STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, April 13, 2017

Mabao ya Barcelona yampa ulaji Dyabala Juventus

SAA chache baada ya kuitia aibu Barcelona katika mechi ya Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, Straika wa Juventus, Paulo Dybala amesaini mkataba mpya na mabingwa hao wa Italia ambao utamalizika mwaka 2022.
Nyota huyo wa kimataifa wa Argentina mwenye umri wa miaka 23 ameifungia Juventus mabao 16 msimu huu na kulikuwa na tetesi zikimuhusisha na kuondoka. Dybala alijiunga Juventus kwa kitita cha Pauni 23 milioni kutoka Palermo na kupewa mkataba wa miaka mitano Juni 2015 na kufanikiwa kushinda mataji mawili mwaka jana.
Dybala alisema siku zote amekuwa akitaka kufanikiwa kwenye kila kitu na anafahamu Juventus ndio mahali sahihi kuwepo kama anataka kushinda mataji. Dybala amefunga mabao 39 na kusaidia mengine 16 kwenye mechi 82 toka ajiunge na Juventus, ikiwa ni dadi kubwa zaidi ya mchezaji yeyote katika klabu kwa muda aliojiunga.

No comments:

Post a Comment