STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 6, 2017

Real Madrid achana nayo, yamtumia Morata kama chambo Juventus

Alvaro Morata kama chambo kwa Juventus

Paulo Dyabala anayewindwa Real Madrid
SIO Mchezo! Klabu ya Real Madrid imepanga kumtumia Alvaro Morata kama chambo cha kuweza kumnasa nyota wa kimataifa wa Juventus, Paulo Dyabala.
Inadaiwa kuwa klabu hiyo imepanga kutoa kitita cha fedha pamoja na Morata ilimradi imbeba Dybala.
Kwa mujibu wa gazeti la The Sun, Madrid imetoa ofa ya Pauni Milioni 77 sambamba na straika wake mkali aliyewahi kuichezea Juventus kwa misimu miwili ya mkataba maalum, Alvaro Morata, ili imnase Muargentina huyo anayetisha kwa mabao Italia.
Hata hivyo mabosi wa Los Blancos wamefichua kuwa wapo tayari pia kuipa Juventus ama Toni Kroos ama Luca Modric, ili mradi dili la Dybala lijipe.
Mkuregenzi wa Juventus, Giuseppe Marotta amedaiwa kugomea mipango hiyo ya Mabingwa wa Dunia, akitaka kumbakisha nyota wao huyo mwenye miaka 23 aliyekuwa miongoni mwa waliokluwa wakiwania tuzo ya Ballon d'Or.
Licha ya msimamo huo wa Blanconeri, wanaoongoza msimamo wa Ligi Kuu ya Italia, Serie A, bado hawaaminiki kwa sababu ya kuwa na kauli za kisiasa, kwani kuna wakati wanadai hawauzi mchezaji, lakini ikiwa kama njaa ya kutaka kufanya biashara yenye faida. Hata kwa Paul Pogba walinukuliwa kutoa msimamo kama huo, lakini mwishowe walimuuza kwa Man United kwa kitita kinono kinachoshikilia rekodi kwa sasa barani Ulaya.

No comments:

Post a Comment