STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, January 15, 2017

Carzola majanga matupu Arsenal, nje wiki 10 zaidi

MAJANGA. Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger anahofu kiungo wake nyota Santi Cazorla anaweza kukaa nje ya uwanja kwa wiki 10 zaidi kutokana na majeruhi ya kifundo cha mguu yanayomsumbua.
Nyota huyo wa kimataifa wa Hispania amekuwa nje ya uwanja toka Oktoba baada ya kucheza mechi 11 katika mashindano yote msimu huu. Lakini Cazorla mwenye umri wa miaka 32 sasa anategemewa kuendelea kukaa nje zaidi kutokana na majeruhi kupona taratibu kuliko ilivyotegemewa awali.
Wenger alisema Cazorla bado hajaanza hata kukimbia hivyo hadhani kama atarejea uwanjani hivi karibuni.

Imeelezwa huenda Wenger akafanya mpango wa kusajili mbadala wake.
Klabu hiyo jana Jumamosi ilivaana na Swansea City na kupata ushindi wa mabao 4-0 ugenini katika mbio za ubingwa wa Ligi Kuu ya England.

No comments:

Post a Comment