STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, January 15, 2017

Beki Mholanzi akichonganisha Chelsea na Man United

Beki Stefan De Vrij
LAZIMA kieleweke. Klabu za Chelsea na Manchester United zimedaiwa kuingia vitani kwa ajili ya kusaka saini ya beki wa Lazio, Stefan De Vrij.
Duru za kisoka zinasema kuwa, Chelsea imejipanga kupambana na Man United katika kipindi cha kiangazi kwa ajili ya kumwania beki huyo wa kimataifa wa Uholanzi ambaye kwa muda mrefu amekuwa akiwindwa na Mashetani Wekundu.
Chelsea inadaiwa nao wako tayari kuingia katika kinyang’anyiro hicho, huku klabu yake ya Lazia imeondoa uwezekano wa kumuuza beki huyo katika kipindi hiki cha usajili wa dirisha dogo.
Hatua hiyo imetoa mwanya kwa klabu hiyo kuweka kitita cha Euro milioni 40 kwa timu itakayomhitaji majira ya kiangazi, ambapo klabu yoyote kati ya Man United ama Chelsea wakituliza kichwa inaweza kueleweka kwao kwa beki huyo.

No comments:

Post a Comment