STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 6, 2017

Msuva mkimchekea tu, kabeba mwanangu!

Msuva Kulia akiwajibika katika mechi za Ligi Kuu Bara dhidi ya Azam. Timu hizo kesho zitavaana kwenye Kombe la Mapinduzi visiwani Zanzibar.
UMEIANGALIA orodha ya Wafungaji Bora wa sasa wa michuano ya Kombe la Mapinduzi? Jina la Simon Msuva bila shaka ndilo linaloongoza kwa sasa akiwa ametupia kambani mabao manne.
Sasa kama hujui, idadi hiyo ya mabao aliyonayo sasa ndiyo iliyompa tuzo Mwaka 2015 alipochaguliwa kuwa Mfungaji Bora akiwafunika wakali wengine.
Msuva kwa sasa anaongoza orodha hiyo na kama kesho Jumamosi atatupia tena kambani kuna uwezekano mkubwa wa kuweka rekodi ya kuwa mchezaji wa kwanza kufunga mabao mengi kwenye michuano hiyo iliyoasisiwa 2007.
Michuano ya Mapinduzi kwa mwaka jana wa 2016, Peter Lwasa wa URA ndiye aliyekuwa Mfungaji Bora akitupia kimiani mabao matatu.
Msuva amekiri kwamba kiu yake katika michuano ya mwaka huu ni kuona anaibuka Mfungaji Bora na hata kunyakua Mchezaji Bora na kuisaidia pia Yanga kubeba taji lao la pili la michuano hiyo inayoendelea visiwani Zanzibar.
Mpaka sasa Msuva amafukuziwa kwa karibu na wachezaji wawili, Abdul-Samad Kassim wa Jang'ombe Boys aliyepiga hat trick ya kwanza katika michuano hiyo na Bokota Labama wa URA-Uganga wenye mabao matatu kila mmoja.
Kwenye michuano ya mwaka huu Mfungaji Bora na Mchezaji Bora atazawadiwa kila mmoja kitita cha Sh. 1 milioni moja kama atakachopewa Kipa Bora, Mchezaji Bora Chipukizi, Mwamuzi Bora na Kocha Bora, fedha ambazo zimetolewa na mmoja wa Wajumbe wa Kamati ya Usajili ya Yanga, Khamis Chuma.

Orodha ya Wafungaji;

4 Simon Msuva                     (Yanga)
3 Bokota Labama                    (URA)
   Abdul Kassim 'Hasgut' (Jang'ombe)
2 Khamis Makame         (Jang'ombe)
   Donald Ngoma                  (Yanga)
   Mzamiru Yassin                 (Simba)
1 Seif Hassan 'Banda'             (Taifa)
   Juma Liuzio                      (Simba)
   Laudit Lufunga  o.g           (Simba)
   Thabani Kamusoko            (Yanga)
   Bakar Mahadhi                  (Yanga)
   Shaaban Idd                      (Azam)

   Salum Songoro                    (KVZ)

No comments:

Post a Comment