STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 6, 2017

Kocha Mourinho kiroho safi ongezeko la timu WC

AMEKUBALI. Kocha wa klabu ya Manchester United, Jose Mourinho 'Special One', amekuwa kocha wa kwanza kuunga  mkono mapendekezo ya kuongeza timu kufikia 48 katika Kombe la Dunia akiamini kuwa wachezaji watalindwa vyema.
Rais wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA, Gianni Infantino ana matumaini mpango wake kuwa na makundi 16 yenye timu tatu kuanzia michuano ya mwaka 2026 utapitishwa wakati wa kikao cha kamati ya utendaji ya shirikisho hilo wiki ijayo.
Muungano wa Klabu Ulaya ambao United pia ni mjumbe wake, tayari wameshaonyesha kutounga mkono pendekezo hilo, lakini Kocha Mourinho yeye anaunga mkono.
Akihojiwa kuhusiana na suala hilo, Mourinho alisema anaunga mkono kwa vile ana uhakika FIFA itazingatia maslahi ya wachezaji kwa kutowachezesha mechi nyingi zaidi kuliko sasa.

No comments:

Post a Comment