STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 6, 2017

Simba yabanwa, Yanga ikiisubiri nusu fainali Mapinduzi Cup


Benchi la Simba likifuatilia moja ya mechi zao za Mapinduzi Cup 2017
Yanga kabla ya mechi yao ya Jamhuri Pemba
NA RAHMA WHITE, Z'BAR
SIMBA, jana usiku ilishikwa shati na Watoza Ushuru wa Uganda, URA, lakini kesho Jumamosi kutakuwa na kazi kubwa itakayozikutanisha timu za Yanga na Azam ili kuamua hatma ya Kundi B katika Kombe la Mapinduzi 2017.
Michuano hiyo inayoendelea usiku wa leo kwa pambano moja tu la Kundi A kati ya Taifa Jang'ombe 'Wakombozi wa Ng'ambo dhidi ya KVZ, inachezwa kwenye Uwanja wa Amaana, Zanzibar na jana Simba ilitoka suluhu na URA.
Kwa matokeo hayo Simba imeendelea kuongoza kundi A ikiwa na pointi saba baada ya kushushwa kwa muda katika nafasi hiyo na Jang'ombe Boys ambayo jioni ya jana ilipata ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya KVZ.
Katika pambano hilo la mapema, Abdul Samad Kassim Hasgut alikuwa mchezaji wa kwanza kwa msimu huu kufunga hat trick wakati wakiizamisha KVZ ambayo ilitangulia kupata bao dakika ya tano tu kupitia Salum Songoro.
Hata hivyo kazi ipo kesho asikuambie mtu, Yanga na Azam zitavaana kuamua nani aongoze kundi ili kuelekea mechi za njusu fainali zitakazopigwa wiki ijayo.
Yanga inaongoza msimamo wa kundi hilo ikiwa na pointi sita huku Azam ikiwa nyuma yao na pointi zao nne na Jamhuri ni ya tatu ikiwa na pointi moja ambapo mapema jioni ya kesho itavaana na Zimamoto ambayo imeshaaga mashindano hayo mapema kwa kupigwa mechi zao mbili za awali.
Pambano la Yanga na Azam linavuta hisia kubwa kutokana na ushindani uliopo baina ya timu hiyo, japo safari hii Azam inaonekana wanyonge kwa kufanya vibaya katika Ligi Kuu Bara na juzi kati ilibanwa mbavu na Jamhuri na kutoka nao suluhu. Jamhuri ilitunguliwa na Yanga mabao 6-0 katika mechi yao ya kwanza na wengi walidhani Azam ingefuata nyayo hizo, lakini ikajikuta ikiomba pambano limalizike kwa namna Jamhuri walivyowakimbiza uwanjani.
Matokeo yoyote kwa Yanga mbali na kipigo yataifa uongozi wa kundi hilo na kusikiliza mechi za keshokutwa Jumapili za Kundi A ili kujua itavaana na nani kwenye hatua ya nusu fainali.
Jumapili vinara wa Kundi A, Simba itavaana na Jang'ombe Boys iliyopo nafasi ya pili majira ya usiku na mapema jioni ya siku hiyo URA iliyopo nafasi ya tatu itamaliza kazi dhidi ya Taifa Jang'ombe.
Matokeo yoyote ya kundi hilo yanaweza kuzifusha timu za Simba, Jang'ombe Boys, URA  na hata Taifa jang;ombe kucheza nusu fainali na moja yao itakuwa na nafasi ya kuvaana na Yanga ambayo katika mechi mbili za awali imeshinda kwa mabao nane huku wavu wao ukiwa haujaguswa tofauti na wapinzani wa kundi hilo la A.
Mechi za wikiendi hii za kukamilishia hatua ya makundi za michuano hiyo ndizo zitakazoamua timu zipi tatu za mwisho za kuungana na Yanga iliyotangulia mapema kucheza nusu fainali.

Mambo yalivyo Kombe la Mapinduzi 2017

Des 30, 2016
Taifa Jang'ombe 1-0 Jang'ombe Boys (Seif Hassan 'Banda')

Jan 01, 2017
URA 2-0 KVZ  (Bokota Labama  57', 90')
Taifa Jang'ombe 1-2 Simba (Mzamiru 27', Liuzio 41'; Lufunga 76 Og)

Jan 02, 2017
Azam 1-0 Zimamoto (Shaaban Idd 79')
Yanga 6-0 Jamhuri (Msuva 19', 40', Ngoma 23', 37', Kamusoko 59', Mahadh 85')

Jan 03, 2017
URA 1-2 Jang'ombe Boys (Bokota Labama 31'; Khamis Makame '19', 51')
KVZ 0-1 Simba (Mzamiru 44')

Jan 04, 2017
Yanga 2-0 Zimamoto (Msuva 11', 21')
Azam 0-0 Jamhuri

Jan 05, 2017
KVZ 1-3 Jang'ombe Boys (Salum Songoro 5'; Abdul Kassim 20', 35', 45)
Simba 0-0 URA

Ratiba ilivyo sasa


Leo Ijumaa

Taifa Jang'ombe v KVZ Saa 2:30 usiku

Kesho Jumamosi

Jamhuri v Zimamoto Saa 10:00 jioni
Azam v Yanga Saa 2:30 usiku

Jumapili Jan 08, 2017

Simba v Jang'ombe Boys Saa 10:00 jioni
Taifa Jang'ombe v  URA Saa 2:30 usiku

Jan 10, 2017
Nusu Fainali

Mshindi A v Wa Pili B Saa 10:00 jioni
Mshindi B v Wa Pili A Saa 2:30 usiku

Jan 13, 2017

Mshindi NF1 v Mshindi NF2 Saa 2:30

Msimamo
Kundi A:
                         P  W  D  L  F  A  Pts
1. Simba           3   2   1   0  3  1   7
2. Jang'ombe     3   2   0  1   5  3   6
3.  URA             3   1   1  1   3  2   4
4. Taifa              2   1   0  1   2  3   3
5. KVZ               3   0   0  3   1  6   0

Kundi B
                       P  W  D  L  F  A  Pts
1. Yanga           2   2   0  0  8  0  6
2. Azam            2   1  1   0  1  0  4
3. Jamhuri        2   0   1   1  0  6  1
4. Zimamoto     2   0   0   2  0  3  0

Wafungaji:
4 Simon Msuva         (Yanga)
3 Bokota Labama     (URA)
   Abdul Kassim 'Hasgut' (Jang'ombe)
2 Khamis Makame    (Jang'ombe)
   Donald Ngoma      (Yanga)
   Mzamiru Yassin     (Simba)
1 Seif Hassan 'Banda' (Taifa)
   Juma Liuzio            (Simba)
   Laudit Lufunga  o.g (Simba)
   Thabani Kamusoko(Yanga)
   Bakar Mahadhi        (Yanga)
   Shaaban Idd            (Azam)

Orodha ya Mabingwa wa Mapinduzi
Mwaka     Bingwa            Mshindi wa Pili
2007         Yanga SC          Mtibwa Sugar
2008         Simba SC          Mtibwa Sugar
2009         Miembeni          KMKM
2010         Mtibwa Sugar    Ocean View
2011         Simba SC          Yanga SC
2012         Azam FC           Simba SC
2013         Azam FC           Tusker FC
2014         KCCA                Simba SC
2015         Simba SC          Mtibwa Sugar
2016         URA                  Mtibwa Sugar
2017          ??                          ??

No comments:

Post a Comment