STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, April 13, 2017

Yanga wawafuata Waalgeria kwa mafungu

MABINGWA wa Soka nchini, Yanga wameondoka nchini kwa mafungu kundi la kwanza likitimka jioni hii na jingine linatarajiwa kuondoka usiku huu ili kuwahi pambano lao la Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya MC Alger ya Algeria.
Kundi la kwanza lilitimka saa 10 likitumia ndege ya Shirika la Emirates Air likiwa na wakuu wa benchi la ufundi chini ya Kocha George Lwandamina sambamba na nahodha Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Hassan Kessy, Said Juma ‘Makapu’, Simon Msuva, Geoffrey Mwashiuya, Juma Mahadhi na straika Amissi Tambwe ambao watapitia Dubai.
Mbali na Lwandamina wengine wa benchi la ufundi waliopo kwenye kundi hilo ni Wasaidizi wake, Juma Mwambusi, Kocha wa mazoezi ya utimamu wa mwili, Noel Mwandila kutoka zambia na kocha wa makipa, Juma Pondamali.
Pia kundi hilo lina Meneja Hafidh Ally, Daktari Edward Bavu na Mchua Misuli, Jacob Onyango.
Kundi la pili litafuatia muda mchache ujao litaondoka kwa Ndege ya Shirika la Uturuki likiwa na wachezaji 13 na baadhi ya Maofisa wa timu hiyo likipitia Istanbul ambao ni makipa; Deogratius Munishi ‘Dida’ na Beno Kakolanya; mabeki; Juma Abdul,  Mwinyi Mngwali, Andrew Vincent ‘Dante’ na Kevin Yondan.
Pia wamo viungo ni Thabani Kamusoko, Haruna Niyonzima, Deus Kaseke na Emmanuel Martin wakati mshambuliaji ni Donald ngoma. 
Wawakilishi hao walishinda mchezo wa awali jijini Dar es Salaam wiki iliyopita kwa bao 1-0 hivyo inahitaji sare ama kutofungwa zaidi ya mabao 2-1 ili kutinga makundi na kuwang;oa wenyeji wao MC Alger.
Yanga haijawahi kuitoa timu yoyote ya Afrika Kaskazini wala kupata ushindi ugenini katika nchi hizo, zaidi ya sare mbili ilizopata mwaka 1992 dhidi ya Ismailia ya Misri waliotoka nao 1-1 sawa na ile ya 2008 dhidi ya Al Alkhdar ya Libya.
Kama Yanga itapenya hapo itafuzu makundi ya michuano hiyo na kuweka rekodi kwa mara ya pili mfululizo kwani mwaka jana ilipenya, ikiwa chini ya Kocha Hans Pluijm ambaye alitimuliwa na kutua Singida United iliyopanda Ligi Kuu msimu ujao.

No comments:

Post a Comment