STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, January 15, 2017

Manchester City aibu tupu, wapigwa 4-0

Picha zote kwa hisani ya Mirror
AIBU tupu. MANCHESTER City jioni hii imekumbana na aibu kubwa baada ya kutandikwa mabao 4-0 na Everton kwenye uwanja wa Goodson Park, mjini Liverpool.
City inayonolewa na Kocha Pep Guardioala kwa kipigo hicho imesalia nafasi ya tano ya msimamo na ikiwa katika hati hati ya kuzidiwa maarifa na watani zao wa Jiji la Manchester, Man United iwapo itafanikiwa kuifunga Liverpool kwa idadi kubwa ya mabao, kwani zinaweza kulingana na kuzidiana uwiano wa mabao.
United ina pointi 39 na mabao 31 ya kufunga na kufungwa 19 wakati City kwa kipigo cha jioni hii imesaliwa na pointi 42 na mabao 41 ya kufunga na kufungwa 26, ikiwa na maana wana uwiano tofauti na mabao matatu tu mpaka sasa.
Mabao yaliyoiangamiza City leo ikiwa kiigo chao cha tano msimu huu yalitumbukizwa na Romelu Lukaku dakika ya 34, Kevin Mirallas dakika 47', Tom Davies dakia ya 79 na chipukizi Ademola Lookman aliyefunga dakika za nyingeza za mpambano huo mkali ambao umemfanya Guardiola kujikuta kwenye simanzi kubwa.
Muda mchache ujao Man United itakuwa wenyeji wa Liverpool kwenye Uwanja wa Old Trafford, kwenye mchezo wao wa kwanza wa Ligi Kuu msimu huu timu hizo zilishindwa kutambiana kwa kutofungana. Mechi ilichezwa Oktoba 17, 2016.

No comments:

Post a Comment