STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, January 15, 2017

PSG yaingia vita ya kumnasa Depay wa Man United

Memphis Depay
PSG nayo imoooo! Klabu ya Paris Saint-Germain ya Ufaransa, imedaiwa nayo kuingia kwenye mbio za kumwania winga wa Manchester United, Mholanzi Memphis Depay.
Meneja wa United Jose Mourinho tayari ameshamwambia winga huyo kutafuta timu nyingine, huku Everton na Olympique Lyon zote zikitajwa kumtaka.
PSG walikaribia kumsajili Depay kabla hajakwenda Old Trafford kwa kitita cha Pauni milioni 25 mwaka 2015, lakini sasa wanaonekana kumhitaji tena mchezaji huyo ambaye hajacheza katika kikosi cha United toka Novemba mwaka jana. United inataka kitita cha Paundi milioni 15 kwa Depay baada ya kukataa ofa ya Paundi milioni 10 iliyotolewa na Everton inayoshiriki Ligi Kuu ya England.

No comments:

Post a Comment