramadhani Chombo 'Redondo' wamefahamika hawatakuwepo kwenye pambano kati ya timu yao na Prisons-Mbeya siku ya Jumamosi.
Baba Ubaya atalikosa pambano hilo kwa sababu ya kuwa majeruhi sawa na ilivyo kwa kiungo mkabaji Abdallah Seseme na beki wa pembeni Miraj Adam waliovishwa POP.
Henry na Redondo watakosekana katika mechi hiyo kutokana na kuenguliwa kwenye kambi ya timu hiyo iliyopo Bamba Beach, Kigamboni.
Kwa mujibu wa Afisa Habari wa Simba, Ezekiel Kamwaga ni kwamba klabu yao imekuwa na utaratibu wa kuingia kambini kila wanapokabiliwa na mechi na wachezaji wanaofanya vyema kwenye mechi iliyopita na mazoezini ndiyo hujumuishwa kambini kutokana na mapendekezo ya makocha.
Kamwaga alisema hivyo kwa mtazamo wa makocha wao, Henry na Redondo hawakuwaridhisha na ndiyo maana wameungana na makinda wengine waliosajiliwa katika kikosi hicho kutoitwa kambini.
"Huu ni utaratibu wa kawaida na umekuwa ukitumiwa tangu alipokuwepo kocha Patrick Liewig, huwa nasema Simba ya sasa ni 'Simba-LUKU', yaani kadri unavyonunua umeme ndivyo utakavyoutumia na wachezaji kadri wanavyofanya vyema ndivyo wanavyopimwa na makocha," alisema.
Kamwaga alisema hajaelewa ni kwa nini  baadhi ya vyombo vya habari vimeliona tukio la kutoitwa kambini kwa akina Redondo na Henry kuwa kitu cha ajabu wakati ni utaratibu uliopo siku zote Simba.
"Klabu imesajili wachezaji 36 wakiwamo wale wa U20, na kambini huingia wachezaji 25 hasa wanaofanya vyema na kushawishi makocha, hivyo kuachwa kwa akina Henry na Redondo sidhani kama ni issue kubwa wakati msimu uliopita tulikuwa tunaingia kambini bila akina Boban, Kazimoto na watu hawakusema lolote," alisema Kamwaga.
Simba ina kibarua kigumu mbele ya Prisons ambayo imeonyesha kuzinduka hivi sasa ili kuweza kulinda nafasi yao kileleni kwani tayari inapumuliwa na timu za Azam na Mbeya City na iwapo itateleza na Yanga kushinda Kagera siku ya Jumamosi inaweza kuwaengua katika nafasi hiyo.
Mechi nyingine kwa wikiendi hii ni zile zitakazochezwa Jumapili kwa Ashanti kuvaana na Coastal Union kenye uwanja wa Chamazi, Ruvu Shooting kuvaana na Rhino Rangers uwanja wa Mabatini-Mlandizi, Mgambo JKT kujiuliza kwa Mbeya City jijini Tanga, Azam kuwaalika JKT Ruvu kwenye uwanja wa Taifa wakati Mtibvwa itapepetana na Oljoro JKT kwenye mashamba ya Miwa ya Manungu Turiani Morogoro.

Kibadeni kupasua la rohoni kesho Msimbazi


Kocha wa Simba  Abdallah Kibadeni akiwa kwenye mazoezi ya timu hiyo
KOCHA Mkuu wa klabu ya Simba, Abdallah Kibadeni kesho anatarajiwa kuteta na wanahabari kuweka mambo sawa juu ya kinachoendelea katika kambi ya klabu yake pamoja na maandalizi yao dhidi ya mchezo wao na Prisons-Mbeya utakaochezwa Jumamosi kwenye uwanja wa Taifa.
Akizungumza na MICHARAZO, Kibadeni alisema amelazimika kuitisha mkutano huo kutokana na baadhi ya magazeti kuripoti taarifa 'mbaya' dhidi ya kambi yake na benchi nzima la Simba kitu alichodai kinachafua taswira ya Simba na kuleta sintofahamu miongoni mwa wanachama na mashabiki wao.
Kibadeni aliyeichukua timu hiyo baada ya Mfaransa Patric Liewig kutimuliwa alisema mkutano huo utafanyika majira ya saa 5 asubuhi ya kesho kwenye makao makuu ya klabu hiyo mtaa wa Msimbazi.
"Kuna baadhi ya wanahabari wamekuwa wakituchonganisha Simba, hivyo nimeitisha mkutano kesho nizungumze kuweka mambo sawa, kadhalika kuelezea maandalizi ya jumla dhidi ya pambano leo na Prisons," alisema Kibadeni maarufu kama King Mputa.
Kibadeni aliongeza kuwa, kuanza sasa wanahabari watakaotaka kujua chochote kuhusu Simba ni lazima wapate taarifa hizo kwa Msemaji wa Klabu, Ezekiel Kamwaga hata yale ya ufundi ambapo atakuwa anawauliza benchi la ufundi na kutoa majibu kwa wanahabari ili kuhofia kuivuruga Simba inayoongoza Ligi Kuu kwa sasa ikiwa na pointi 15.
Naye Msemaji wa Simba, Kamwaga alithibitisha kuwepo kwa mkutano huo wa kesho, akidai kocha wao hajafurahia na baadhi ya taarifa zinazoripotiwa zinazoonekana kama zina lengo la kuivuruga timu yao.

Hatimaye Mwananchi lamaliza kifungo kuanza kutoka tena kesho

GAZETI LA MWANANCHI LATOKA KIFUNGONI
Mkurugenzi Mtendaji wa Mwananchi Communications limited(MCL)Tido Mhando akizungumza na waandishi wa habari jijini kuhusu kuanza uchapishaji wa gazeti la Mwananchi kuanzia Oktoba 11, lililokuwa limefungiwa kwa wiki mbili. Kulia ni Mhariri Mtendaji wa Gazeti la Mwananchi, Denis Msacky na Meneja Masoko wa Kampuni hiyo,Bernard Mukasa.