STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, April 13, 2017

Messi aichanganya Argentina adhabu ya FIFA


WAMEPAGAWA. Kitendo cha nyota wa kimataifa wa Argentina, Lionel Messi kufungiwa mechi nne na Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) limewatia wazimu Waargentina kiasi Chama cha Soka nchini humo (AFA) kuamua kujitosa kumtetea.
Rais wa AFA, Claudio Tapia amefunga safari mpaka Hispania ili kujadili kesi inayuomkabili Messi, ambaye ndiye tegemeo na tumaini la nchini hiyo katika mbio zake za kucheza Fainali za Kombe la Dunia 2018.
Tapia alisisitiza safari ya kwenda nchini Hispania ni mahsusi kwa ajili ya kwenda kujadili kesi ya Lionel Messi ya kufungiwa mechi nne na Shirikisho la Soka Duniani-FIFA na sio kwenda kuzungumza na Jorge Sampaoli au Diego Simeone kuhusiana na kibarua cha kuinoa nchi hiyo.
Messi alilimwa adhabu hiyo na FIFA baada ya kumtolea kauli chafu mwamuzi wakati wa ushindi wa bao 1-0 Argentina iliyopata dhidi ya Chile mwezi uliopita na kumfanya kukosa mchezo waliofungwa na Bolivia mabao 2-0 na nyingine tatu zijazo za kufuzu Kombe la Dunia.
Nyota huyo wa Barcelona anayo nafasi ya kukata rufani ya kutaka kupunguzwa kwa adhabu hiyo mwezi ujao kitu ambacho Tapia alitaka kwenda kujadili naye ana kwa ana.
Tapia alisema FIFA imemtaka Messi kupeleka shauri lake hilo la kufungiwa mechi nne baada ya mchezo wao dhidi ya Chile Alhamisi Mei 4 mwaka huu hivyo ilikuwa muhimu kwenda kujadiliana naye kuhusiana na hilo.
Mchezo ujao wa Argentina utakuwa ni ule wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya Brazil utakaofanyika nchini Australia Juni mwaka huu huku mechi za kufuzu Kombe la Dunia zikitarajiwa kuendelea Agosti.

No comments:

Post a Comment