STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 6, 2017

Hebu msikieni Gerard Pique na ulalamishi wake

Wachezaji wa Barcelona wakimlalamikia mwamuzi katika mechi yao ya jana dhidi ya Atheltico Club
Beki Gerard Pique akisikitika akiwa nyavuni wakati timu yake ikipokea kipigo cha mabao 2-1.
KUMBE wepesiiii. Barcelona wameuanza mwaka vibaya baada ya kujikuta wakitunguliwa mabao 2-1 na Athletico Club, huku beki wake Gerard Pique akitupa lawama kwa waamuzi wa pambano hilo.
Pique amedai kuwa waamuzi nchini Hispania wanawapendelea mahasimu wao wakuu, Real Madrid baada ya klabu hiyo kuchapwa katika mchezo wa Kombe la Mfalme uliochezwa usiku wa jana.
Barcelona walilalamikia penalti mbili, moja iliyomhusisha Neymar na nyingine Pique, ambazo zilikataliwa katika mchezo huo wa mkondo wa kwanza hatua ya timu 16 bora, ingawa baadae wenyeji Bilbao walipoteza wachezaji wawili kwa kadi nyekundu Raul Garcia na Ander Iturraspe.
Akihojiwa beki huyo wa kimataifa wa Hispania alisema penalti hizo zilikuwa za wazi kabisa, lakini anadhani wanajua kwanini wanafanyiwa hivyo.
Pique aliendelea kudai kuwa waamuzi wamekuwa wakiwakwamisha kwa kuonyesha upendeleo kwa Madrid akitolea mfano wa mechi yao ya jana dhidi ya Sevilla ambayo walishinda mabao 3-0.

No comments:

Post a Comment